Semiconductors/Microchips zinavyoiweka Tawain katikati ya mpambano mkali wa China na Marekani

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,620
46,264
Mgogoro wa China na Taiwan ni wa muda mrefu sana ila kwa sasa unakolezwa zaidi na vita vya Teknolojia ya semiconductors/microchips kati ya Marekani na China ambao wote wanategemea kwa sehemu kubwa Taiwan katika uzalishaji na ku supply kwao.

Taiwan ndiye kiongozi katika dunia ya sasa kwa 65% katika teknolojia ya microchips zinazotumika katika simu, computer, ndege, rockets, magari, vifaa vya hospitali, jeshi n.k. Ni kama vile ilivyo OPEC kwenye mafuta. Kampuni ya TSMC peke yake inazalisha 50% ya soko la dunia. Asilimia zilizobaki ndizo zinazalishwa na Korea Kusini, Marekani, China bara na Ulaya.

Xi Jinping, Rais wa China tangu aingie madarakani imeonekana ana nia na mpango wa kuimeza na kuinganisha kabisa Taiwan na China bara. Akifanikiwa na kama ataichukua Taiwan bila vita ambavyo vitaharibu biashara inamaanisha CCP itakuwa na total control ya biashara ya semiconductors jambo ambalo litakuwa pigo kubwa kwa US kwa kipindi kirefu. Pia Taiwan ikifanikiwa kujitenga kabisa inamaanisha China itapoteza ndoto ya kuwa wamilikaji wakuu wa biashara ya microchips duniani. Hapa ndipo kuna hesabu kali za kula au kuliwa.

Marekani tayari imepitisha Chips and Science Act, mpango dollar bilioni 53 kwa ajili ya kurudisha uwekezaji mkubwa wa semiconductor US, katika mpango huu makampuni yatakayowekeza US katika sekta ya semiconductors na kuonyesha mkakati wa kutofanya biashara ya semiconductors na China yatapewa ruzuku katika biashara zao.

Kuna wakati Taiwan ilipuuzwa na pande zote mbili, ila sasa hivi vita vya teknolojia vimeirudisha kuifanya "hot cake" ya kuwatoa wakubwa wa dunia roho.
 
China anaipigia Taiwan mahesabu ya juu sana kwa sababu akiingia kwa vita na uharibifu mkubwa itakuwa hakuna alichofaidi hata akiichukua, Taiwan haitakuwa na faida kwake ikiwa magofu.
Mchina sio mjinga aingie kichwa kichwa pale Taiwan.

Taiwan sio Ukraine

Naitamani hii vita ya ndugu
 
Sababu ni hayo yote pamoja suala la usalama kimkakati kwa washirika wake wanaoizunguka Taiwan pia.
So U.S.A anaposema atailinda ROC dhidi ya PRC sababu sio freedom & democracy bali ni semiconductors ?
 
Sababu ni hayo yote pamoja suala la usalama kimkakati kwa washirika wake wanaoizunguka Taiwan pia.

Mgogoro wa China na Taiwan ni wa muda mrefu sana ila kwa sasa unakolezwa zaidi na vita vya Teknolojia ya semiconductors/microchips kati ya Marekani na China ambao wote wanategemea kwa sehemu kubwa Taiwan katika uzalishaji na ku supply kwao.

Kuna wakati Taiwan ilipuuzwa na pande zote mbili, ila sasa hivi vita vya teknolojia vimeirudisha kuifanya "hot cake" ya kuwatoa wakubwa wa dunia roho.
Ok
 
Sababu ni hayo yote pamoja suala la usalama kimkakati kwa washirika wake wanaoizunguka Taiwan pia.
Ok, let make things simple. suala la muungano kati ya serikali mbili zinazo jitambulisha kama wamiliki wa China yote alipaswi kuhusishwa na masuala ya teknolojia ya semiconductors kwa sababu hii ni hoja isiyo kuwa na uzito.

Chanzo cha mgogoro huu hakina uhusiano wowote ule na teknolojia ya semiconductors sio tu kwa miaka ya mwanzo wa mgogoro huu hata sasa sio PRC wala ROC wenye kuonesha hali ya kuwa mgogoro umebebwa na sababu kuu ya mapigano juu ya umiliki wa teknolojia, viwanda na usambaaji wa semiconductors duniani

Hii ni vita ya wenyewe kwa wenyewe ambayo haiikuisha kwa sababu mbalimbali zilizo pelekea vita hio kutokwisha

Kuna juhudi mbalimbali za kumaliza mgogoro huu kwa njia ya amani toka pande zote mbili hizi ni jitihada zilizo anza kufanyiwa kazi kwa pande zote mbili kwa muda mrefu mpaka sasa.

