Schizophrenia ni nini?

Jahface kotto

Member
Jun 3, 2016
26
8
Wadau naomba mnifahamishe nataka kujua. Schizophrenia ni nini na wanatambulika vipi watu waliokuwa nayo hapa duniani?

Mnamo tarehe 06/06/2006 nilipata maono nikiwa kule UESPANYA. Maono ya REVELATION. Na baada ya hayo maono kuna siku nilokuwa nimekaa kwenye PARK fulani nikiwa naota JUA kama ilivyokuwa desturi ya watu tunaoishi huku.

Nikiwa nimekaa kwenye bench naota JUA huku nikiwa naliangalia ghafla nikajihisi kitu nisichokijua bila ya kukiona kikitoka ndani ya JUA na kunipiga kwenye paji langu la uso na kujihisi km kimefumua kwa nyuma kwenye kisogo, kisha wkt huo huo nikaanza kusikia sauti ikoongea nami toka ndani ya JUA ikiniambia kuwa yeye ni MUNGU mkubwa mwenye namba 666 na amependezwa nami, kwahiyo kuna kitu anataka niuambie ulimwengu. Kwa kweli nilishangaa sana tukio hilo!

Sauti iliniambia mambo mengi kwakweli siwezi kuyaelezea hapa yote. Baada ya hapo hiyo sauti ikawa inanitokea kila mara lakini safari hii hiyo sauti ikawa naisikia kutoka ndani ya kichwa changu sio kutoka nje. Yaani sio km mfano wa kusikia sauti kutoka kwa mtu unaeongea nae, hapana, hiyo sauti nilikuwa safari hii nasikia ndani ya kichwa changu.

Baadae nikaja kusafiri na kwenda kuishi Ujerumani na sasa hivi nna miaka kumi tangu niwe na hilo tatizo cha ajabu ile sauti bado nnayo tu.

Nimejaribu kwenda hospitari lkn bila ya vipimo kwa kusikiliza maelezo yangu tu wakaniambia kuwa nna hiyo SCHIZOPHRENIA. Sasa basi bado najiuliza ni nini hiyo SCHIZOPHRENIA, na kama ni ugonjwa, je kuna uwezekano mtu kupata ugonjwa toka ndani ya JUA? Na cha ajabu madoctor wameniambia kuwa nisimwambie mtu yeyote kuhusu hili tatizo.

Tafadhali waungwana naomba mnishauri nifanye nini ili hii sauti initoke kichwani maana naona wazungu wameshindwa. Pia naumia sana sababu sauti inaniambia mambo mengi ambayo mengine hayapaswi hata kutambulika kwa binaadamu anaendelea kushi hapa duniani!

Asanteni natumaini mtanisaidia!

==============================
MAJIBU
maelezo ya ki layman from wikipedia.

Skizofrenia" ni ugonjwa wa akili unaosababisha fikira na hisia zisizo za kawaida.Watu wengi walio na ugonjwa huu husikia yasiyokuwemo ([kuota njozi]). Watu hawa huwa na woga na makisio yasiyoeleweka. Watu hawa pia wanaweza kuamini mambo ya kiajabu na yasiyoeleweka . Watu hawa wanaweza kuzungumza na kuwaza bila mantiki. Watu hawa huwa na ugumu wa kuhusiana na watu wengine inavyofaa au kudumisha kazi. Dalili kwa kawaida huanza katika ujana baada ya umri wa miaka 16.

Vipengele kadhaa muhimu vinaweza kusababisha skizofrenia. Vipengele hivi ni pamoja na uhusiano wa kijamii na mtu aliye na hali hii, mazingira ya hapo awali ya mtu, mfumo wa neva unaodhibiti mwili na akili ya mtu, na taratibu za kiakili na kijamii. Baadhi yadawa, zikiwemo dawa za kuagiziwa na daktari, zinaweza kusababisha dalili au kuzifanya mbaya zaidi. Utafiti wa hivi sasa unaangazia jukumu la mfumo wa neva ingawa hakuna mtu aliyepata kisababishi hata kimoja cha kiogani kilichojitenga. Miungano mingi ya dalili zinazoweza kutokea imepelekea mjadala kuhusu iwapo ugonjwa huu ni hali moja au hali nyingi tofauti. Neno "skizofrenia" linatokana na maneno mawili ya Griki yanayomaanisha "kugawanya" na "akili". Hata hivyo, skizofrenia haimaanishi "akili iliyogawanyika" wala kusababisha watu kuwa na nafsi nyingi (au "zilizogawanyika"). Watu wengi hushindwa kutofautisha skizofrenia na hali kama hizo

