Sayansi ya uchawi na umbile lake

Sayansi ya uchawi na umbile lake

ambao ni bongolala kama mimi hakuna tulichokielewa hapa hata lengo la mtoa post bado sijalielewa nimeona tu mablaa blaa ambayo sijui hata yanalenga ku portray nini
Asante, kwa kutoa dukuduku lako na pia naelewa lugha iliyotumika hapa kwenye uzi ni ngumu na ya kitaalamu zaidi, ntajaribu kukufafanulia kwa lugha rahisi hili watu wengi waweze kuelewa kilichoandikwa.

Ninazungumzia uwepo wa ulimwengu zaidi ya mmoja tunao-ufahamu katika eneo hili hili moja tunaloishi, yaani kuna dunia ambayo tunaishi sisi (inayoonekana) pia kuna ulimwengu mwingine wanaoishi viumbe vya kiroho wa nuru (malaika) na wa gizani (majini/mapepo) usioonekana.

Viumbe malaika wa mwangaza wao utoa ushirikiano kwa mtu anayewaomba kwa dhati pasipo mikataba umiza wakati wale wa gizani kila wanachokutendea kina malipo yake na kwa kuwa njia pekee ya kumtawala binadamu ni kumiliki tamaa ya moyo wake basi wanaitumia vyema kama silaha ya kumchapia mshirikina.

Mchawi akishajiingiza katika mikataba ya kichawi basi atamtumikisha jini kumfanyia lolote lile alitakalo kipindi akiwa hai na anao mwili na jini atafanya kila kitu ila pindi akishaupoteza mwili kwa maana ya kufa basi anageuzwa mtumwa na lile jini na atamtumikia jini uyo na uzao wake.

Ndiyo maana kuna neno kurithishana mikoba au kutoa kafara na sadaka kwa mizimu ya ukoo (hiyo mizimu inayotamkwa ndiyo hao majini wenye maagano na mchawi) na wasipotimiziwa mahitaji yao uendelea kuandama ukoo huo kizazi hata kizazi.

Hiki ndicho umfanya mchawi haogope mno suala la kufa kuliko kitu kingine chochote kile, na mara nyingi wachawi wengi uhakikisha wanaishi umri mrefu mno iwezekanavyo.

Na ufa uzeeni sana wakiwa vibibi au vibabu kizee na uepuka mno mazingira yanayoweza kuwafanya wakafa mapema ikiwemo anasa,kusafiri mara kwa mara,kupigana,n.k

Wao ujifanisha kuwa wapatanishi, wakarimu na watu wa watu, hawakosi kwenye nyumba za ibada na shughuli za kijamii na huwa ni watu wa kutegemewa na kuzungumziwa vizuri na kila mtu hii yote ni defence mechanism ili wasishtukiwe na kudhurika.

Pia wengi upendelea kuishi maisha ya kimaskini na asili, utumia sana tiba za mitishamba kujiagua, utafuta hirizi au kujiganga kiasi kwamba hata ikitokea akinasika hata apigwe vipi akati roho mpaka haitoe ile dawa ndipo afe kwa sababu anajua adhabu yake akishakufa na alishaiuza nafsi yake ni kimbembe.

Nadhani inatosha kwa hapo hayo mengine yaliyobakia hayaitaji ufafanuzi kwa kuwa yatazua taharuki za kiimani.
 
Asante, kwa kutoa dukuduku lako na pia naelewa lugha iliyotumika hapa kwenye uzi ni ngumu na ya kitaalamu zaidi, ntajaribu kukufafanulia kwa lugha rahisi hili watu wengi waweze kuelewa kilichoandikwa.

Ninazungumzia uwepo wa ulimwengu zaidi ya mmoja tunao-ufahamu katika eneo hili hili moja tunaloishi, yaani kuna dunia ambayo tunaishi sisi (inayoonekana) pia kuna ulimwengu mwingine wanaoishi viumbe vya kiroho wa nuru (malaika) na wa gizani (majini/mapepo) usioonekana.

Viumbe malaika wa mwangaza wao utoa ushirikiano kwa mtu anayewaomba kwa dhati pasipo mikataba umiza wakati wale wa gizani kila wanachokutendea kina malipo yake na kwa kuwa njia pekee ya kumtawala binadamu ni kumiliki tamaa ya moyo wake basi wanaitumia vyema kama silaha ya kumchapia mshirikina.

Mchawi akishajiingiza katika mikataba ya kichawi basi atamtumikisha jini kumfanyia lolote lile alitakalo kipindi akiwa hai na anao mwili na jini atafanya kila kitu ila pindi akishaupoteza mwili kwa maana ya kufa basi anageuzwa mtumwa na lile jini na atamtumikia jini uyo na uzao wake.

Ndiyo maana kuna neno kurithishana mikoba au kutoa kafara na sadaka kwa mizimu ya ukoo (hiyo mizimu inayotamkwa ndiyo hao majini wenye maagano na mchawi) na wasipotimiziwa mahitaji yao uendelea kuandama ukoo huo kizazi hata kizazi.

Hiki ndicho umfanya mchawi haogope mno suala la kufa kuliko kitu kingine chochote kile, na mara nyingi wachawi wengi uhakikisha wanaishi umri mrefu mno iwezekanavyo.

Na ufa uzeeni sana wakiwa vibibi au vibabu kizee na uepuka mno mazingira yanayoweza kuwafanya wakafa mapema ikiwemo anasa,kusafiri mara kwa mara,kupigana,n.k

Wao ujifanisha kuwa wapatanishi, wakarimu na watu wa watu, hawakosi kwenye nyumba za ibada na shughuli za kijamii na huwa ni watu wa kutegemewa na kuzungumziwa vizuri na kila mtu hii yote ni defence mechanism ili wasishtukiwe na kudhurika.

Pia wengi upendelea kuishi maisha ya kimaskini na asili, utumia sana tiba za mitishamba kujiagua, utafuta hirizi au kujiganga kiasi kwamba hata ikitokea akinasika hata apigwe vipi akati roho mpaka haitoe ile dawa ndipo afe kwa sababu anajua adhabu yake akishakufa na alishaiuza nafsi yake ni kimbembe.

Nadhani inatosha kwa hapo hayo mengine yaliyobakia hayaitaji ufafanuzi kwa kuwa yatazua taharuki za kiimani.
Sasa huyu Mchawi anatoa ishara gani kikawaida. Mana mm niliwahi kugombana na mtu siku ya pili nikafukuzwa kazi Kenge yule
 
kwahiyo unaeza somea uchawi wa sayansi
Uchawi ni sayansi ambayo inagawanyika katika aina kuu mbili yaani uchawi mweusi na uchawi mweupe.

Uchawi mweusi ule wa kuwanga usiku na kutupia watu majini kuwatia mabalaa wengi wetu tunautambua kama ndiyo uchawi.

Lakini uchawi mweupe ule unaofanyika hadharani madhabahuni, unaofundishwa darasani kwenye masomo ya sayansi na biashara, matendo yenye nia ya kupumbaza akili au tahajudi n.k

Kwetu tunachukulia kuwa si uchawi bali sayansi au uwezo fulani tusio jua chanzo chake na tunavutiwa kuufanya uchawi huo pasipo kuhoji wala kuwa na mashaka nao.
 
Sasa huyu Mchawi anatoa ishara gani kikawaida. Mana mm niliwahi kugombana na mtu siku ya pili nikafukuzwa kazi Kenge yule
Mchawi hana ishara na kumtambua labda uwe na uwezo wa asili wa kutambua uchawi au na wewe huwe ni mshirikina vinginevyo simamia kile anachokiamini ili usitetereke.
 