Matumizi ya nguvu katika mgogoro huu kama njia ya kutamatisha mgogoro huu ni tokeo la mwisho endapo jitihada za amani katika kumaliza mgogoro huu zikigonga mwamba
 
Sijazungumzia chanzo cha huu mgogoro kabisa. Nimezungumzia "episode" ya sasa tu ya mahusiano kuwa mabovu zaidi kati ya pande zote tatu inachangiwa na nini. Kama CCP walivyoweka katika katiba ya China (anti- secession law)/sheria ya kutojitenga na ikibidi kutumia nguvu kuzuia hilo baada ya Chen Shui-bian ambaye alikuwa na msimamo wa kujitenga kabisa na China bara alipochaguliwa tena kuwa Rais wa Taiwan mwaka 2004 na, mgogoro wowote wa muda mrefu huwa kuna vipindi tofauti vya kupungua na kuogezeka uhasama kunakochangiwa na matukio mengine ya wakati husika.
Ok, let make things simple. suala la muungano kati ya serikali mbili zinazo jitambulisha kama wamiliki wa China yote alipaswi kuhusishwa na masuala ya teknolojia ya semiconductors kwa sababu hii ni hoja isiyo kuwa na uzito.

Chanzo cha mgogoro huu hakina uhusiano wowote ule na teknolojia ya semiconductors sio tu kwa miaka ya mwanzo wa mgogoro huu hata sasa sio PRC wala ROC wenye kuonesha hali ya kuwa mgogoro umebebwa na sababu kuu ya mapigano juu ya umiliki wa teknolojia, viwanda na usambaaji wa semiconductors duniani

Hii ni vita ya wenyewe kwa wenyewe ambayo haiikuisha kwa sababu mbalimbali zilizo pelekea vita hio kutokwisha

Kuna juhudi mbalimbali za kumaliza mgogoro huu kwa njia ya amani toka pande zote mbili hizi ni jitihada zilizo anza kufanyiwa kazi kwa pande zote mbili kwa muda mrefu mpaka sasa.

Matumizi ya nguvu katika mgogoro huu kama njia ya kutamatisha mgogoro huu ni tokeo la mwisho endapo jitihada za amani katika kumaliza mgogoro huu zikigonga mwamba
 
Sijazungumzia chanzo cha huu mgogoro kabisa. Nimezungumzia "episode" ya sasa tu ya mahusiano kuwa mabovu zaidi kati ya pande zote tatu inachangiwa na nini. Kama CCP walivyoweka katika katiba ya China (anti- secession law)/sheria ya kutojitenga na ikibidi kutumia nguvu kuzuia hilo baada ya Chen Shui-bian ambaye alikuwa na msimamo wa kujitenga kabisa na China bara alipochaguliwa tena kuwa Rais wa Taiwan mwaka 2004 na, mgogoro wowote wa muda mrefu huwa kuna vipindi tofauti vya kupungua na kuogezeka uhasama kunakochangiwa na matukio mengine ya wakati husika.
Hujazungumzia chanzo cha mgogoro fine. Umezungumzia episode ya sasa pia nayo sio sahihi.

Mgogoro uliopo kuhusu masuala ya Chips, semiconductors kwa sasa ni baina ya China PRC na U.SA usio na mahusiano na China ROC

Influence ya U.S.A imeweza kuwa shawishi baadhi ya washirika wake kuweka ban kwa China PRC kuhusu usambazaji wa teknolojia ya utengenezaji wa semiconductors katika ngazi zote baadhi ya washirika wa U.S.A walio ungana naye katika vita hiyo ni pamoja na Japan na Netherlands.

Ugomvi wa U.S.A na China PRC upo kwenye semiconductors tu pasipo kuhusisha masuala ya ROC na umiliki wake wa teknolojia ya chips kama ndicho kichochezi kikubwa cha mgogoro wa U.S.A, China PRC na China ROC kwa sasa
 
Sijazungumzia chanzo cha huu mgogoro kabisa. Nimezungumzia "episode" ya sasa tu ya mahusiano kuwa mabovu zaidi kati ya pande zote tatu inachangiwa na nini. Kama CCP walivyoweka katika katiba ya China (anti- secession law)/sheria ya kutojitenga na ikibidi kutumia nguvu kuzuia hilo baada ya Chen Shui-bian ambaye alikuwa na msimamo wa kujitenga kabisa na China bara alipochaguliwa tena kuwa Rais wa Taiwan mwaka 2004 na, mgogoro wowote wa muda mrefu huwa kuna vipindi tofauti vya kupungua na kuogezeka uhasama kunakochangiwa na matukio mengine ya wakati husika.
China PRC sasa wapo kwenye mpango wao mkubwa wa kupunguza au kuondoa kabisa utegemezi katika nyanja zote kutoka mataifa ya nje katika kila kitu. Mpango huo ni mpaka miaka ya 2049-2050.

