Sekretarieti ya Ajira; Ukiritimba huu hadi lini?

Sekretarieti ya Ajira; Ukiritimba huu hadi lini?

Abx

Senior Member
Joined
Oct 16, 2012
Posts
139
Reaction score
79
Habari wana bodi,

Ni juzi kati tuliitwa kwenye usaili wa mchujo (interview) hapo maktaba ile kufika jibu likawa kama huna cheti ishia hapo hapo, sasa sisi wengine tulikuwa na matokeo ya muda (provisional results) toka taasisi yetu ya mafunzo, tukazuiliwa kuingia tulikuwa wengi kama 60 hv.

Cha kusikitisha ghafla akaja kijana mmoja namfaham kwa kumuacha pale nliposoma soma mimi, na kuwa ndo alikuwa amefanya mtihan wake wa mwisho hatavile provisional hana nlonayo mimi, alifika pale na kuingia bila kikwazo chochote, na hakuonesha utambulisho wowote wa sifa ya nafasi ya kazi ile aliyokuja kufanyia usaili.

HII SI SAWA KABISA, HATA KAMA WEWE UNAJIITA MTETEZI WA WANYONGE BADO HUKU VIJANA WAKO WANAKUANGUSHA KULE PAMEOZA MZEE PAANGALIWE KWA JICHO LA TATU NA LA KIPEKEE, Vinginevyo elimu yetu sisi makapuku toloitegemea itukomboe tutakuwa ni kupoteza muda tu bora tukalime matikiti maji kule Magu.
 
Unakamata mnapiga kipigo cha mwixi mnachukua na Video kabisa.... Ili ijulikane Ajira Ngumu.. Watu 60 mnashindwa na mtu mmoja
 
Hivyo vitu huwa hawaruhusu kabisa Provisional cerificate au Results slip wala usiangaike kwenda kule .....
 
Mkuu tangu lini provisional result ukaombea kazi serikalini labda uyo waliomruhusu alikuwa na transcript
 
Mkuu hili jambo kinategemeana na mtu mliekutana nae ni yupi, kuna wengine wana roho mbaya sana kiasi kwamba kamaa umepoteza cheti na una vibali vyote vya polisi wanakuzuia

hilo la provisional result inategemea na mtu, kuna dogo nilifanya nae interview kwa hiyo, ila walimwambia aende chuo wampe barua kuwa ni kweli amemaliza hapo na anasubiri cheti, walimpa akapiga oral vzuri tu
 
Ila mbona tangia zamani na hata kwenye website wameandika kuwa hawa accept.


Ilikuwa sio riziki yako kijana wewe koma nafasi zipo nyingi watatangaza
Kuna jambo lipo nyuma ya pazia, ukweli system bado kwa sehemu fulani ina upendeleo, yaani pamoja na kupungua rushwa kubwa, rushwa ndogo bado ipo. Ni muhimu serikali ikaliangalia
 
Mkuu unadhan wote tunafanana? Huwezi jua huyo alikua mtu wa kitengo na walitaka wamuweke kwenye idara yenye hiyo kazi mliyoomba ili awe "mtuma taarifa" wa kitengo!! Na usishangae akipata kazi!!

Wewe mmatumbi mwenzangu twenzetu tukalime viazi mviringo!! Acha kulalamika!
 
Eti pameoza kisa kijana kapita ndo unasema pameoza,kwanza unavyoandika ni dhahiri umekariri.unajua maana ya kuoza wewe,alafu bahati ya mwenzio usiilalie mlango wazi mkuu,
 
Aisee tuna lawama sana watz ushaambiwa hawaruhusu transcript we bado unaenda nayo ukitaka nchi iendeshwe unavotaka mkuu hatufiki Mimi nimefanya usaili sina ninayemjua nimefanya wanavyotaka sasa hivi nipo kazini. Tuache kuchafuana jamani vigezo na mashart kuzingatiwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom