SAUTI YA KIVULI

SAUTI YA KIVULI

Joined
Dec 27, 2018
Posts
60
Reaction score
105
SURA YA KWANZA
MLANGO WA TANO
MIAKA MITATU BAADAE
TSS HQ-DAR ES SALAAM
Nchi ilikuwa imetulia na kurejea katika hali yake ya utulivu kama ilivyokabidhiwa na waasisi wa taifa hili pindi walipoamua kung'atuka katika nafasi zao na kuwa kama wananchi wengine, watu walikuwa bize kuinua uchumi wao na nchi kwa ujumla, kwasababu amani na ulinzi vili tamalaki ijapokuwa ilikuwa imesalia miezi kadhaa kabla ya uchaguzi mkuu wa raisi, wabunge na madiwani, katika idara nyeti ya ujasasi kulikuwa na kikao kilichokuwa kinaendelea.


"jamani nimewaiteni hapa kuwaelezea mambo machache ijapokuwa kuna mengi tu tumekuwa tuki habarishana mara kwa mara ila siyo kwamba ndiyo iwe mazoea, ijapokuwa bahari imetulia haina maana ndiyo tujisahau na kukiachia chombo kielee maana hatujui ni muda gani na wimbi la namna gani litatuyumbisha, hasa ukiangalia mwakani mwezi wa kumi na mbili ni mwezi utakaofanyika uchaguzi mkuu niwaombe tu kama ni umakini uwe mara mbili ya vile tuliokuwa nao mwanzo" aliongea Chifu huku akiweka kituo na kupiga funda kubwa la maji kisha akawatazama watu waliokuwa mle ndani katika nyuso zao kisha akamgeukia jenerali na kisha akampa ishara atoe neno.


'kwanza nitoe pongezi kwako wewe mkurugenzi wa idara ya ujasusi. kwa maana bila mbinu zako nadhani hivi sasa tungekuwa tunaongelea mengine, nasema hivi nikiwa na uhakika kwamba mbali na kuwa ulinzi umeimarishwa kila mahali kiasi kwamba ukidondosha noti ya elfu kumi hata ukirudi kesho yake unaikuta kama ulivyoidondosha, kama nilivyosema mwanzo jicho letu halitasinzia kuhakikisha haturudi kule tulipokuwa" aliongea jenerali huku akiwatazama wajumbe walioko ndani ya chumba kile kisha akagandisha macho yake katika uso wa chifu aliyeishia kutabasamu na kukubaliana na kile kijana wake anacho kizungumzia.


"nashukuru kama na wenzangu kama mmeweza kuliona hilo nina imani kabisa sasa hivi tunaongea lugha moja na hakuna kati yetu atakayeleta uzembe katika upande wake, hatutakuwa na uvumilivu kwa kiongozi yeyote atakayeufanya usingizi wetu uwe kitendawili, baada ya kusema hivyo nadhani tungeendelea kutekeleza majukumu yetu ipasavyo ikiwa kama hakuna mwenye swali" kufikia hapo akaupisha ukimya uliomeza fikra za viongozi wale wa vyombo vya ulinzi na usalama,ndani ya dakika moja waliafikiana kikao kile kiishie pale na baada ya dakika mbili simu yake ilitekenya kwenye mifuko yake akaitoa na kuipokea.


"ubavu wa yule msaliti umeonekana mwanza, amekuwa mama ntilie mitaa ya kiwanda cha soda.......tunasubiri neno moja kutoka kwenye kinywa chako akapate malipo yake Butimba" ilizungumza sauti nzito huku ikisubiri kinywa cha mtu aliyekuwa upande wa pili.


"nalitambua hilo ila hatuna haraka naye, bado tunafatilia nyendo zake ili tuweze kupata samaki mkubwa huyu ni dagaa tu muda ukifika nitakupa maelekezo" alizungumza Chifu kwa utulivu


"sawa mkuu tunaendelea kuzitazama nyayo zake na ripoti itakufikia mezani mkuu kama ataonyesha mabadiliko yoyote hatutakuwa wavumilivu ila atakuja kuwatapika kwa lazima ni hayo tu" ilisema sauti ya upande wa pili


"lets wait and see, ila hakikisha unapozichunguza nyayo zake hakikisha hatambui, unajua upo kimkakati na utambue unazifata nyayo za jasusi aliyebobea, be carefully ofisa.....titititi" simu ilikatwa na kumfanya mtu yule ashushe pumzi nyingi, na kunyoosha mikono yake juu ya meza kubwa ya ofisi na ya kisasa.


