Serikali boresheni mishahara ya Walimu wa nchi hii

Mama Naa

JF-Expert Member
Aug 31, 2020
385
949
Amani iwe juu yenu nyote.

Mwalimu wa Nchi hii nadhani ametengenezewa UMASKINI kuanzia anaajiliwa mpaka anastafu. Kwanza ni watu wanaotoka kaya Maskini bado akiajiliwa anaishi kwenye umaskini akistaafu bado anakutana na KIKOKOTOO.

Mwalimu akiajiriwa anaanza na mshahara wa TGTS D1 (SANAA) 771,000/= na SAYANSI ni 750,000/= na hawa ni wa Degree Moja.

Hapo Mwalimu alipe kodi ya nyumba, Maji , Umeme, asomeshe, Ale, ahudumie familia na wengine ukoo Mzima. Bado mnataka avae apendeze kama kada zingine.

Mwalimu ili apande daraja afikie TGTS E1 basi itamchukua miaka 4 mpaka 5 nayo inategemeana na Rais wa wakati huo. (SIASA).

Hivi ni kwa nini daktari umlipe TGHS D1 (1270000) tofauti ya laki tano na mwalimu wa Degree na yeye ana degree wakati wengine walisoma wote hadi F6?

Walimu ndio nguzo ya Taifa, Taifa bora linatokana na raia wake walioelimika vizuri kwa kuwa na Walimu bora.

HAKUNA WALIMU BORA BILA MASLAHI BORA.

UALIMU ni vile tu umebebwa sana na watoto wa maskini ila SIO kazi ya kufanya.

Mwalimu hana House allowance, hana perdiem, hana extra duty, hana overtime bado awe mtumishi bora, Watu wanafanya bora liende tu.

Serikali waangalieni Walimu kwa jicho la pekee kama mnataka Taifa liwe bora.

Serikali haishindwi kuhudumia vizuri walimu 250,000+ (Msingi 170,000+ na sekondari 89,000+ huku walimu wa masomo ya Sayansi na hisabati wakiwa 23,000+)

Sio haki eti Mwalimu wa Degree kufikia Mshahara wa 1280,000 ambao ni TGTS F1 ni mpaka akae kazini miaka 8 - 10+ BADO TUNATAKA TAIFA LILILOELIMIKA?

INATIA UCHUNGU SANA, WANASIASA MMEJIWEKEA MASLAHI BORA SANA ILA WATUMISHI MKAAMUA KUWAPA KIKOKOTOO.

WATZ NI KWA NINI TUMEKUBALI MBUNGE MIAKA 5 APEWE MILIONI 270+ HALAFU MTUMISHI APEWE MILIONI 40+ KWA MIAKA 30 - 40 YA UTUMISHI?

TAIFA HILI LINA LAANA WALLAH.
 
E0816C52-AC84-490C-8775-004D4391648B.jpeg
 
Sema walimu waikatae Kwa Ile CWT pale ndio Kuna tatizo. Then ualimu usiwe kitu cha holela. Wenzenu Wana leseni, bila leseni huwezi kuwa mfamasia, bila leseni huwezi kuwa Engineer I mean kupata kazi, bila leseni huwezi kuwa Daktari, bila leseni huwezi kuwa wale sijui CPA Gani huko, bila leseni huwezi kuwa Wakili (reg.no.)

Nyie mnakwama wapi? Kwanini msivunje CWT mkaanzisha Board ya Walimu as a Professional entity?
 
Huwezi leta mageuzi kwa watu wasio jitambua kama waalimu maana haki zao na mafao yao yaliyupo kwa mujibu wa Sheria na mikataba ya kazi wanashindwa kuyatetea wanabaki kuwaomba watawala kuwatimizia kitu ambacho ni haki Yao kabisa huu si uzuzu na uzwazwa wamebaki kuvaa nguo za CWT tu,siku ya Mei mosi na kupewa nafasi za sensa na usimamizi wa uchaguzi ambazo kazi hizo zilipaswa kuwa za vijana jobless.

"Akili ni nywele kila mtu ana zake"
 
Tatizo linaanzia pale wengi wanaochukuliwa kuwa waalimu ni wale ambao matokeo yao ya kidato cha nne na sita ni udhaifu!

Utaratibu ungebadilishwa uwe kama vyuo vikuu ambavyo huchukua waliofaulu vizuri (cream) tu. Vinginevyo wataendelea kunyanyasika na hawawezi kijinasua kwa kuwa wanafahamu ukweli kuwa wao ni dhaifu katika masomo wanayofundisha!
 
Sema walimu waikatae Kwa Ile CWT pale ndio Kuna tatizo. Then ualimu usiwe kitu cha holela. Wenzenu Wana leseni, bila leseni huwezi kuwa mfamasia, bila leseni huwezi kuwa Engineer I mean kupata kazi, bila leseni huwezi kuwa Daktari, bila leseni huwezi kuwa wale sijui CPA Gani huko, bila leseni huwezi kuwa Wakili (reg.no.)

Nyie mnakwama wapi? Kwanini msivunje CWT mkaanzisha Board ya Walimu as a Professional entity?
Zanzibar bila leseni hufanyi kazi ya UALIMU ila mambo bado magumu sana.
 
Huwezi leta mageuzi kwa watu wasio jitambua kama waalimu maana haki zao na mafao yao yaliyupo kwa mujibu wa Sheria na mikataba ya kazi wanashindwa kuyatetea wanabaki kuwaomba watawala kuwatimizia kitu ambacho ni haki Yao kabisa huu si uzuzu na uzwazwa wamebaki kuvaa nguo za CWT tu,siku ya Mei mosi na kupewa nafasi za sensa na usimamizi wa uchaguzi ambazo kazi hizo zilipaswa kuwa za vijana jobless.

"Akili ni nywele kila mtu ana zake"
Nimeeleza hapo juu boss, tatizo kubwa ni umaskini. Walimu wengi ni maskini sana bora apate kidogo kuliko kukosa kabisa.
 
Tatizo linaanzia pale wengi wanaochukuliwa kuwa waalimu ni wale ambao matokeo yao ya kidato cha nne na sita ni udhaifu!

Utaratibu ungebadilishwa uwe kama vyuo vikuu ambavyo huchukua waliofaulu vizuri (cream) tu. Vinginevyo wataendelea kunyanyasika na hawawezi kijinasua kwa kuwa wanafahamu ukweli kuwa wao ni dhaifu katika masomo wanayofundisha!
Unaishi dunia gani huo mfumo ukishqbadilika miaka mingi sana. Saizi mtu wa chini kwenda ualimu ni Division 3 kwenye cheti. Lkn hilo sio tatizo kada nyingi wanaenda failure

Mfano uhasibu unaweza anza cheti mtu mwenye D nne tu, au uandishinwa habari na utangazaji. So hoja yako haina nguvu
 
Huwezi leta mageuzi kwa watu wasio jitambua kama waalimu maana haki zao na mafao yao yaliyupo kwa mujibu wa Sheria na mikataba ya kazi wanashindwa kuyatetea wanabaki kuwaomba watawala kuwatimizia kitu ambacho ni haki Yao kabisa huu si uzuzu na uzwazwa wamebaki kuvaa nguo za CWT tu,siku ya Mei mosi na kupewa nafasi za sensa na usimamizi wa uchaguzi ambazo kazi hizo zilipaswa kuwa za vijana jobless.

"Akili ni nywele kila mtu ana zake"
Nani anaeweza tetea maslahi na haki zake katika wafanyakazi wa nchi hii ukiwaondoa hao walimu? Madaktari? Sio waliogoma wakachukuliwa wanajeshi kwenda kutibu, wengine wakang'olewa kucha bila ganzi? Hii yako sio hoja ni makasiriko tu
 
Amani iwe juu yenu nyote.

Mwalimu wa Nchi hii nadhani ametengenezewa UMASKINI kuanzia anaajiliwa mpaka anastafu. Kwanza ni watu wanaotoka kaya Maskini bado akiajiliwa anaishi kwenye umaskini akistaafu bado anakutana na KIKOKOTOO.

Mwalimu akiajiriwa anaanza na mshahara wa TGTS D1 (SANAA) 771,000/= na SAYANSI ni 750,000/= na hawa ni wa Degree Moja.

Hapo Mwalimu alipe kodi ya nyumba, Maji , Umeme, asomeshe, Ale, ahudumie familia na wengine ukoo Mzima. Bado mnataka avae apendeze kama kada zingine.

Mwalimu ili apande daraja afikie TGTS E1 basi itamchukua miaka 4 mpaka 5 nayo inategemeana na Rais wa wakati huo. (SIASA).

Hivi ni kwa nini daktari umlipe TGHS D1 (1270000) tofauti ya laki tano na mwalimu wa Degree na yeye ana degree wakati wengine walisoma wote hadi F6?

Walimu ndio nguzo ya Taifa, Taifa bora linatokana na raia wake walioelimika vizuri kwa kuwa na Walimu bora.

HAKUNA WALIMU BORA BILA MASLAHI BORA.

UALIMU ni vile tu umebebwa sana na watoto wa maskini ila SIO kazi ya kufanya.

Mwalimu hana House allowance, hana perdiem, hana extra duty, hana overtime bado awe mtumishi bora, Watu wanafanya bora liende tu.

Serikali waangalieni Walimu kwa jicho la pekee kama mnataka Taifa liwe bora.

Serikali haishindwi kuhudumia vizuri walimu 250,000+ (Msingi 170,000+ na sekondari 89,000+ huku walimu wa masomo ya Sayansi na hisabati wakiwa 23,000+)

Sio haki eti Mwalimu wa Degree kufikia Mshahara wa 1280,000 ambao ni TGTS F1 ni mpaka akae kazini miaka 8 - 10+ BADO TUNATAKA TAIFA LILILOELIMIKA?

INATIA UCHUNGU SANA, WANASIASA MMEJIWEKEA MASLAHI BORA SANA ILA WATUMISHI MKAAMUA KUWAPA KIKOKOTOO.

WATZ NI KWA NINI TUMEKUBALI MBUNGE MIAKA 5 APEWE MILIONI 270+ HALAFU MTUMISHI APEWE MILIONI 40+ KWA MIAKA 30 - 40 YA UTUMISHI?

TAIFA HILI LINA LAANA WALLAH.
Madaktari wanao anza kazi wa degree ni 1.5m nilisoma kwenye mtandao
 
Back
Top Bottom