Matibabu hasa ni kwa kutumia dawa ili kupunguza dalili kuu. Dawa hizi husitisha nyendo katika sehemu za ubongo zinazochakata kemikali inayoitwa dopamine. (Baadhi ya dawa hizi pia husitisha shughuli katika sehemu ambazo huchakata kemikali inayoitwaserotonin.) Matibabu ambayo pia ni muhimu ni pamoja na therapi ya kiakili, usaidizi katika kutafuta na kudumisha kazi na pia marekebisho ya kimahusiano. Katika matukio makubwa ambapo kuna hatari kwa mtu binafsi na watu wengine, mtu anaweza kuhitaji kulazwa hospitalini. Hatua hii inaweza kuchukuliwa kwa idhini au bila idhini ya mtu huyu. Hata hivyo, matukio ya kulazwa hospitalini siku hizi yamepunguka na kuwa nadra ikilinganishwa na hapo awali.

Skizofrenia hudhaniwa kuathiri hasa michakato ya kiakili, lakini pia huchangia matatizo ya muda mrefu pamoja na mwenendo na hisia. Watu walio na skizofrenia wana uwezekano wa kuwa na hali zingine pia, zikiwemo mfadhaiko na wasiwasi. Takriban asilimia 50 ya watu walio na skizofrenia hutumia madawa ya kulevya wakati mmoja maishani mwao. Matatizo ya kijamii kama vile ukosefu wa kazi kwa muda mrefu, umaskini na ukosefu wa makao hutokea mara nyingi. Kwa wastani, watu walio na skizofrenia hufa miaka 12 hadi 15 mapema zaidi ya wale wasio na hali hii: Watu walio na skizofrenia wana matatizo ya mwili mengi zaidi, na wana kiwango cha uwezekano wa kujiua cha asilimia 5 zaidi ya watu wa kawaida.
 
maelezo ya ki layman from wikipedia.

Skizofrenia" ni ugonjwa wa akili unaosababisha fikira na hisia zisizo za kawaida.Watu wengi walio na ugonjwa huu husikia yasiyokuwemo ([kuota njozi]). Watu hawa huwa na woga na makisio yasiyoeleweka. Watu hawa pia wanaweza kuamini mambo ya kiajabu na yasiyoeleweka . Watu hawa wanaweza kuzungumza na kuwaza bila mantiki. Watu hawa huwa na ugumu wa kuhusiana na watu wengine inavyofaa au kudumisha kazi. Dalili kwa kawaida huanza katika ujana baada ya umri wa miaka 16.

Vipengele kadhaa muhimu vinaweza kusababisha skizofrenia. Vipengele hivi ni pamoja na uhusiano wa kijamii na mtu aliye na hali hii, mazingira ya hapo awali ya mtu, mfumo wa neva unaodhibiti mwili na akili ya mtu, na taratibu za kiakili na kijamii. Baadhi yadawa, zikiwemo dawa za kuagiziwa na daktari, zinaweza kusababisha dalili au kuzifanya mbaya zaidi. Utafiti wa hivi sasa unaangazia jukumu la mfumo wa neva ingawa hakuna mtu aliyepata kisababishi hata kimoja cha kiogani kilichojitenga. Miungano mingi ya dalili zinazoweza kutokea imepelekea mjadala kuhusu iwapo ugonjwa huu ni hali moja au hali nyingi tofauti. Neno "skizofrenia" linatokana na maneno mawili ya Griki yanayomaanisha "kugawanya" na "akili". Hata hivyo, skizofrenia haimaanishi "akili iliyogawanyika" wala kusababisha watu kuwa na nafsi nyingi (au "zilizogawanyika"). Watu wengi hushindwa kutofautisha skizofrenia na hali kama hizo

Matibabu hasa ni kwa kutumia dawa ili kupunguza dalili kuu. Dawa hizi husitisha nyendo katika sehemu za ubongo zinazochakata kemikali inayoitwa dopamine. (Baadhi ya dawa hizi pia husitisha shughuli katika sehemu ambazo huchakata kemikali inayoitwaserotonin.) Matibabu ambayo pia ni muhimu ni pamoja na therapi ya kiakili, usaidizi katika kutafuta na kudumisha kazi na pia marekebisho ya kimahusiano. Katika matukio makubwa ambapo kuna hatari kwa mtu binafsi na watu wengine, mtu anaweza kuhitaji kulazwa hospitalini. Hatua hii inaweza kuchukuliwa kwa idhini au bila idhini ya mtu huyu. Hata hivyo, matukio ya kulazwa hospitalini siku hizi yamepunguka na kuwa nadra ikilinganishwa na hapo awali.

Skizofrenia hudhaniwa kuathiri hasa michakato ya kiakili, lakini pia huchangia matatizo ya muda mrefu pamoja na mwenendo na hisia. Watu walio na skizofrenia wana uwezekano wa kuwa na hali zingine pia, zikiwemo mfadhaiko na wasiwasi. Takriban asilimia 50 ya watu walio na skizofrenia hutumia madawa ya kulevya wakati mmoja maishani mwao. Matatizo ya kijamii kama vile ukosefu wa kazi kwa muda mrefu, umaskini na ukosefu wa makao hutokea mara nyingi. Kwa wastani, watu walio na skizofrenia hufa miaka 12 hadi 15 mapema zaidi ya wale wasio na hali hii: Watu walio na skizofrenia wana matatizo ya mwili mengi zaidi, na wana kiwango cha uwezekano wa kujiua cha asilimia 5 zaidi ya watu wa kawaida.
 
Wadau naomba mnifahamishe nataka kujiua. Schizophrenia ni nini na wanatambulika vipi watu waliokuwa nayo hapa duniani?

Mnamo tarehe 06/06/2006 nilipata maono nikiwa kule UESPANYA. Maono ya REVELATION. Na baada ya hayo maono kuna siku nilokuwa nimekaa kwenye PARK fulani nikiwa naota JUA kama ilivyokuwa desturi ya watu tunaoishi huku.

Nikiwa nimekaa kwenye bench naota JUA huku nikiwa naliangalia ghafla nikajihisi kitu nisichokijua bila ya kukiona kikitoka ndani ya JUA na kunipiga kwenye paji langu la uso na kujihisi km kimefumua kwa nyuma kwenye kisogo, kisha wkt huo huo nikaanza kusikia sauti ikoongea nami toka ndani ya JUA ikiniambia kuwa yeye ni MUNGU mkubwa mwenye namba 666 na amependezwa nami, kwahiyo kuna kitu anataka niuambie ulimwengu. Kwa kweli nilishangaa sana tukio hilo!

Sauti iliniambia mambo mengi kwakweli siwezi kuyaelezea hapa yote. Baada ya hapo hiyo sauti ikawa inanitokea kila mara lakini safari hii hiyo sauti ikawa naisikia kutoka ndani ya kichwa changu sio kutoka nje. Yaani sio km mfano wa kusikia sauti kutoka kwa mtu unaeongea nae, hapana, hiyo sauti nilikuwa safari hii nasikia ndani ya kichwa changu.

Baadae nikaja kusafiri na kwenda kuishi Ujerumani na sasa hivi nna miaka kumi tangu niwe na hilo tatizo cha ajabu ile sauti bado nnayo tu.

Nimejaribu kwenda hospitari lkn bila ya vipimo kwa kusikiliza maelezo yangu tu wakaniambia kuwa nna hiyo SCHIZOPHRENIA. Sasa basi bado najiuliza ni nini hiyo SCHIZOPHRENIA, na kama ni ugonjwa, je kuna uwezekano mtu kupata ugonjwa toka ndani ya JUA? Na cha ajabu madoctor wameniambia kuwa nisimwambie mtu yeyote kuhusu hili tatizo.

Tafadhali waungwana naomba mnishauri nifanye nini ili hii sauti initoke kichwani maana naona wazungu wameshindwa. Pia naumia sana sababu sauti inaniambia mambo mengi ambayo mengine hayapaswi hata kutambulika kwa binaadamu anaendelea kushi hapa duniani!

Asanteni natumaini mtanisaidia!
 
Ni kama inability ambayo mtu anakuwa nayo mara nyingi anashindwa kutofautsha reality na imagination...chanzo kikuu hakijajulikana ila inasadikika ni genetic issue za mtu...kuna theory nyng kuhusu hii kitu...
 
Ni kama inability ambayo mtu anakuwa nayo mara nyingi anashindwa kutofautsha reality na imagination...chanzo kikuu hakijajulikana ila inasadikika ni genetic issue za mtu...kuna theory nyng kuhusu hii kitu...
Sawa ndugu nashukuru kwa kutaka kunifahamisha lkn nafikiri uenda ikawa unajuwa zaidi kuhusu hii kitu kwaiyo naitaji ufafanuzi zaidi kuhusu hii kitu, pls!
 
Mkuu hiyo ni schizophrenia, mojawapo ya dalili zake ni hallucinations (yaani kuona au kusikia vitu ambavyo kiuhalisia havipo) mf. Ulipokuwa unaona mtu kwenye jua (visual hallucination) na hiyo sauti kwenye ubongo ni auditory hallucination
 
Schizophrenia ni ugonjwa wa akili ambao huathiri jinsi watu wanavyofikiri, wanavyoona, wanavyohisi au wanavyoielewa dunia inayowazunguka. Dalili za msingi za schizophrenia ni hallucination(kuona au kusikia vitu amabavyo havipo katika mazingira ya kawaida mfano kuona kitu ambacho mtu mwingine hakioni/hakipo).

Kwa kawaida, dalili huwa zinagawanywa katika makundi mawili; dalili chanya na dalili hasi.

Dalili chanya ni hallucination, kushindwa kupangilia mazungumzo/mazungumzo yasioeleweka pia kushindwa kupangilia tabia/tabia zisizoeleweka. Tabia hasi ni kushindwa kuzungumza, kujitenga, kutokuwa hisia.

Pia wagonjwa wa schizophrenia huweza kuwa na huzuni au furaha kupita kiasi isiyoeleweka. Hakuna kipimo cha maabara kinachoweza kupima km una Schizo. Ili daktari aweze kusema kuna listi ya tabia/dalili za schizo huwa nazo na ukiwa na dalili 2 au zaidi kwenye hizo basi wewe utakuwa na schizophrenia na dalili hizo lzm ziwepo kwa miezi 6 au zaidi..

Matibabu yapo ila inashauriwa kutoanza na dawa kwanza ila phychosocial support ndo msaada... Dawa kama clozapine husaidia tatizo kutojirudia!!
 
Schizophrenia ni ugonjwa wa akili ambao huathiri jinsi watu wanavyofikiri, wanavyoona, wanavyohisi au wanavyoielewa dunia inayowazunguka. Dalili za msingi za schizophrenia ni hallucination(kuona au kusikia vitu amabavyo havipo katika mazingira ya kawaida mfano kuona kitu ambacho mtu mwingine hakioni/hakipo).

Kwa kawaida, dalili huwa zinagawanywa katika makundi mawili; dalili chanya na dalili hasi.

Dalili chanya ni hallucination, kushindwa kupangilia mazungumzo/mazungumzo yasioeleweka pia kushindwa kupangilia tabia/tabia zisizoeleweka. Tabia hasi ni kushindwa kuzungumza, kujitenga, kutokuwa hisia.

Pia wagonjwa wa schizophrenia huweza kuwa na huzuni au furaha kupita kiasi isiyoeleweka. Hakuna kipimo cha maabara kinachoweza kupima km una Schizo. Ili daktari aweze kusema kuna listi ya tabia/dalili za schizo huwa nazo na ukiwa na dalili 2 au zaidi kwenye hizo basi wewe utakuwa na schizophrenia na dalili hizo lzm ziwepo kwa miezi 6 au zaidi..

Matibabu yapo ila inashauriwa kutoanza na dawa kwanza ila phychosocial support ndo msaada... Dawa kama clozapine husaidia tatizo kutojirudia!

Asante nashukuru ndg! Lkn je hili tatizo linahusiano wowote na spirity na km ndio spirity yake ni mbaya au nzuri?

Sababu pia nimejaribu kufuatilia jinsi watu wanavyoliongelea hili tatizo kwenye google nimekuta watu wanalizungumzia kwa hisia tofauti wengine wanasema hii sauti niliokuwa nayo ni ya Allah yaani MUNGU kwa waislam na wengine wanasema ni Jini supernature ambae anapatikana kwenye msahafu na anatambulika kwa alama zake za namba 666 ambazo kwa kulingana na maono yangu hapo mwanzo ni ilikuwa 06/06/2006.