Suala la kujitegemea katika teknolojia serikali imetenga fedha zaidi ya billions of dollars katika kukuza zaidi sekta ya teknolojia katika masuala yote ikiwemo mambo ya semiconductors etc

Vikwazo vya marekani na mataifa mbalimbali ya magharibi vimekuwa vikitumika kama njia ya kuzuia ukuaji wa teknolojia wa China na makampuni yake njia pekee na iliyo bora kama taifa ni kuwa self- reliance katika upande huo
 
Sijazungumzia chanzo cha huu mgogoro kabisa. Nimezungumzia "episode" ya sasa tu ya mahusiano kuwa mabovu zaidi kati ya pande zote tatu inachangiwa na nini. Kama CCP walivyoweka katika katiba ya China (anti- secession law)/sheria ya kutojitenga na ikibidi kutumia nguvu kuzuia hilo baada ya Chen Shui-bian ambaye alikuwa na msimamo wa kujitenga kabisa na China bara alipochaguliwa tena kuwa Rais wa Taiwan mwaka 2004 na, mgogoro wowote wa muda mrefu huwa kuna vipindi tofauti vya kupungua na kuogezeka uhasama kunakochangiwa na matukio mengine ya wakati husika.
Kuhusu suala la katiba na kujitenga au kusaka uhuru si katiba ya PRC wala ROC inayo ruhusu kitendo hicho.

Hivyo katiba zote mbili kati ya PRC na ROC hakuna inayo ruhusu kujitenga au kusaka uhuru kutoka katika nchi ya China.
 
Nawasoma kwa ukaribu sana na mnautanua ubongo wangu kupokea ambavyo nilikuwa sijavipokea kabla.......
 
Mgogoro wa China na Taiwan ni wa muda mrefu sana ila kwa sasa unakolezwa zaidi na vita vya Teknolojia ya semiconductors/microchips kati ya Marekani na China ambao wote wanategemea kwa sehemu kubwa Taiwan katika uzalishaji na ku supply kwao.

Taiwan ndiye kiongozi katika dunia ya sasa kwa 65% katika teknolojia ya microchips zinazotumika katika simu, computer, ndege, rockets, magari, vifaa vya hospitali, jeshi n.k. Ni kama vile ilivyo OPEC kwenye mafuta. Kampuni ya TSMC peke yake inazalisha 50% ya soko la dunia. Asilimia zilizobaki ndizo zinazalishwa na Korea Kusini, Marekani, China bara na Ulaya.

Xi Jinping, Rais wa China tangu aingie madarakani imeonekana ana nia na mpango wa kuimeza na kuinganisha kabisa Taiwan na China bara. Akifanikiwa na kama ataichukua Taiwan bila vita ambavyo vitaharibu biashara inamaanisha CCP itakuwa na total control ya biashara ya semiconductors jambo ambalo litakuwa pigo kubwa kwa US kwa kipindi kirefu. Pia Taiwan ikifanikiwa kujitenga kabisa inamaanisha China itapoteza ndoto ya kuwa wamilikaji wakuu wa biashara ya microchips duniani. Hapa ndipo kuna hesabu kali za kula au kuliwa.

Marekani tayari imepitisha Chips and Science Act, mpango dollar bilioni 53 kwa ajili ya kurudisha uwekezaji mkubwa wa semiconductor US, katika mpango huu makampuni yatakayowekeza US katika sekta ya semiconductors na kuonyesha mkakati wa kutofanya biashara ya semiconductors na China yatapewa ruzuku katika biashara zao.

Kuna wakati Taiwan ilipuuzwa na pande zote mbili, ila sasa hivi vita vya teknolojia vimeirudisha kuifanya "hot cake" ya kuwatoa wakubwa wa dunia roho.
Mitambo ya kutengenezea hizo chip inatengenezwa Netherlands kule wamewekeza tu, China wakizingua wanahamisha teknologia
 
Sio kirahisi hivyo japo huo ni ukweli kwamba teknolojia na mitambo vilitoka West walipo outsource na pia wanasayansi walioleta hayo mapinduzi makubwa Taiwan walisoma vyuo vya Marekani ila Taiwan yenyewe waliweka mkakati wa kuwa watengenezaji wa dunia wa microchips kwa kujitegemea na sasa imeshapiga hatua nyingi sana mbele.
Mitambo ya kutengenezea hizo chip inatengenezwa Netherlands kule wamewekeza tu, China wakizingua wanahamisha teknologia
 
China anaipigia Taiwan mahesabu ya juu sana kwa sababu akiingia kwa vita na uharibifu mkubwa itakuwa hakuna alichofaidi hata akiichukua, Taiwan haitakuwa na faida kwake ikiwa magofu.
Naona anafanya simulation ya attack,wenzake wanamchora tu
 
China PRC sasa wapo kwenye mpango wao mkubwa wa kupunguza au kuondoa kabisa utegemezi katika nyanja zote kutoka mataifa ya nje katika kila kitu. Mpango huo ni mpaka miaka ya 2049-2050.

Suala la kujitegemea katika teknolojia serikali imetenga fedha zaidi ya billions of dollars katika kukuza zaidi sekta ya teknolojia katika masuala yote ikiwemo mambo ya semiconductors etc

Vikwazo vya marekani na mataifa mbalimbali ya magharibi vimekuwa vikitumika kama njia ya kuzuia ukuaji wa teknolojia wa China na makampuni yake njia pekee na iliyo bora kama taifa ni kuwa self- reliance katika upande huo
Sekta ya semiconductors/Chips bado sana kwa China mainland. Bila Taiwan wako nyuma sana katika hii teknolojia.
 
Back
Top Bottom