SERIKALI HAINA FEDHA

SERIKALI HAINA FEDHA

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,739
Reaction score
4,933
MAHITAJI YA SHIRIKISHO LA VYAMA VYA WAFANYAKAZI TANZANIA NI MZIGO WETU SOTE NA SIYO SERIKALI PEKE YAKE.
Kutokana na ukweli kuwa hakuna jipya chini ya jua. Leo baada ya kufuatilia maadhimisho ya siku ya kimataifa ya wafanyakazi Duniani nililazimika kukaa katika maktaba yangu nyumbani na kutafuta kitabu ambacho kiingeweza kunionesha mtazamo wa Taifa ulivyokuwa mwanzo na kinachofanyika leo. Kwa haraka nilikiona Kitabu cha UJAMAA" Kilichoandikwa na Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka 1968 na nilijaribu kukipitia hususan kuanzia uk 17-25 ndipo nilipopata mawazo na msukumo wa kuandika haya unayoyasoma.

Kuna kosa kubwa ambalo Taifa letu lilishalifanya juu ya kuchagu silaha ya kupambana na unyonge wetu. Kosa hili mpaka leo linaendelea licha ya miaka mingi kupita. Ni kama tulikosea na tukaamua kuendelea kukosea. TUCTA walichokitamka leo kama hitaji la wafanyakazi siyo kipya ila ni7 muendelezo wa kosa lile lile.

Katika kitabu hiki cha Ujamaa uk. 17 na 18 "...ni dhahiri kwamba tumefanya makosa katika kuchagua silaha; kwani silaha tuliyoichagua ni fedha. Tunataka kuondoa unyonge wetu kwa kutumia silaha ambayo sisi wenyewe hatuna. Katika mawazo yetu na vitendo vyetu ni kama tumemkata shauri kwamba bila fedha mapinduzi Mapinduzi haiwezekani. Ni kama tumesema Fedha ndiyo msingi wa maendeleo. Bila fedha hakuna maendeleo".

Ukiangalia kwa kina utagundua hali hii leo umekuwa kama imani kwa viongozi wa Serikali, wanasiasa na watumishi. Maombi makuu kwa Serikali ni "FEDHA". Ni kama tumeafikiana kuwa "Tukipata fedha tutaendelea, bila fedha hatutaendelea".

Mbunge akisimama bungeni kuwakilisha wananchi anaowaongoza hutaja mipango inayoitaka Serikali kutoa fedha. Kiongozi wa chama au shirikisho la wafanyakazi mara kadhaa huikumbusha Serikali kuongeza kima cha mishahara na kuboresha miundombinu ya kazi ambayo kwa kweli huhitaji fedha.

Mawaziri kila mwaka hufanya makadirio ya matumizi na kuonesha fedha wanazohitaji ili kutekeleza mipango ya maendeleo isipokuwa Waziri mmoja tu, Waziri wa fedha ambaye hushughulika na hesabu za makadirio ya mapato. Hi ni sawa na kusema wengine wote wao hufanya hesabu za makadirio ya matumizi.

Serikali kusema haina fedha siyo jibu jipya. Katika kitabu hiki cha Ujamaa( uk.20) "...kusema Serikali haina fedha maana yake Wananchi hawana fedha". Kumbe tunaposema fedha maana yake zipo mifuko I mwa wanachi na tunapoidai Serikali fedha zaidi ni sawa na kutaka fedh tulizo nazo sisi (yaani, mimi na wewe) zitumike zaidi.

Kwa maana nyingine tunapohitaji serikali itoe fedha zaidi ni sawa na kukubali kuwa kiasi cha kodi inayochukua serikali ni kidogo mno na hakiwezi kuendesha masuala mengi yanayohitaji fedha, hivyo iongeze kututoza kodi mara dufu. Ni ngumu kulipokea hili lakini lilishasemwa na ndivyo ilivyo.

Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambrage Nyerere aliutoa pia mfano huu "..kukataa kodi na kutaka Serikali iongeze fedha ni sawa na kudai maziwa zaidi bila kutaka ng'ombe akamuliwe tena.
..................................................................................................................................
Siku njema ya Wafanyakazi Duniani.
"NG'OMBE HANA MAZIWA ZAIDI"
..............
"Jambo letu lipo"
 
Bora mshahara uongezwe hata kama kodi inaongezeka zaidi kuliko kodi na tozo kuongezeka wakati mshahara uko palepale.
 
Bora mshahara uongezwe hata kama kodi inaongezeka zaidi kuliko kodi na tozo kuongezeka wakati mshahara uko palepale.
Mahitaji ya fedha lakini ni mengi Mkuu na yote tunaomba Serikali fedha.
 
Fedha zote walizozikuta hazina wameshazimaliza zote, Raisi wenu anakwenda Dubai na msururu kwa ndege ya kukodi, juzi kati kaishi USA karibia wiki 2 na umati mzima kwa ndege ya kukodi hao wote wanahudumiwa kila kitu, Makamba kachukuwa 30 Million dollars kutoka Serikalini, sasa nini kimebakia ? Hela ya kulipa Wafanyakazi itatokea wapi ?
 
Fedha zote walizozikuta hazina wameshazimaliza zote, Raisi wenu anakwenda Dubai na msururu kwa ndege ya kukodi, juzi kati kaishi USA karibia wiki 2 na umati mzima kwa ndege ya kukodi hao wote wanahudumiwa kila kitu, Makamba kachukuwa 30 Million dollars kutoka Serikalini, sasa nini kimebakia ? Hela ya kulipa Wafanyakazi itatokea wapi ?

Fedha zote walizozikuta hazina wameshazimaliza zote, Raisi wenu anakwenda Dubai na msururu kwa ndege ya kukodi, juzi kati kaishi USA karibia wiki 2 na umati mzima kwa ndege ya kukodi hao wote wanahudumiwa kila kitu, Makamba kachukuwa 30 Million dollars kutoka Serikalini, sasa nini kimebakia ? Hela ya kulipa Wafanyakazi itatokea wapi ?
Hapo ulipobold pana uzito kidogo...ni strong statement, unaweza kupashehenesha kidogo?
 
MAHITAJI YA SHIRIKISHO LA VYAMA VYA WAFANYAKAZI TANZANIA NI MZIGO WETU SOTE NA SIYO SERIKALI PEKE YAKE.
Kutokana na ukweli kuwa hakuna jipya chini ya jua. Leo baada ya kufuatilia maadhimisho ya siku ya kimataifa ya wafanyakazi Duniani nililazimika kukaa katika maktaba yangu nyumbani na kutafuta kitabu ambacho kiingeweza kunionesha mtazamo wa Taifa ulivyokuwa mwanzo na kinachofanyika leo. Kwa haraka nilikiona Kitabu cha UJAMAA" Kilichoandikwa na Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka 1968 na nilijaribu kukipitia hususan kuanzia uk 17-25 ndipo nilipopata mawazo na msukumo wa kuandika haya unayoyasoma.

Kuna kosa kubwa ambalo Taifa letu lilishalifanya juu ya kuchagu silaha ya kupambana na unyonge wetu. Kosa hili mpaka leo linaendelea licha ya miaka mingi kupita. Ni kama tulikosea na tukaamua kuendelea kukosea. TUCTA walichokitamka leo kama hitaji la wafanyakazi siyo kipya ila ni7 muendelezo wa kosa lile lile.

Katika kitabu hiki cha Ujamaa uk. 17 na 18 "...ni dhahiri kwamba tumefanya makosa katika kuchagua silaha; kwani silaha tuliyoichagua ni fedha. Tunataka kuondoa unyonge wetu kwa kutumia silaha ambayo sisi wenyewe hatuna. Katika mawazo yetu na vitendo vyetu ni kama tumemkata shauri kwamba bila fedha mapinduzi Mapinduzi haiwezekani. Ni kama tumesema Fedha ndiyo msingi wa maendeleo. Bila fedha hakuna maendeleo".

Ukiangalia kwa kina utagundua hali hii leo umekuwa kama imani kwa viongozi wa Serikali, wanasiasa na watumishi. Maombi makuu kwa Serikali ni "FEDHA". Ni kama tumeafikiana kuwa "Tukipata fedha tutaendelea, bila fedha hatutaendelea".

Mbunge akisimama bungeni kuwakilisha wananchi anaowaongoza hutaja mipango inayoitaka Serikali kutoa fedha. Kiongozi wa chama au shirikisho la wafanyakazi mara kadhaa huikumbusha Serikali kuongeza kima cha mishahara na kuboresha miundombinu ya kazi ambayo kwa kweli huhitaji fedha.

Mawaziri kila mwaka hufanya makadirio ya matumizi na kuonesha fedha wanazohitaji ili kutekeleza mipango ya maendeleo isipokuwa Waziri mmoja tu, Waziri wa fedha ambaye hushughulika na hesabu za makadirio ya mapato. Hi ni sawa na kusema wengine wote wao hufanya hesabu za makadirio ya matumizi.

Serikali kusema haina fedha siyo jibu jipya. Katika kitabu hiki cha Ujamaa( uk.20) "...kusema Serikali haina fedha maana yake Wananchi hawana fedha". Kumbe tunaposema fedha maana yake zipo mifuko I mwa wanachi na tunapoidai Serikali fedha zaidi ni sawa na kutaka fedh tulizo nazo sisi (yaani, mimi na wewe) zitumike zaidi.

Kwa maana nyingine tunapohitaji serikali itoe fedha zaidi ni sawa na kukubali kuwa kiasi cha kodi inayochukua serikali ni kidogo mno na hakiwezi kuendesha masuala mengi yanayohitaji fedha, hivyo iongeze kututoza kodi mara dufu. Ni ngumu kulipokea hili lakini lilishasemwa na ndivyo ilivyo.

Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambrage Nyerere aliutoa pia mfano huu "..kukataa kodi na kutaka Serikali iongeze fedha ni sawa na kudai maziwa zaidi bila kutaka ng'ombe akamuliwe tena.
..................................................................................................................................
Siku njema ya Wafanyakazi Duniani.
"NG'OMBE HANA MAZIWA ZAIDI"
..............
"Jambo letu lipo"

Unajaribu kujustify Serikali kutowajibika , hiyo ni dalili kuwa unajipendekeza!! Kama Serikali ya jirani yetu Kenya mwaka huu tu wamepandisha minimum wage by 12%; how are they different from us?
The main difference is that they have a constitution that obliges the government to be accountable to the people! Wameweza kuthibiti matumizi ya hovyo ya Serikali yao hivyo Serikali inauwezo wa kuongeza mishshara. Samia anazurura zurula tu na hii corona iliyozagaa Duniani; huku nyuma chawa wake wanakula kihenge halafu akirudi anasingizia Vita ya Putin kushindwa kuongeza mishahara!!! Ameshindwa kuiongoza serikali kuthibiti matumizi!
Halafu kesho kutwa anakwea pipa Kwenda Canada badala ya kufanya mazungumzo kwa ZOOM hivyo kuokoa matumizi yasiyokuwa ya lazima!! She is being manipulated.
 
Kwa tu aoelewa tunajua mama mwaka jana alipotamka mwaka huu atakuja na package nzuri ulikua ni mshawasha wa urais, alikua anadhani anaweza kuropoka chochote na lolote sasa amekutana na hali halisi amechanganyikiwa.

Mapato ya serikali kwa mwezi ni Trilioni 1.6, wage bill ya serikali bilioni 600, foreign debt service 700B, Matumizi ya kawaida ya serikali ni zaidi ya 500B, tayari una pungufu ya zaidi ya 200B. Ukiongeza mshahara hata 5% ya wage bill yako inakimbilia 700B, unazidi kuongeza deficit gap.

