mayenga
JF-Expert Member
- Sep 6, 2009
- 4,118
- 1,973
Wakati juhudi za kupambana na janga hili zikiendelea,kuna mambo ya msingi na muhimu kama nchi nahisi hayajaenda sawa. Kwa haraka haraka na bila kuchelewa nashauri serikali kufanya mambo yafuatayo:
1. Upo uhaba wa vitendea kazi kwa watumishi zikiwemo Mask aina N95 ambazo kwa mujibu wa Naibu Waziri wa afya,ni watumishi tu wanatakiwa kuzivaa, serikali itaifishe mask za aina hii kwenye maduka yote nchini ikiwemo kuzikusanya na kuzipeleka kwenye bohari za dawa.
2. Mheshimiwa Rais amezungumza wazi kuhusu baa la njaa. Hali ya hewa tuliyonayo ni uhalisia kuwa hakuna uwezekano wa kuwa na chakula cha kutosha muda mfupi ujao.Serikali ichukue hatua haraka na kuzuia kusafirisha chakula nje ya nchi. Hii itegemee na uhalisia wa uwepo wa chakula kwenye ghala la taifa walau cha miezi 10 mpaka 12.
3. Budget ya dharura wizara ya afya ipitishwe ikiwemo kununua vipimo vya COVID-19 na kila mkoa uwe nayo ili kubaini hali halisi.
4. Vifaa vikishakuwepo tuwe na mandatory testing kwa raia wote ili kuwa na takwimu sahihi na pengine kuzuia kasi ya kuendelea kuenezeana.
5.Serikali ifuate ushauri wa Spika kuepuka nchi kuwa kwenye confusion.Leo hii matamko ya ugonjwa huu ni mengi.Tuwe na one stop centre badala ya kuwaacha wakuu wa wilaya,wakuu wa mikoa, mawaziri,maaskari kila mtu anakuja na tamko lake.Mfano kwa sasa watu wa Dar es Salaam hawatakiwi Iringa.
7. Mpaka sasa hatuna COVID-19 Protective and Prevention Rregulations ambazo pengine ndo ungekuwa msaafu na rejea kwa viongozi na watumishi.Kanuni hizi Zitungwe upesi sana.
8. Viwanda vyetu vya ndani-SIDO vianze mara moja kuzalisha bidhaa kama barakoa zenye kiwango na kuwauzia watu kwa bei ambayo wataimudu.Hii itasaidia kuepusha kila mtu kutengeneza barakoa zisizo na kiwango.
9. Kuna haja ya kurudisha kwa muda tume ya Bei (Price Regulation Commission) ili kudhibiti upandaji holela wa vyakula na bidhaa muhimu maana kila mtu yuko kwenye taharuki na huo umekuwa mwanya kwa wafanyabiashara kupamdisha bei maradufu.
10. Kuna baadhi ya watumishi wa umma nadhani sasa watumbuliwe maana kwa matamshi yao hawatusaidii kama taifa.
1. Upo uhaba wa vitendea kazi kwa watumishi zikiwemo Mask aina N95 ambazo kwa mujibu wa Naibu Waziri wa afya,ni watumishi tu wanatakiwa kuzivaa, serikali itaifishe mask za aina hii kwenye maduka yote nchini ikiwemo kuzikusanya na kuzipeleka kwenye bohari za dawa.
2. Mheshimiwa Rais amezungumza wazi kuhusu baa la njaa. Hali ya hewa tuliyonayo ni uhalisia kuwa hakuna uwezekano wa kuwa na chakula cha kutosha muda mfupi ujao.Serikali ichukue hatua haraka na kuzuia kusafirisha chakula nje ya nchi. Hii itegemee na uhalisia wa uwepo wa chakula kwenye ghala la taifa walau cha miezi 10 mpaka 12.
3. Budget ya dharura wizara ya afya ipitishwe ikiwemo kununua vipimo vya COVID-19 na kila mkoa uwe nayo ili kubaini hali halisi.
4. Vifaa vikishakuwepo tuwe na mandatory testing kwa raia wote ili kuwa na takwimu sahihi na pengine kuzuia kasi ya kuendelea kuenezeana.
5.Serikali ifuate ushauri wa Spika kuepuka nchi kuwa kwenye confusion.Leo hii matamko ya ugonjwa huu ni mengi.Tuwe na one stop centre badala ya kuwaacha wakuu wa wilaya,wakuu wa mikoa, mawaziri,maaskari kila mtu anakuja na tamko lake.Mfano kwa sasa watu wa Dar es Salaam hawatakiwi Iringa.
7. Mpaka sasa hatuna COVID-19 Protective and Prevention Rregulations ambazo pengine ndo ungekuwa msaafu na rejea kwa viongozi na watumishi.Kanuni hizi Zitungwe upesi sana.
8. Viwanda vyetu vya ndani-SIDO vianze mara moja kuzalisha bidhaa kama barakoa zenye kiwango na kuwauzia watu kwa bei ambayo wataimudu.Hii itasaidia kuepusha kila mtu kutengeneza barakoa zisizo na kiwango.
9. Kuna haja ya kurudisha kwa muda tume ya Bei (Price Regulation Commission) ili kudhibiti upandaji holela wa vyakula na bidhaa muhimu maana kila mtu yuko kwenye taharuki na huo umekuwa mwanya kwa wafanyabiashara kupamdisha bei maradufu.
10. Kuna baadhi ya watumishi wa umma nadhani sasa watumbuliwe maana kwa matamshi yao hawatusaidii kama taifa.