Elections 2010 Seif achukua fomu za kugombea tena CUF, akemea ving'ang'anizi wa madaraka


Seif na Mwalimu walikutana Msasani nyumbani kwa Mwalimu na si Butiama! Ndugu yangu Mwiba ingekuwa vizuri ungetuambia source wako aliyekupa maongezi 'ya siri' ya Mwalimu na Seif ikiwemo Mwalimu kumuomba msamaha Seif! Sina hakika kama Maelezo ya Mkutano wa Seif na Mwalimu yalishatolewa rasmi! Ninachofahamu mimi Mwalimu ni kweli alikuwa 'akimpenda' Seif! Ziko sababu nyingi tu ukiachilia mbali Seif, Salmin, JK na vijana wengine wa wakati huo walifanya kazi kwa karibu na Mwalimu kipindi cha Mwalimu alipong'atuka madakarakani na kubaki na kofia ya Uenyekiti wa CCM. Lingine linalozungumzwa ni kuwa Seif ndiye aliyempelekea Mwalimu ule waraka wa Rais wa Zanzibar wakati huo Aboud Jumbe aliyemtaka Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar kufungua kesi ya mgogoro wa Kikatiba kuhusu Muungano wa Tanzania. Hili utakumbuka lilipelekea Jumbe kuvuliwa Urais wa Zanzibar.

Mimi ningemsahuri Seif kwa sasa hivi asigombee tena Urais wa Zanzibar. Anaweza kubaki kuwa Katibu Mkuu wa CUF ili kurithisha madaraka makubwa kwa vijana bila kuathiri chama lakini atengeneze 'Seif' mwingine. Hata kama unakula chakula kizuri kikizidi kiwango hukinaisha! Muda wa Seif kusimama kwenye nafasi za juu za Uchaguzi pale visiwani nionavyo mimi UMEKWISHA! Katiba haimzuii lakini alama za nyakati ZINAMZUIA!
 
Na hao anaosema wanang'ang'ania je wanavunja kanuni ama taratibu zao ? Je kuna kanuni iliyomzuia Mugabe kugombea na akaivunja ? Ninavyoelewa ni kuwa wanang'ang'ania kwa sababu kanuni, sheria na taratibu zao zinaruhusu.
hivi wewe unadhani tatizo ni Mugabe kugombea?, au tatizo ni kumnyima ushindi mshindi halali?.
chukulia mfano, uwaziri mkuu wa uingereza hauna kikomo, kikomo chako ni pale watu watakapokuchoka na kukutoa hata kama ni ndani ya miezi miwili tangu uchukue madaraka incase uchaguzi mkuu unaitishwa na chama chako kushindwa, lakini kama chama chako kinapendwa na kila uchaguzi mkuu unapoitishwa kinashinda,unaweza kukaa madarakani hata maisha yako yote.

sidhani kama ni vizuri kumlimit mtu anayecheza na kanuni ambazo wala hatuzipingi wala kuzikana, mimi ninadhani badala ya kumpinga mtu tupinge kanuni na taratibu, kwa sababu mtu anakuja na kupita lakini kanuni ni taasisi zipo always unless zibadilishwe
 
wameghafilika hawajui kwamba seif ni ccm .. anawaangamiza bila kujijua .. kwanini yeye kila uchaguzi na kama hajafanikisha siku zote hizo .. ana uhakika gani kwamba atafanikisha this time??? anyway yangu macho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…