Sera ya viwanda inayofaa tanzania

kingadvisor

Senior Member
Dec 21, 2011
109
30
Wachina , wajapani na wahindi waligundua kuwa ili waendelee wanahitaji viwanda.Swali likaja ni viwanda vya namna gani na waanzie na vya namna gani wakagundua sio vile vya kuzalisha (manufacturing) bali vya kuunganisha (assembling).Mfano unaunda gari tairi zinauzwa mitaani,engine zinauzwa ziko za kila aina ,carburator,na vitu vingi vya gari viko masokoni kibao na hutengenezwa na mikampuni kibao duniani.Unachofanya wewe ni kuanzisha kiwanda cha kuunganisha hivyo vyote ulivyonunua madukani.ukishaunga kama ni pikipiki uliyounganisha badala ya kuita honda unaita toyo au chochote.

Hizi nchi zimebobea kwenye assembling hizo pikipiki zilizojaa Tanzania zingine nasikia wana-assemble vyumbani wenyewe wanaita bedroom Industries kama vile fund cherehani aweza shonea chumbani wachina na wahindi waweza assemble baiskeli na pikipiki vyumbani aweza tengeneza tatu kwa wiki hata nne akiwa na mafundi wake wa welding,chuma n.k Tanzania twaweza anza na assembling light industries.Vyuo vyetu wawe wanatrain watu namna ya kuassemble kuanzia ku-assemble saa za mikononi,baiskeli,pikipiki n.k waende na wanafunzi madukani wanunue kifaa kimoja kimoja kisha waassemble na kutoa product fulani.
Hiyo itachochea wakimaliza wakimbilie uanzishaji viwanda vya assembling za vitu mbalimbali kama wachina,wahindi na wajapani walivyo.
Haya mapikipiki hata vijana wetu wa VETA waweza kuanza kuyaassemble.

Vyuo vikuu navyo vijikite kwenye masomo ya assembling ni mahali rahisi pa kuchochea technolojia kwa vitendo.Hawa wenzetu wamebobea kwenye assembling iwe ya TV,RADIO,SAA,MAGARI,SIMU,Matrekta N.K hawahangaiki sana kufikiri kubuni vitu vipya wao hubobea kwenye kuassemble vilivyokwishabuniwa na ambavyo spare part zimezagaa mitaani za components zake.Naamini tukiwa na siasa na sera inayokazia ASSEMBLING INDUSTRIES muda si mrefu Tanzania itaanza kuzalisha magari,pikipiki,baiskeli,n.k mitaani. Nawasilisha.

kingadvisor@yahoo.com
 
Wazo zuri. Hasa assambling ya vifaa vya kilimo na vile vya kuprocess mazao ya kilimo. Kwa mfano dakika hii ninaandika hapa kuna mradi mkubwa wa kuzalisha maziwa kwa wingi unaelekea kuiva. Lakini changamoto ni namna yatakavyokusanywa toka kwa wakulima, kuwa proccesed na kusambaza kwa walaji kabla hayajaharibika.
 
Back
Top Bottom