Mchawi hana ishara na kumtambua labda uwe na uwezo wa asili wa kutambua uchawi au na wewe huwe ni mshirikina vinginevyo simamia kile anachokiamini ili usitetereke.
Sasa mkuu Nina shida hapa Kuna mtu nahisi anakuja kuniwangia usiku. Natakiwa nifanyeje kumkomoa?
 
Hivi mwisho wa maamuma au watu wasiojua chochote kiroho, watu wasio wachawi wala wafanya ibada mwisho wao wakitoka mwilini huwa upande gani?
Ni swali fikirishi kidogo kwa kuwa asiyejua chochote na wala ajayaishi maisha yake kwa kuchagua upande hana chakupoteza wala kuongeza pindi akifa,

Isipokuwa ikiwa hukumu yake itaamuliwa na pande mbili kinzani basi watamjaji kwa kigezo cha matendo yake je yalikuwa mema au mabaya?

Kama itaonekana pengine somo alilopaswa kujifunza akulielewa then atapewa second chance kwa wale wanaoamini reincarnation wanajua ninachomaanisha.

Na kwa namna nyingine mi nafikiri mtu huyu kwa upande mwingine amejiepusha au kajiondosha katika vifungo au shtaka lisilomuhusu na kujali muda wake kuishi kama binadamu/kiumbe hai asiye na ushirika na chochote kile akiishi kama asili inavyotaka hivyo hawajibiki kwa yeyote wala kuwajibika kwa chochote kile pindi akifa yameishia hapo.
 
Aiseeeeeee...nashangaa sana mtu anaposema kuwa SHETANI ni nadharia tu hayupo.!
Ushetani upo na ni nguvu kubwa inayotawala pakubwa katika ulimwengu huu kama ilivyo nguvu ya Mungu, Mkanda unaotenganisha tawala hizi mbili ni mwembamba sana kiasi kwamba unaweza dhani unamtumikia Mungu kumbe unamwabudu na kumuhusudu shetani.
 
Naona mkuu Kuna uhusiano mkubwa mnoo wa uchawi na elimu nyota. Hii Ina misingi ipi hasa kwenye mipango ya kuangamiza
"Elimu nyota" ni fumbo kumaanisha elimu ya muingiliano wa binadamu na majini (viumbe vya kiroho ambavyo havionekani kwa macho)
NB: Kwa taarifa zaidi kuwajua viumbe nyota fuatilia uzi wangu wa Je, upi ni msingi wa falsafa ya Freemasons?
 
Asante, kwa kutoa dukuduku lako na pia naelewa lugha iliyotumika hapa kwenye uzi ni ngumu na ya kitaalamu zaidi, ntajaribu kukufafanulia kwa lugha rahisi hili watu wengi waweze kuelewa kilichoandikwa.

Ninazungumzia uwepo wa ulimwengu zaidi ya mmoja tunao-ufahamu katika eneo hili hili moja tunaloishi, yaani kuna dunia ambayo tunaishi sisi (inayoonekana) pia kuna ulimwengu mwingine wanaoishi viumbe vya kiroho wa nuru (malaika) na wa gizani (majini/mapepo) usioonekana.

Viumbe malaika wa mwangaza wao utoa ushirikiano kwa mtu anayewaomba kwa dhati pasipo mikataba umiza wakati wale wa gizani kila wanachokutendea kina malipo yake na kwa kuwa njia pekee ya kumtawala binadamu ni kumiliki tamaa ya moyo wake basi wanaitumia vyema kama silaha ya kumchapia mshirikina.

Mchawi akishajiingiza katika mikataba ya kichawi basi atamtumikisha jini kumfanyia lolote lile alitakalo kipindi akiwa hai na anao mwili na jini atafanya kila kitu ila pindi akishaupoteza mwili kwa maana ya kufa basi anageuzwa mtumwa na lile jini na atamtumikia jini uyo na uzao wake.