POLICE CENTRAL-DAR ES SALAAM


saa 8:15 mchana.


"ndugu waandishi wa habari, tumewaalika leo, kuapa taarifa mbalimbali zinazohusu hali ya usalama wa raia na mali zao vile vile hatua madhubuti tutakazo chukua na zilizochukuliwa, jeshi la polisi kanda maalum ya dar es salaam kwa takribani mwezi mmoja uliopita tuliendesha oparesheni ya kuwabaini, kuwatia nguvuni, kuwahoji na kuwafikisha katika vyombo vya sheria wahalifu hao, nipende kusema hadi hii leo tumefanikiwa kuwakamata wahalifu wapatao kumi na saba(17) na muda wowote watafikishwa mahakamani." alimeza kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam Chacha Msamalo kimincha.


"hilo ni moja mbili, ndugu waandishi wa habari na wananchi wa Dar es salaam kwa takribani wiki mbili zilizopita tulikuwa tukisumbuliwa na wimbi la uporaji mali kwa kutumia silaha na mauaji, huku lawama kubwa tukielekezewa sisi kwenye mitandao mbali mbali ya kijamii kwa ukubwa wa jambo hili, jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola tuliweza kuwakamata watu wanane, tumewafanyia mahojiano ya kina na waliwataja watu wawili kama viongozi wao wanaowafadhili kiuchumi na silaha za kufanyia uhalifu kuwa ni SAIDI BANDIKA,mfanyabiashara na mmiliki wa timu ya mpira wa miguu iitwayo Sungura na ndugu Elvyn byashalila, mbunge wa afrika mashariki na mwenyekiti wa makampuni ya Embetogwa yanayojishulisha na utengenezaji wa bidhaa mbalimbali."


"watuhumiwa hao kwa nyakati tofauti tofauti kuanzia sasa watafikishwa katika vyombo vya sheria vile vile nitoe rai kwa wananchi wote kwa ujumla kuweza kushirikiana na jeshi la polisi katika kufichua na kupambana na uhalifu bila kuoneana aibu, na pia nitoe onyo kwa wote wanaojishughulisha na uhalifu kuwa tutakabiliana nao na watapata wakati mgumu sana, Asanteni kwa kunisikiliza" alimalizia taarifa yake kamanda yule wa polisi, mweusi na mkakamavu mwenye macho makali na sauti nzito.


taarifa ile ya kamanda wa polisi ilizua gumzo katika mitandao ya kijamii huku kila mtu akifatilia picha mjongeo zilizokuwa zikiwaonesha wahalifu wale waliotajwa wakiwa katika ulinzi mkali ikiwa ni pamoja na miongponi mwao kufikishwa mahakamani siku hiyo kujibu tuhuma mbali mbali zinazowakabili.


MWANZA


IGOMA STREET


"oyaaa sista weka kama jana ila maharage usiweke kabisa, zingatia ujazo wa nyama na mchuzi uwiane" aliongea kijana mmoja aliyekuwa amechafuka mavazi yake kwa oili na grisi kiasi cha kumfanya ajulikane kiwepesi kama fundi gereji.


"hizo nyama kuwiana na mchuzi buchani wanalitambua hilo, nyama ni mbili hutaki katafte watakaokuwekea utakavyo" alijibu mdada yule aliyekuwa ndani ya vazi la ushungi na dera na punde akaingia kijana mwingine mwenye mwili wa kawaida na kisha kuagiza ugali kwa dagaa wa kukaangwa, baada ya mtu wa kwanza kumaliza kula, kulipia nakutoweka mghahawani pale mwanamke yule alijisogeza mezani pale huku akiwa na shauku ya kujua kimemleta nini kijana yule ambaye dhahiri shairi ilionesha wanajuana


"Bosco umefata nini huku" alianza mwanamke yule kwa udadisi


"nimetumwa na mkuu kukuuliza umefikia wapi kwenye ule mpango" alikoroma mtu yule huku akiendelea kusukumia matonge ya ugali mdomoni


"bosco nisiwe muongo hii nchi kwasasa wame activate usalama masaa ishirini na nne, hatua pekee niliyopiga ni ya ukusanyaji wa habari ambayo imepelekea hatua ya utekelezaji kusuasu.......alikatishwa kwa ishara na kijana yule.


