Asanteni kwa mjadala mzuri.
Kuhusu timu kuwa na uwezo mzuri wa kushambulia, wataalam wa mpira wanasema njia nzuri ya 'kujilinda ni kushambulia' Falsafa hiyo imeenea sana kwenye mpira wa sasa. Mfano: Tazama mpira wa Barcelona na Spain: Utagundua kwamba timu hizo zina viungo na washambuliaji imara na wazuri kuliko walinzi. Fikiria beki kama Gerald Pique na golikipa Valdes, hawa watu wawili uwezo wao ni wa kawaida sana, kinachowaokoa ni kwamba timu 'zao', namaanisha Barcelona Cf, au Hispania zinakuwa na washambuliaji na viungo wazuri na hivyo mpira unachezwa zaidi katikati au kwenye lango la wapinzani. Mabeki wanakuwa na kazi ndogo tu ya kuondoa hatari ambazo hutokea mara chache tu!
Kuhusu timu kuwa na uwezo mzuri wa kushambulia, wataalam wa mpira wanasema njia nzuri ya 'kujilinda ni kushambulia' Falsafa hiyo imeenea sana kwenye mpira wa sasa. Mfano: Tazama mpira wa Barcelona na Spain: Utagundua kwamba timu hizo zina viungo na washambuliaji imara na wazuri kuliko walinzi. Fikiria beki kama Gerald Pique na golikipa Valdes, hawa watu wawili uwezo wao ni wa kawaida sana, kinachowaokoa ni kwamba timu 'zao', namaanisha Barcelona Cf, au Hispania zinakuwa na washambuliaji na viungo wazuri na hivyo mpira unachezwa zaidi katikati au kwenye lango la wapinzani. Mabeki wanakuwa na kazi ndogo tu ya kuondoa hatari ambazo hutokea mara chache tu!