Septemba 6 2014: Simba vs Gor Mahia, kutoka Uwanja wa Taifa

Septemba 6 2014: Simba vs Gor Mahia, kutoka Uwanja wa Taifa

Baada ya ujio wa Patrick Phili na vuguvugu la usajiri, SIMBA SC leo wanajitupa uwanja wa Taifa.
Kwa updates pitia hapa
Yanga walitumia mbinu kubwa sana kuahirisha mechi ya Bata Bullets maana kwa ushindi wa Simba ingekuwa ndio mwisho wa aidha Jaja au Maximo au wote, bahati nzuri nilipitia vijiwe kadhaa vya Yanga tukisubiri mechi na kwa kweli hali si nzuri wapenzi wana hasira sana na Jaja
 
Ni mwendo unaotia matumaini licha ya baadhi ya watu kubeza isijekuwa kama Manchester United.

Manchester ilishinda mechi zote za kirafiki na kuzifunga hadi timu kubwa kama Real Madrid na Liverpool, lakini haijaonja ushindi wowote katika mechi nne za mashindano ilizocheza mpaka sasa. Imefikia hata hatua ya kufungwa mabao 4-0 na timu ya Daraja la Kwanza ya MK Dons.

Wakati ukiendelea kutafakari hayo, Mwanaspoti linakuletea mambo 10 yaliyojionyesha kwenye mchezo wa Simba na Gor Mahia ambapo Simba ilishinda mabao 3-0, wafungaji wakiwa Raphael Kiongera (mawili) na Ramadhani Singano ‘Messi'.

Phiri anaiwezea Simba

Kwa wiki tatu ambazo Phiri amekuwa klabuni hapo, mabadiliko makubwa yameonekana.

Msimu uliopita ilikuwa na kikosi dhaifu kilichoshindwa hata kuifunga Ashanti United iliyoshuka daraja.

Juzi iliwakosa Pierre Kwizera, Amri Kiemba, Haruna Chanongo, Saidi Ndemla, Joram Mgeveke na Amissi Tambwe waliokwenda kwenye majukumu ya kitaifa, pia ikawakosa Jonas Mkude na Issa Rashid ' Baba Ubaya' ambao ni majeruhi, lakini ilicheza kwa kiwango cha juu.

Ilikuwa zaidi ya Simba ya wiki nne zilizopita iliyochezwa dhidi ya Zesco ya Zambia wakati huo ikiwa chini ya Mcroatia Zdravko Logarusic.

Friends usipime

Ni miezi miwili tangu Kundi la Friends of Simba lichukue madaraka katika klabu hiyo chini ya Rais Evans Aveva. Usajili wa maana uliowaongeza akina Kwizera, Raphael Kiongera, Elius Maguli na Shaban Kisiga, umeimmarisha mno timu. Licha ya wachezaji hao Simba pia imewasajili kipa Hussein Sharrif ‘Casillas' na Peter Manyika Junior, beki Mohammed Hussein ‘Tshabalala' na Abdi Banda ambao pia wameonyesha uwezo wa kuvutia.

Okwi ataisaidia Simba

Kesi ya mshambuliaji mpya wa Simba, Emmanuel Okwi raia wa Uganda ilitarajiwa kusikilizwa jana Jumapili kuamua kama Okwi ni halali wa Simba ama la. Endapo mambo yatakwenda vizuri kwa Simba ni dhahiri kuwa Okwi atafanya makubwa msimu ujao. Katika mchezo wa juzi Okwi alicheza kwa kiwango cha juu licha ya ukweli kwamba hajacheza mechi ya mashindano kwa muda mrefu.
 
Mfumo 3-5-2 unaifaa Simba

Katika mchezo wa juzi Simba ilitumia mfumo wa 3-5-2 ambao ulionekana kuendana na kasi ya vijana wa timu hiyo. Kipindi cha kwanza pale mbele alisimama Okwi na Elius Maguli wakati kipindi cha pili alitoka Maguli na kuingia Raphael Kiongera. Katika safu ya ulinzi walisimama Joseph Owino, Rajab Isihaka na Miraji Adam. Abdi Banda alicheza beki lakini alisogea kwa mbele kidogo.

Vijana Simba waimarika

Kocha aliyetimuliwa na Simba mapema mwezi uliopita, Mcroatia Zdravko Logarusic hakuwa akiwapenda vijana wa klabu hiyo. Alitaka wachezaji wenye uzoefu mkubwa.

Wachezaji William Lucian ‘Gallas', Rajab Isihaka, Ramadhani Singano ‘Messi', Ibrahim Twaha wakawa na wakati mgumu, lakini sasa nuru imewawakia.

Ubingwa hautabiriki

Simba imeshinda mechi zote nne za kirafiki ilizocheza tangu kuwasili kwa kocha Phiri. Yanga nayo imeshinda mechi zote nne za kirafiki. Mabingwa watetezi Azam FC walicheza kwa kiwango cha juu kwenye michuano ya Kombe la Kagame, walitolewa katika hatua ya robo fainali kwa mikwaju ya penalti. Hawakupoteza mchezo wowote katika michezo mitano waliyocheza. Hii ni ishara kuwa timu hizi ziko kwenye ubora wake kwa sasa.

Kisiga bado ana vitu mguuni

Kama ulitazama mchezo wa juzi na mechi nyingine yoyote ya Simba utakubaliana na mimi. Waswahili watakwambia Ng'ombe hazeeki maini. Kiungo mshambuliaji Shabaan Kisiga bado ana vitu mguuni. Anaweza kuichezesha timu, anapiga pasi kamili na wakati mwingine anasaidia kukaba. Nilipata wasiwasi wakati Simba wanamsajili baada ya kutemwa Mtibwa lakini Kisiga tayari ameanza kudhihirisha kuwa bado ana vitu vya kuipatia klabu hiyo.

Oktoba 12, Taifa patafurika

Kama hali itaendelea hivi, Jumapili ya Oktoba 12 jitahidi kuwahi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mapema. Jitahidi sana. Mashabiki wa Simba wamerejesha imani kwa timu yao. Katika mechi ya juzi licha ya tiketi kuuzwa siku ya mchezo pekee uwanja ulifurika. Majukwaa yaliyokuwa yakipwaya msimu uliopita yalionekana kujaa. Simba na Yanga zina mechi tatu za ligi pekee kabla ya kukutana. Endapo wimbi hili la ushindi lililoanzia kwenye mechi za kirafiki litaendelea ni dhahiri kuwa siku hiyo uwanjani kutakosekana mahali pa kukaa.



 
Uuzwaji mbovu wa tiketi

Uwanja wa Taifa juzi uligeuka kama soko la Tandale ama Buguruni. Kulikuwa na uuzwaji mbovu wa tiketi kama visheti ama vitumbua vya bei chee eneo la Mbagala Rangi Tatu. Mashabiki wa soka waliojitokeza kwa wingi kushuhudia mechi hiyo walipata matatizo makubwa katika kununua tiketi. Ni gari moja pekee lililokuwa likiuza tiketi za mchezo huo nje ya Uwanja wa Taifa. Madirisha matatu pekee ya gari hilo yalitumika kuuza tiketi kwa watu zaidi ya 15,000 waliojitokeza kushuhudia mchezo huo. Ni aibu sana kwa timu kubwa kama Simba kuwa na uuzwaji mbovu wa tiketi.

Aina hii mbovu ya uuzaji wa tiketi ndiyo unaochangia upotevu wa pato la mlangoni.


Chanzo; Mwanaspoti Jumatatu Sept 8
 
Back
Top Bottom