"ule mpango umeshahairishwa kwasasa, mpango utakaouona kwenye emaili yako ndiyo wenyewe na unatakiwa kukamilika ndami ya siku tatu mbele, nadhani tumeelewana tutaonana Goma nkutakie kazi njema." aliunguruma tena kijana yule


"sawa nitatekeleza kwa weledi mtoe wasiwasi mkuu" aliongea mwanamke yule kwa sauti ya polepole ambayo hata ukiwa mita mbili huwezi kusikia kunachozungumzwa ila si masikio ya kachero mbobevu Leyla Shigembe kutoka idara ya ujasusi ya jeshi aliyekuwa akijifanya ni mhudumu katika hoteli hiyo natangu mwanzo wa mazungumzo alijifanya yuko bize kuosha vyombo jikoni, vifaa alivyovitega kwa siri vilinasa mazungumzo yale ambayo yalitumwa kwenye ofisi fulani ya siri ndani ya makao makuu ya jeshi.


"watch every steps you hit Diane, mkuu anakusubiri kwa hamu kubwa wewe na kazi yako" alimaliza kusema kijana yule na kupotea eneo hilo kama upepo kuondoka kwake kukamfanya mwanamke huyu kufunga mghahawa wake mapema huku akimdanganya mhudumu yule kuwa amepata taarifa mbaya kuwa dada yake amepata ajari na amekimbizwa hospitali ya mkoa.


"sawa dada uranijulisha kunavokwenda" rafudhi ya kisukuma ilimtoka kachero yule


"mxiuew kama mwema vile kumbe jasusi mkubwa, alinichukulia mimi boya basi wakubwa zake wataitoa taarifa za msiba wako na utabaki na siri yako kaburini mbwa mweusi wewe" alijisemea kimoyomoyo Diane huku akimalizia kufunga virago vyake kabla ya kupotea eneo lile.


MSASANI-DAR ES SALAAM


Saa 12:45 jioni


ndani ya jumba moja kifahari na lenye mandhari mazuri, ghorofa moja ilitosha kuifanya iwe moja ya nyumba kali ndani ya mtaa ule, ndani ya jumba hili kulikuwa na kikao kizito kilichowahusisha wanandoa wawili, vijana wa makamo waliokuwa na miaka takribani miwili tangu wafurahie fungate lao, hawa hawakuwa wengine bali ni Kanali Charz na mkurugenzi msaidizi wa idara ya ulinzi wa raisi ndani ya idara ya ujasusi katika taifa hili.


"nataka uniambie kila kitu na usinifiche hata nukta kama unapenda nyumba hii iendelee kuwa na amani Charz" aliongea kwa utulivu na kumuangalia mmewe aliyekuwa amekalia sofa la mtu mmojja huku akionekana dakika kadhaa nyuma alikuwa amezama katika dimbwi la mawazo, kabla hajamaliza kuchakata sentensi ile alipigwa swali jingine lililomsisimua sana


"tangu umesoma kikaratasi kule kisiwani hujawahi kuwa kanali Charz niliyekuwa namuona kila uchwao kwa miezi kadhaa na hali hiyo imejitokeza baada ya kupapasa koti lako, kikaratasi kile hujataka kunishirikisha ujumbe uliomo ndani ulikuwa unahusu nini?mbali ya kuwa mimi na wewe ni mwili mmoja kiimani ila mwenzangu ukute hujamalizana kidemu chako, tusikilizane kama unaona kwamba kukaa kimya mi suluhisho ni heri tukaachana tu kila mtu akae na siri zake nimechoka mimi." alimaliza na sauti iliyoambatana na kama sauti ya kilio.


"natambua yote unayozungumza ni haki yako na uko sahihi.naomba nikwambie hili suala limetokea wakati na muda ambao mimi na wewe hatujawa kama sasa,sitaki jambo hili liwaingize kwenye picha watu wasiohusika na..........."Itaendelea.
 
Ilipoishia toleo lililopita
"tangu umesoma kikaratasi kule kisiwani hujawahi kuwa kanali Charz niliyekuwa namuona kila uchwao kwa miezi kadhaa na hali hiyo imejitokeza baada ya kupapasa koti lako, kikaratasi kile hujataka kunishirikisha ujumbe uliomo ndani ulikuwa unahusu nini?mbali ya kuwa mimi na wewe ni mwili mmoja kiimani ila mwenzangu ukute hujamalizana kidemu chako, tusikilizane kama unaona kwamba kukaa kimya mi suluhisho ni heri tukaachana tu kila mtu akae na siri zake nimechoka mimi." alimaliza na sauti iliyoambatana na kama sauti ya kilio.
"natambua yote unayozungumza ni haki yako na uko sahihi.naomba nikwambie hili suala limetokea wakati na muda ambao mimi na wewe hatujawa kama sasa,sitaki jambo hili liwaingize kwenye picha watu wasiohusika na..........." alikatishwa sentensi hiyo

Read my lips……
"naona ushakuwa mwanasiasa siku hizi na mimi unaelewa sifagiliagi kabisa mauongo, ni hivi kesho nitakuachia nyumba yako uyamalize matatizo yako na sihitaji unisemeshe nkutakie jioni njema natoka naenda ikulu nina kikao na mheshimiwa saa 2 usiku" aliongea hivyo Chiku huku akisimama tayari kwa kuzipiga hatua, hatua ya kwanza ilipita salama, hatua ya pili iliambatana na mwanamke yule kuvutwa na kisha kutua katika kifua cha mwanaume yule kisha akanong'onezwa masikioni mwake na sauti nzito
"Nelson Matambula yupo hai na isitoshe wamesema hili halijaisha hiyo ina maana kwamba kazi tuliyoifanya haikuwa na tija" aliongea kwa utulivu kanali Charz
"Nelly huyu huyu aliyekuwa ADC wa raisi mstaafu kabla ya kupangiwa majukumu mengine" aliongea mwanamke yule aliyekuwa anataka ufafanuzi wa hoja hiyo iliyoibuka.
"huyo huyo ndiyo alikuwa malaika wetu wa kifo nchini Congo na ndiye aliyebeba yale madini kutoka mkononi mwa kiongozi wetu brigedia Farijika Lufwefwe, hii inamaanisha katika kikosi chao ni yeye ndiyo aliyebakia kwani wenzake wote waliuawa na habari hiyo imebaki kuwa classfied ni sisi wachache tu tuliokuwa na vyanzo sahihi hapo hapo nyumba nyeupe ndiyo tunajua hata chief kuna mambo amefichwa." aliongea na kumeza funda kubw la mate mdomoni mwake na kisha kuendelea
"kama watu hawa wameshajua nipo kazini ina maana wanajua nitatoboa siri na hiko ndiyo chanzo cha maisha yangu kuwindwa kama swala porin, mwanzo nilikuwa nimejichimbia zangu vijijjini huko ni heshima ya yule mzee tu ndiyo iliyonirudisha hibyo kuna kazi iliyo mbele yetu ambayo kila hatua ni namba hivyo inabidi mahesabu yazingatie kanuni zake tukikosea tu tumepotea ndiyo maana sijataka kugharimu maisha ya watu wengine mke wangu" aliongea kwa hisia kali sana kanali Charz
"oooops......ntakuwa nawe bega kwa bega kuhakikisha maisha yrtu hayaingiliwi na matukio ya dizaini hiyo" alisema hivyo huku akimshika mkono huku akimtazama usoni mmewe, aliyeishia kutingisha tu kichwa kisha akambeba mkewe kuzifuata ngazi za kuelekea chumbani kwao.
KIGAMBONI-DAR ES SALAAM
Saa 20:15 usiku
moja ya fukwe hizi, ilipata ugeni wa watu wanne, wenye miili mikubwa na ya kutisha iliowafanya waonekane wamepata miili hiyo kwa kuzingatia ratiba nzuri ya mazoezi, mbali na rangi nyeusi ya ngozi bado haikutosha kusema walikuwa watanzania, watu hawa wanne waliokuwa katika nguo za kuogelea walikuwa wageni katika nchi hii na walikuwa katika kikazi.
"target yetu iko wapi" ilikuwa ni sauti iliyosikika kwa chini huku mvumo wa upepo wa bahari ukienda sanjari na mvurugano wa mawimbi bahari, rafudhi yake ilimtambulisha taifa analotokea alikuwa mkenya
"hey tiger wachana na papara maadamu tushafika tutajua tukifika site" alinong'ona jamaa mwingine aliyepanda hewani huku kichwa chake cheusi tii hakikuwa na unywele zaidi ya ndevu nyingi alizofuga mithili ya wayahudi kama sio maustadhi.
"twendeni pande hii wazeiya" aliongea huku akitoa ishara ilioishiria wapite upande huo, kwa idadi hiyo ya watu wanne sasa walikuwa wakiutafuta uelekeo wa kurudi posta huku mwendo ukiwa wa taratibu, mbali na pilika pilika za watu katika mitaa ile ya kigamboni na hasa katika viunga vile ila tembea ya watu wale wanne kisha kugawanyika kama vile hawajuani kilizivuta hisia kali za kikachero kwa koplo Zakaria
"hii miili ya kazi.......leo mjini kuna kazi ila ngoja inyeshe nitaona panapovuja" lilikuwa ni wazo lililopita kichwani kwa askari huyu wa jeshi la wananchi kutoka kikosi cha wanamaji(Navy) aliamua ku deal na mmoja wao ili tu ajue nia na dhamira yao, alikuja kutahamaki watu wale walikuwa wakiufata uelekeo zilipopakwi daladala ziendazo mbagala na viunga vyake naye akaunga na kusimama jirani na mlango wa nyuma wa gari lile brandi ya TATA, gari liliendelea kuchanja mbuga mpaka inatimia saa nne usiku ndipo ilipotia breki katika kituo cha daladala mbagala rangi tatu, abiria wote waliteremka huku watu wale wanne wakiendelea na maigizo yao na miguu yao ilikoma katika baa ya CITY OF SIN, ni kweli jina lilisadifu yaliyo ndani ya bar hiyo kisha kikafuatiwa na kitendo cha jamaa yule mwenye jina la Tiger kupewa ufunguo wa gari na mhudumu wa kiume wa bar ile, kitendo kilichofanyika ndani ya sekunde zisizozidi kumi kiasi kwamba kilishindwa kuonekana kwa watu waliokuwa na hamsini zao isipokuwa mmoja tu koplo zaka aliyebana kwenye kona huku kitendo kile kikimsisimua kuwa sasa mji unaenda kupata kazi, alijipa utulivu pale huku akijifanya kana kwamba pombe imemkolea huku akitembea kwa kuyumba yumba kiasi cha kukaribia meza iliyokaliwa na jamaa mweupe kiasi mwenye nywele ndefu na mwili uliojaa kwa mazoezi makali, hatua ya kwanza ilipita salama, hatua ya pili iliambata na tukio la mhudumu wa bar ile akipigwa kikumbo na kumfanya apepesuke na kudondosha trey aliyokuwa amebeba na kupelekea chupa ya pombe nayo kudondoka, chupa ile ilidakwa kwa ustadi mkubwa na kisha kuwekwa kwenye meza.
"wewe kaka msenge nini unatembeaje hivyo kama mwanamke na unabahati ingedondoka leo ndo ungejua kwanini kuku hakojoi" alipayuka kwa sauti mhudumu yule kitu kilichomfanya mtu yule ageuke kwa lengo kama kumshambulia mwanamke yule na hapo aliganda kwani alikuwa akitazamana na kikaratasi kilichodondoka chini huku kikiwa na maelezo machache 'MSASANI,BLOCK J PLOT NO. 457'
"Unasemaje wewe malaya nitakubamiz..........." alikatishwa kauli na mkono mgumu uliomkamata kwenye kola ya shati lake…….itaendelea
Nb: huu ni mwendelezo wa kitabu cha pili ambacho kimesharuka hapa hapa katika jukwaa hili
 
Ilipoishia toleo lililopita
wewe kaka msenge nini unatembeaje hivyo kama mwanamke na unabahati ingedondoka leo ndo ungejua kwanini kuku hakojoi" alipayuka kwa sauti mhudumu yule kitu kilichomfanya mtu yule ageuke kwa lengo kama kumshambulia mwanamke yule na hapo aliganda kwani alikuwa akitazamana na kikaratasi kilichodondoka chini huku kikiwa na maelezo machache 'MSASANI,BLOCK J PLOT NO. 457'
"Unasemaje wewe malaya nitakubamiz..........." alikatishwa kauli na mkono mgumu uliomkamata kwenye kola ya shati lake.
Chukua Pozi na fuatana nami neno kwa neno……..
"umenunua ugomvi siyo basi nitawapa ugomvi wote wawili kissha usiku huu nitaumaliza na nyinyi wake zangu haya nifuateni tusiwaharibie watu starehe yao" alimaliza kwa kurusha rusha mikono huku akimtazama mtu aliye mbele yake huku akiendelea kuigiza kana kwamba amezidiwa na wingi wa pombe.
"hey msee huna bibi ya kudozi nayo usiku mpaka ughasighasi bibi za wengine, ita uber ikimbize hiyo fuvu yako kwa pillow" alimuachia huku akijua ni pombe imemzidi mtu huyo bila kung'amua mwenzie yupo kazini na keshagundua uhalisia wa mtu yule hata udakaji wa chupa ile ya pombe na alihusudu uwezo wa watu hawa na kitu ambacho hakikujua ni uingiaji wao nchini kwani huyu mmoja rafudhi yake ilimtambulisha kuwa anatoka nchi jirani. akapotea eneo hilo na kuibukia kinondoni studio na simu yake ilipata uhai kisha kubofya namba kadhaa na kuiweka sikkioni huku akisikilizia utulivu wa eneo hilo na kwenye simu baada ya sekude kadhaa sauti nzito iliunguruma masikioni mwake.
"Dogo inakuwaje mbona usiku usiku kulikoni???" ilianzidha mazungumzo sauti ile
"kwema ama siyo kwema naweza kusema kiufupi mji umetembelewa na watalii inavyoonesha kuwa wanatafuta mnyama mmoja anaekaa banda zuri" aliongea Koplo Zakaria
"dogo unajua ni usiku sana alafu nimetoka kuzinguana na shemeji yako kunaa mambo kadhaa yananisumbua hebu nyoosha maelezo vizuri" aliongea Kanali Charz huku akionekana kuanza kuchoka
"kuna watalii wanatafutaa nyumba namba 457,blockJ, msasani na inavyoonesha ni kuwa hawana siku nyingi jijini na kwa ku......" alikatishwa
"hebu ngoja kwanza hao watalii wako wangapi na wanatoka nchi ipi?" aliuliza kwa sauti yachini na yenye msisitizo.
"wanatoka Kenya na wapo wanne ingawa huyu mmoja hajulikani ni wa wapi inaonesha ni watu wa kikosi maalumu na wako kumfuta mtu katika ardhi hii" aliongea koplo zakaria
"ngoja niifanyie kazi hii taarifa na asubuhi kesho tuonane 346 HALLkijua cha usoni" hakusubiei neno jingine simu ikakatwa.
ENTEBE-UGANDA
saa 01;45 usiku
"mwambie mbwa wa machakos awaambie kazi ya kumfuta yule kobra mweusi ananinyima usingizi nategemea taarifa nzuri nimkapo" kiswahili kilichonyooka kiliunguruma katika masikio ya mtu aliyekuwa simuni.
"limeisha hilo genera......." alikatishwa
"dont repeat that sentence again especially the last word" ilifoka sauti ile na kuikata simu
**********
Usiku huu ulisindikizwa na mvu iliyoanza muda mfupi katika usiku huu mnene. kanali Charz alikuwa njiani akirudi nyumbani kwake akitokea nyumbani kwa chifu kumueleza yaliyojiri na kuona ni jinsi gani hatua hizo kwani nyumba iliyokuwa katika mpango wa wageni wale ilikuwa ni nyumba anayoimiliki yeye mwenyewe na mkewe ambaye sasa ameteuliwa kuwa mkurugenzi msaidizi wa idara ya ujasusi, aliiona hatari iliyo mbele yake, kujulikana anapoishi ni kuiweka familia katika hatari kwani amekwisha piga simu kwenye namba ya mkewe inaita bila kupokelewa haliisivyo kawaida, wasiwasi ukamjaa huku akiongeza mwendo wa gari dakika kumi zilitosha kumfikisha mtaa anaokaa ambao ulimpokea kwa ukimya na hapo mwili ukamsisimka huku sasa akiirudisha akili kazini akaipita nyumba anayokaa huku macho yake yakiwa kazini katika kuzisoma nyendo za adui, hakumaliza hatuakumi mlio wa mpasuko wa kioo ulimstua kiasi cha kukanyaga mafuta mangi na ni kama malaika wema walimnusuru kwani kioo cha upande wa nyuma kilimwagika baada ya risasi kadhaa kukitawanya, mapambano hayakukoma kwani hata huko mbele mambo hayakuwa mazuri kwani alipokelewa na mvu ya risasi kutoka kwa mtu aliyejificha sehemu fulani.
"eeehhhh Mungu nisaidie akapiga gia nakuirudisha gari kwa nyuma na hapo kioo cha nyuma nacho kilisambaratika kwa risasi kadhaa alizidi kurudi nyuma kabla umeme wa mtaa ule kukatika na kisha kitu kama mlio wa upepo kutoka ikafuatia na hapo hapo akajitupa nje huku akihama hapa na pale na alipishana na gari la mauti, ndiyo kwani risasi zilichimba chini na zilikuwa zinakuja kama mvua.
"nikizembea kwenye giza hili jua la kesho litaamka likiwa na tangazo la msiba wangu, hawa watu wanausongo na mimi watanimaliza kama nisipofanya kitu" alijiwazia huku akijificha kwenye ukuta wa nyumba iliyo karibu na pale huku akipiga hesabu za kuwatoka watu wale huku ikionesha wamedhamiria kumtoa roho yake kikatili sana, giza lilikuwa zito huku mvua na radi za hapa na pale zikipiga akiwa amejibanza pale alipata kushuhudia jitu jeusi lenye koti ya rangi ya damu ya mzee

IKULU
MASAA MAWILI YALIYOPITA
katika ofisi iliyopambwa vizuri kimpangilio ikiwa namna ya kila kitu kilikuwa mahali pake, hewa nzuri na safi ilikuwa ikitamalaki katika ofisi hiyo ya mkuu wa nchi, ni nadra sana muda kama huu kuwakarimu wageni wa mmiliki wake kwani ilipumzika kwa muda wa miaka miwili na siku zake, leo mheshimiwa raisi Glory Steven mbele yake alikuwa anatizamana na watu wawili wazito kinyadhifa katika jicho la taifa watu hawa hawakuwa wengine bali ni mkurugenzi wa idara ya ujasusi pamoja na msaidizi wake, wakijadili ripoti ya uhalifu wa kiwango cha juu, cha utoroshwaji wa meno ya trmbo na faru kupitia biashara ya mazao ya nafaka kuelekea nchi jirani ya kenya.
"mheshimiwa raisi hii habari imetusisimua sana mara tu ilipotufikia na tukashauriana tukuone ili tuone namna gani ya kushughulika na hawa washenzi" aliongea Chifu huku akimtazama mheshimiwa raisi.
"msipige ngoma kwa shoka haitatoa mlio, hili mimi ninalifahamu mbona nilipata habari hiyo asubuhi ya leo na mpaka sasa hivi na muweke rekodi sawa macho na masikio yangu yako Kilimanjaro na nimeagiza hatua za haraka zianze kuchukuliwa ," aliongea kwa utulivu huku akiwatazama
"nikupongeze mheshimiwa raisi kwa kuwa hatua moja mbele yetu ila......."
"ghrrrrr ghrrrrr ghrrrrr...." mtetemo wa simu ya mkurugenzi msaidizi ulimfanya mzee huyo kukatisha alichokuwa anakieleza na kubaki wakimuangalia mkurugenzi msaidizi wa idara ya ujasusi.
"khooo..........ni baba Ian,huenda atakuwa amefika nyumbani kisha amenikosa ila tuendelee" alilainisha koo kwa kujikoholesha na kutoa maelezo hayo mafupi lakini atu wale waliendelea kumtazama
"ungepokea tu simu ukamsikiliza yawezekana ana shida ya kifamilia au binafsi......kwani Ian alishatoka kwa bibi yake?" aliuliza chifu huku akimtazama Chiku
"hapana hiki kikao ni muhimu nitampigia simu baada ya hapa kwa maana najua ameshaanza kupatwa na wivu si mnajua ndoa yenyewe bado changa, upweke wa kukaa pekeake kwasababu Ian kakatalia kwa bibi yake hataki kurudi" alimaliza kujibu kile kilichoulizwa na kisha kuinamisha kichwa chini kwa aibu za kike kike.
"ooops....ni hivi nusu saa iliyopita kabla hatujakutana hapa nilikuwa na Kanali Charz aliyenipa habari ya kuingia nchini kwa raia wa kigeni kutoka nchi jirani waliofika kwa kazi moja ya kuiwinda nyumba namba 457,block J iliyoko msasani"…………itaendelea je wavamizi watafanikiwa kuifikia nyumba namba 457 mkamiqji anajadiliwa na je atafanikiwa kutoka salama ungana nami toleo lijalo.
 
Back
Top Bottom