Sasa yatosha kuendelea na mijadala hii

Sasa yatosha kuendelea na mijadala hii

Yakini

Member
Joined
Nov 20, 2012
Posts
75
Reaction score
19
Tunajua kila mtu anauhuru wa maoni, na ndivyo ilivyo katika jambo lililotokea ndani ya chadema. Ni wito wangu kwa wadau wote kuendeleza mijadala inayobeba mashiko ya nchi yetu kwa sasa. Nchi yetu inaelekea katika wakati muhimu sana katika kukamilisha mchakato wa Kutengeneza katiba mpya, tunahitaji kujikita katika hilo pamoja na mambo mengine yenye maslahi kwa umma. Nchi yetu ipo katika hali tete ukizingatia rasilimali za nchi yetu zinatumika vibaya na watanzania wanakumbwa na wingu kubwa la umaskini. Sioni kama ni busara kuendeleza mijadala hii na kusahau mambo muhimu yanayoendelea nchini mwetu.
 
mkuu usituhamishe kweny hoja!na hata hili suala la mbowe kutafuna ruzuku za chama ni suala la maslahi ya nchi,kwahyo tutaendelea kulijadili mpaka tujue mwisho wake
 
mkuu usituhamishe kweny hoja!na hata hili suala la mbowe kutafuna ruzuku za chama ni suala la maslahi ya nchi,kwahyo tutaendelea kulijadili mpaka tujue mwisho wake

Tuhuma hizi unaleta .Ma CCM wenzako hawathubutu kutamka haya wewe unasema katafuna Ruzuku .Mbowe na ruzuku kweli ?
 
Back
Top Bottom