Mkereketwa_Huyu
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 9,188
- 6,323
Baada ya kuangalia "The Great Migation" ya wanyama wanaotoka Serengeti kwenda Maasai Mara Kenya kukimbia ukame Tanzania, kwa kweli nimeshikwa na hasira. Kwa nini? Maasai Mara ni sehemu ndogo sana tena sana kulinganisha na Serengeti, ila TV za dunia zimehamia huko na kuitangaza Kenya as if Serengeti iko huko. Yaani wanavyotangaza ni kama vile Serengeti is nothing compared to Maasai Mara. Pia kinacho udhi ni kwamba Kenya wanapata pesa za utalii wa hii Great Migration mara 20 zaidi ya Tanzania (source - CCTV China). TANAPA kazi yao ni nini? Kila kukicha viongozi wanasafiri nje ya nchi kuitangaza Tanzania, sasa kwanini tunazidiwa kete na majirani? Hakuna nchi duniani yenye mbuga kama zetu, kwanini tunakuwa mazezeta? Je, Maasai Mara ni bora shinda The mighty Serengeti? Hii nchi bwana, basi tu.