Hapo hatujazungumzia mikopo ya elimu ya Juu, madawa na vifaa tiba, ujenzi wa miundombinu na ukarabati wa miundombinu, rushwa, matumizi yasiyo ya lazima kama hayo ya kwenda Dubai Expo, royal tour, nk.

Huyu mama wakati anaongea mwaka jana tunaojua uhalisia tulisema hizi ni mshawasha wa urais tu.

Mwaka 2019 waalimu waliongezewa mshahara kati ya shilingi elfu 2 hadi elfu 15, hicho ndio kinafuata mwaka mpya wa fedha kwa watumishi wote.

Tusubiri.
 
Unajaribu kujustify Serikali kutowajibika , hiyo ni dalili kuwa unajipendekeza!! Kama Serikali ya jirani yetu Kenya mwaka huu tu wamepandisha minimum wage by 12%; how are they different from us?
The main difference is that they have a constitution that obliges the government to be accountable to the people! Wameweza kuthibiti matumizi ya hovyo ya Serikali yao hivyo Serikali inauwezo wa kuongeza mishshara. Samia anazurura zurula tu na hii corona iliyozagaa Duniani; huku nyuma chawa wake wanakula kihenge halafu akirudi anasingizia Vita ya Putin kushindwa kuongeza mishahara!!!
Halafu kesho kutwa anakwea pipa Kwenda Canada badala ya kufanya mazungumzo kwa ZOOM hivyo kuokoa matumizi yasiyokuwa ya lazima!! She is being manipulated.
Maneno mengi niliyoyaandika hapo nimenukuu katika kitabu cha Ujamaa cha mwaka 1968 kilichoandikwa na Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Lengo hasa ni kuonesha misingi ya haya tunayoyaona leo na siyo kujipendekeza. Nikutoe shaka kabisa, sina tabia hiyo ya kujipendekeza ila napenda sana kuwa na mawazo huru ambayo mtu yeyote anaweza kuutazama kwa mtazamo wake. Simzuii mtu kuona aonacho.

Umetua mchango mzuri sana kwenye hoja yako. Ni kweli ipobkila sababu ya kupunguza matumizi ya Serikali yasiyokuwa ya lazima.
 
Kwa tu aoelewa tunajua mama mwaka jana alipotamka mwaka huu atakuja na package nzuri ulikua ni mshawasha wa urais, alikua anadhani anaweza kuropoka chochote na lolote sasa amekutana na hali halisi amechanganyikiwa.

Mapato ya serikali kwa mwezi ni Trilioni 1.6, wage bill ya serikali bilioni 600, foreign debt service 700B, Matumizi ya kawaida ya serikali ni zaidi ya 500B, tayari una pungufu ya zaidi ya 200B. Ukiongeza mshahara hata 5% ya wage bill yako inakimbilia 700B, unazidi kuongeza deficit gap.

Hapo hatujazungumzia mikopo ya elimu ya Juu, madawa na vifaa tiba, ujenzi wa miundombinu na ukarabati wa miundombinu, rushwa, matumizi yasiyo ya lazima kama hayo ya kwenda Dubai Expo, royal tour, nk.

Huyu mama wakati anaongea mwaka jana tunaojua uhalisia tulisema hizi ni mshawasha wa urais tu.

Mwaka 2019 waalimu waliongezewa mshahara kati ya shilingi elfu 2 hadi elfu 15, hicho ndio kinafuata mwaka mpya wa fedha kwa watumishi wote.

Tusubiri.
Mkuu nakupata vyema kabisa. Mambo ni mengi muda mchache.
 
Umetua mchango mzuri sana kwenye hoja yako. Ni kweli ipobkila sababu ya kupunguza matumizi ya Serikali yasiyokuwa ya lazima.

Ili Serikali ipunguze matumizi yasoyo ya lazima ni lazima iwe accountable kwa wananchi!! Katiba yetu ya sasa ina haya mapungufu hivyo hiyo haja ya kuwa na katiba itakayosisitiza uwajibikaji wa Serikali kwa Wananchi.
 
Back
Top Bottom