Na pia ndugu niliendelea kufuatilia na wengine wanasema kuwa Yesu Kristo na mtume Muhammad nao inasemekana walikuwa na schizophrenia. Afu istoshe kwenye hayo maono yangu nilikuwa najihisi kama Yesu na kuona kuwa ulimwengu mzima unanisujudia na kila upande yaani wa wazungu na waarabu na watu wa mataifa yote wakinigombania.

Pia iyo sauti kichwani inaniambia kuwa yeye ni MUNGU wa 666 ambapo pia nikifikilia nguvu zote za watu wanaouongoza huu ulumwengu ni wanatumia nguvu za 666 ambazo wapo watu wengine wanasema ni BLACK POWER na wapo wengine wanasema ni BLACK magic .

Pia nishawahi kusikiliza docomentry moja ya Bob Marley alikuwa amesema kila muaminifu ambae anakubalika kwa MUNGU lazima anatakiwa awe na sauti kichwani inaongea nae kila wakati. Pia ktk history ya ibaada ya kikristo ya SUNDAY nasikia walikuwa wanamuabudu MUNGU wao enzi hizo wakiamini kuwa yupo ktk JUA .

Sasa swali linakuja, ikiwa Tanzania inasemekana ni sehemu ambapo fuvu la binadamu wa kwanza lilipopatikana, huoni kuwa labda MUNGU anataka uokovu wa ulimwengu utokane na mtu fulani kutoka Tanzania?

Kwa kweli najielewa afu sijielewi kutokana na mengi yanayozungumzwa na watu kuhusu hii 666 ikiambatanishwa na hii sauti!

Naomba ushauri wa mwisho na mniambie mimi nitakuwa ni mtu wa aina gani, sababu najua humu kwenye JF kuna watu wanavichwa saana pia! Niambieni bila ya woga jamani wa kusema huenda mkanitisha.

Asanteni.
 
Pole sana muhimu huzuria ibada kutokana na imani yako na pia jaribu kutafuta kiongozi wa dini awe anakushauri na kusali pamoja
 
Asante nashukuru sana kwa ushauri wako ndg !
Asante nashukuru sana kwa ushauri wako ndg !
Kuna ndugu mmoja humu anaitwa Kaka MNEPHA nilikuwa nakuomba kaka mnepha kama unaona hili tatizo langu naomba unisaidie kuniambia chochote kile sababu nakuamini sana kwa upeo uliokuwa nao asa pale ulipozungumzia swala la BLACK HOLE. km upo naomba uniambie kitu sababu siamini madheebu yoyote yale ya dini !
 
Kuna ndugu mmoja humu anaitwa Kaka MNEPHA nilikuwa nakuomba kaka MNEPHA kama unaona hili tatizo langu naomba unisaidie kuniambia chochote kile sababu nakuamini sana kwa upeo uliokuwa nao asa pale ulipozungumzia swala la BLACK HOLE . km upo naomba uniambie kitu sababu siamini madheebu yoyote yale ya dini !
Kwenye jua uliona dubwasha gani?

Unaweza kulielezea likoje?
 
Schizophrenia is an severe mental disease which it's source is unknown ,, this disease is characterized by presence of the common symptom which is hallucinations
 
Niliwahi sikiliza mhadhara mmoja nikamsikia shekhe akisema kuwa namba 666 ni namba ya kishetani...akasema namba hii hutumika kwenye shughuli za Freemason, akataja vifungu mbalimbali kwenye biblia kimojawapo kilisema watu 666 waingizwe motoni (ikiwa kumbukumbu yangu nzuri) kiujumla hiyo namba aliihusishwa na watu wanaomuabudu shetani ambao ndiyo hao waumini wa Freemason!
 
MUNGU mkubwa mwenye namba 666 amekuchagua? Pia unasema uliona maono? Mi nadhani tatizo lako ni la kiroho zaidi achana na hospitali tafuta ufumbuzi kwa watu wa imani
 
Niliwahi sikiliza mhadhara mmoja nikamsikia shekhe akisema kuwa namba 666 ni namba ya kishetani...akasema namba hii hutumika kwenye shughuli za Freemason, akataja vifungu mbalimbali kwenye biblia kimojawapo kilisema watu 666 waingizwe motoni (ikiwa kumbukumbu yangu nzuri) kiujumla hiyo namba aliihusishwa na watu wanaomuabudu shetani ambao ndiyo hao waumini wa Freemason!
Duuh, I don't believe smthng like that in my mind!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom