Saudia yanunua mfumo wa makombora kutoka Israel

kimsboy

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
8,992
17,892
Saudia yanunua mfumo wa makombora kutoka Israel
Saudi Arabia imeripotiwa kununua mfumo wa ngao ya makombora kutoka utawala wa Kizayuni wa Israel, katika hali ambayo ripoti zinasema tawala mbili hizo zipo mbioni kuweka wazi na kuimarisha uhusiano wao.
Duru za ngazi za juu za kidiplomasia zimeiambia tovuti ya habari ya Imarati ya Khaleejonline kwamba, utawala wa Aal-Saud umefanikiwa kununua mfumo huo wa ngao ya makombora kutoka Tel Aviv kutokana na upatanishi wa Marekani.
Awali utawala wa Kizayuni wa Israel ulikuwa umekataa kuuuzia utawala wa Riyadh mfumo huo wa makombora ukidai kuwa hauwezi kufunga mkataba wowote wa mauzo ya silaha na nchi za Kiarabu eti kwa kuwa huko ni kuhatarisha maslahi yake katika eneo.
Inaarifiwa kuwa, makubaliano hayo ya mauzo ya mfumo huo wa makombora wenye kugharimu makumi ya mamilioni ya dola yataanza kutekelezwa mwezi Disemba, baada ya Saudia kukamilisha malipo
Vyanzo vya habari vimedokeza kwamba, Saudia imenunua mfumo huo kwa shabaha ya kujikinga na makombora ya balestiki yanayovurumishwa kila uchao na wanaharakati wa Ansarullah wa Yemen.
Mwaka uliopita, gazeti moja la Kizayuni lilifichua kuwa, katika mkataba wa mabilioni ya dola wa ununuzi silaha baina ya Marekani na Saudia, baadhi ya mashirika ya uundaji silaha ya Israel yalianishwa kuwa yangestafidi na makubaliano hayo.
4bpt4bc3876c2a19715_800C450.jpg
 
Saudia yanunua mfumo wa makombora kutoka Israel
Saudi Arabia imeripotiwa kununua mfumo wa ngao ya makombora kutoka utawala wa Kizayuni wa Israel, katika hali ambayo ripoti zinasema tawala mbili hizo zipo mbioni kuweka wazi na kuimarisha uhusiano wao.
Duru za ngazi za juu za kidiplomasia zimeiambia tovuti ya habari ya Imarati ya Khaleejonline kwamba, utawala wa Aal-Saud umefanikiwa kununua mfumo huo wa ngao ya makombora kutoka Tel Aviv kutokana na upatanishi wa Marekani.
Awali utawala wa Kizayuni wa Israel ulikuwa umekataa kuuuzia utawala wa Riyadh mfumo huo wa makombora ukidai kuwa hauwezi kufunga mkataba wowote wa mauzo ya silaha na nchi za Kiarabu eti kwa kuwa huko ni kuhatarisha maslahi yake katika eneo.
Inaarifiwa kuwa, makubaliano hayo ya mauzo ya mfumo huo wa makombora wenye kugharimu makumi ya mamilioni ya dola yataanza kutekelezwa mwezi Disemba, baada ya Saudia kukamilisha malipo
Vyanzo vya habari vimedokeza kwamba, Saudia imenunua mfumo huo kwa shabaha ya kujikinga na makombora ya balestiki yanayovurumishwa kila uchao na wanaharakati wa Ansarullah wa Yemen.
Mwaka uliopita, gazeti moja la Kizayuni lilifichua kuwa, katika mkataba wa mabilioni ya dola wa ununuzi silaha baina ya Marekani na Saudia, baadhi ya mashirika ya uundaji silaha ya Israel yalianishwa kuwa yangestafidi na makubaliano hayo.View attachment 865647
Utawala Wa taifa teule la Israeli safi saana
 
Nawakubali sana Hawa waasi Wa Yemen waliochoka kuonewa na saudia
Nalog off
Sio kwamba wamechoka kuonewa na saudia,hao waasi wanapewa makombora na USA.Kichapo kilivyozidi ndo wanakupa ushauri ununue mitambo ya kujikinga,then mshauri anakuchomekea kununua kwa ndugu yake(Israel) mwisho wa siku mshindi ni Trump bingwa wa the art of the deal.We ujiulizi kwa nini vita za afgan,Yemen,Libya aziishi.penye vita ndo penye utajiri
 
USA hanaga urafiki wa kudumu hata kidogo,mkipigana wote anawapa siraha kulingana na uwezo wenu.Atakayeshinda vita ndiye atakayekuwa rafiki yake.CIA kwa sasa haiwezi kukubali vita ya Yemen iishe cze wana pukutisha fedha za Saudis na washirika wake kwa kuwauzia weapons.Somo ninalojifunza ni kuwa utajiri haitafutwi kwa njia ya lelemama.
 
Sio kwamba wamechoka kuonewa na saudia,hao waasi wanapewa makombora na USA.Kichapo kilivyozidi ndo wanakupa ushauri ununue mitambo ya kujikinga,then mshauri anakuchomekea kununua kwa ndugu yake(Israel) mwisho wa siku mshindi ni Trump bingwa wa the art of the deal.We ujiulizi kwa nini vita za afgan,Yemen,Libya aziishi.penye vita ndo penye utajiri
Kumbe kuna Washawasha mpaka kwenye vita! Ahsante sana kwa kunifungua macho.
Nalog off
 
Hujui kinacho endelea katika mataifa haya mawili.

Tatizo mmeviachia vyombo vya habari ndio viwe vyanzo vyenu vya habari. Hapa ndipo mlipopuyanga na mtaendelea kupayanga.
Tupe uyajuayo kuhusu haya mataifa mawili ili nasi tuufahamu
Nalog off
 
familia ya kifalme ya Saudia ni Waisrael kwa asili hivyo hao ni ndugu zao kiasili ila sio kiimani ndio maana hata Israel ikiipiga vp Palestine hutosikia Saudia inalaani tukio hilo.
 
Back
Top Bottom