Ndiyo maana kuna neno kurithishana mikoba au kutoa kafara na sadaka kwa mizimu ya ukoo (hiyo mizimu inayotamkwa ndiyo hao majini wenye maagano na mchawi) na wasipotimiziwa mahitaji yao uendelea kuandama ukoo huo kizazi hata kizazi.

Hiki ndicho umfanya mchawi haogope mno suala la kufa kuliko kitu kingine chochote kile, na mara nyingi wachawi wengi uhakikisha wanaishi umri mrefu mno iwezekanavyo.

Na ufa uzeeni sana wakiwa vibibi au vibabu kizee na uepuka mno mazingira yanayoweza kuwafanya wakafa mapema ikiwemo anasa,kusafiri mara kwa mara,kupigana,n.k

Wao ujifanisha kuwa wapatanishi, wakarimu na watu wa watu, hawakosi kwenye nyumba za ibada na shughuli za kijamii na huwa ni watu wa kutegemewa na kuzungumziwa vizuri na kila mtu hii yote ni defence mechanism ili wasishtukiwe na kudhurika.

Pia wengi upendelea kuishi maisha ya kimaskini na asili, utumia sana tiba za mitishamba kujiagua, utafuta hirizi au kujiganga kiasi kwamba hata ikitokea akinasika hata apigwe vipi akati roho mpaka haitoe ile dawa ndipo afe kwa sababu anajua adhabu yake akishakufa na alishaiuza nafsi yake ni kimbembe.

Nadhani inatosha kwa hapo hayo mengine yaliyobakia hayaitaji ufafanuzi kwa kuwa yatazua taharuki za kiimani.
Kuomba hao malaika wazuri unatumia njia gani?

Na kwa nini uchawi haufanyi kazi kwenye vitu kama benki au vita?
 
Shida kubwa ya haya mambo hata ukielezea na kuandika hata kurasa zaidi ya mia,,,Mwisho tutahitaji uthibitisho tuu,ili utuaminishe ya kwamba uliyo eleza au kuyaandika ukweli wake ni upi nasi tushuhudie ili ututoe tuu wasiwasi ya kwamba uliyoeleza au kuyaandika ni kweli!!!
 
Mtu akifa roho yake inaenda wapi?? Hapo umesema mchawi ataenda kumtumikia jini wake, na asiekua mchawi??
Na anamtumikia huyo jini kwenye mambo yapi hasa??
 
Kuomba hao malaika wazuri unatumia njia gani?

Na kwa nini uchawi haufanyi kazi kwenye vitu kama benki au vita?

Kuomba viumbe roho "WEMA" msaada funguo ni "kutenda mema" sasa itategemea na medium au njia unayotumia wewe kutenda mema ili uombe mema yatokee katika maisha yako mfano wengine usali katika imani zao wakihusisha miungu, wengine ujali wenye uhitaji nakusaidia wasio jiweza,wengine uishi kwa upendo, n.k

Nani kasema uchawi haufanyi kazi benki au vitani, kote huko uchawi ufanya kazi yake vyema tu na kinachozuia uchawi usionekane kufanya kazi huko ni kwa kuwa uchawi tiyari uko installed maeneo hayo ukifanya kazi yake, sasa kuna haja gani ya kuongeza juu ya
 
Vile vyenye kiapo mkuu??????Au ukula kiapo wewe kwenye ulimwengu ule???
Hivyo viapo unavyovitaka wewe ni sehemu ya siri za uchawi na tiyari nimeshagusia (wenda kama unataka nifundishe watu uchawi) kuwa hili uwe mchawi pale unapoudhuria kikao au cerebration ya kichawi unapatanishwa na jini utakaye mtumia kama kijakazi wako kwenye shughuli zako ziwe za kuwanga au kuagua ambaye utaingia nae maagano au mikataba ya kichawi.
 
Mtu akifa roho yake inaenda wapi?? Hapo umesema mchawi ataenda kumtumikia jini wake, na asiekua mchawi??
Na anamtumikia huyo jini kwenye mambo yapi hasa??
Binadamu yeyote yule kama alivyo kiumbe hai wa namna yeyote yule kifizikia ana muda wa kuishi na kufa hata afanye nini.

Ila linapokuja suala la kifo kuna kifo ambacho ni natural death kwa maana ya kifo halisi ambacho hakiepukiki na kifo kilichosababishwa na mazingira ya kichawi, visasi, ajali n.k

Roho zinazokatishwa maisha yake hapa duniani kabla ya muda wake ule rasmi kutimia uendelea kusurvive pasipo mwili unaoonekana kwa macho ya kawaida katika plane ya chini ambayo ni mbingu ya giza totoro (tabaka lililo chini ya mamlaka ya malaika muasi/shetani na jeshi lake)

Roho hizi mara nyingi huendelea kutangatanga bila makao katika plane giza na zingine ni zile ambazo zime-hold ndani yake chuki, simanzi, visasi,maagano n.k

Sasa unapokuwa kama binadamu huna mwili tena umebakia roho na roho yako haijapanda katika plane maalumu ya watu wanaotambulika kuwa wametangulia mbele za haki (waliopumzishwa), unakuwa kwenye mtihani wa shetani ukiwa huna namna ya kujitetea.

Kinachoweza kuiokoa nafsi yako isiteseke au kutumiwa na wachawi katika shughuli zao za kishirikina ( na kunyakuliwa na malaika wenye makazi yao ndani ya tabaka la mwanga) itategemea sana maisha uliyoyaishi pindi ukiwa hai kabla ya kufikwa na mauti hayo (ndiyo maana tunaimizwa muda wote kuishi vyema na kwa upendo, kutowazia mabaya na tusamehe mara kwa mara)

Kiufupi kama unaamini mtu aliumbwa na Mungu basi mwenye kuweza kuichukua pumzi hiyo ni Mungu peke yake na siyo kiumbe mwingine yeyote.

Isipokuwa viumbe hawa tusiowaona wanao uwezo tu wa kufanya mazingaombwe ya kuufanya mwili wako usiwe visible kifizikia ili wakakutumikishe wapendavyo katika ulimwengu wao wa kishirikina mpaka ile siku rasmi ya kifo chako itakapowadia.

Hivyo basi mchawi analitambua vyema hilo kuwa biashara ni mbadilishano kuwa leo anakula yeye kesho analiwa yeye na hana namna ya kulikwepa hilo.
 
Uchawi ni sayansi ambayo inagawanyika katika aina kuu mbili yaani uchawi mweusi na uchawi mweupe.

Uchawi mweusi ule wa kuwanga usiku na kutupia watu majini kuwatia mabalaa wengi wetu tunautambua kama ndiyo uchawi.

Lakini uchawi mweupe ule unaofanyika hadharani madhabahuni, unaofundishwa darasani kwenye masomo ya sayansi na biashara, matendo yenye nia ya kupumbaza akili au tahajudi n.k

Kwetu tunachukulia kuwa si uchawi bali sayansi au uwezo fulani tusio jua chanzo chake na tunavutiwa kuufanya uchawi huo pasipo kuhoji wala kuwa na mashaka nao.
Uchawi sio sayansi.
 
Hivyo viapo unavyovitaka wewe ni sehemu ya siri za uchawi na tiyari nimeshagusia (wenda kama unataka nifundishe watu uchawi) kuwa hili uwe mchawi pale unapoudhuria kikao au cerebration ya kichawi unapatanishwa na jini utakaye mtumia kama kijakazi wako kwenye shughuli zako ziwe za kuwanga au kuagua ambaye utaingia nae maagano au mikataba ya kichawi.
Umegusia juu juu,wape watu experience in the day of taking oath inakuaje???
 
Back
Top Bottom