Sauti ya simu yangu iko chiiini sana!

wende

JF-Expert Member
Sep 6, 2009
714
65
Salaam kwa wana JF wote!
Ni kuwa wakati napiga simu,mpokeaji/receiver ananisikia kwa mbali/shida sana (i.e. sauti yangu inakuwa chini mno). Wakati huo mimi nakuwa namsikia vizuri sana! Inafika muda kila ninayempigia simu,lazima aniambie niongeze sauti ili anisikie vizuri. Kuna wakati fulani mpaka inakuwa kero maana natumia energy kubwa sana ili nisikike clear. Simu yenyewe ni NOKIA ya kichina. Nisaidieni jamani,nifanye nini na hichi kimeo cha kichina ili niweze kusikika vizuri kwa wote ninaowapigia?????. P/se naomba kuwasilisha.
 
Mchina atakufanya uonekane mwenda wazimu kwa kuongea kwa sauti ya juu eti kisa usikike vizuri,

ni heri kuwa na simu ya kawaida tu tena ya bei nafuu kuliko kuwa na simu ya kichina.
 
Jaribu kuangalia voice effect kwanza hakikisha ipo nomal.ikigoma fuata ushauri wa hapo juu kubadili mic.
 
inatatizo la mic peleka kwa fundi alokaribu nawe kama upo dar tuwasiliane
 
Jombi hapo umekwepa !
Apo No! Siwezi kuwa na hasira za namna hiyo!
ha! ha! ha! ha! Uwiii !!! Umegoma ushauri wa kuvunjavunja.jaama kasahau kuwa sisi wabongo hatuna tabia hiyo ya islafu.tabia yetu mtu unapo nunua simu huwa tunakuwa kama tumefunga nayo ndoa maana ikiahariba siitupi napeleka kwa fundi.housing ikibenjuka kidogo nafunga rababendi kama vp ninaibamba na supa gluu.yaani simu inakuwa na vilaka kama yale mashati ya zamani ya bahama teh!teh! Hata iharibike iwe haina network poa tu bado inafaa kusikilizia miziki. Miziki nayo ikigoma inatumika kama tochi.
 
Back
Top Bottom