Sasa Wanawake na Wanaume Tasa ni Dili

Sasa Wanawake na Wanaume Tasa ni Dili

JF2050

JF-Expert Member
Joined
Sep 25, 2010
Posts
2,085
Reaction score
45
Hii ni hoja iliyoibuliwa na baadhi ya vijana niliokutana nao tena kwa mara nyingine jana jioni hapa mtaani.

Kutokana na uhalisia kwamba wanaume na wanawake wengi wenye umri kuanzia miaka 30 na kuendelea wamekwisha kuzaa watoto kabla ya ndoa, katika mahojiano na vijana kadhaa hapa mtaani jana jioni, wengi ambao hiyo hali imewakumba, wameonyesha nia ya kuoa wanawake tasa au kuolewa na wanaume tasa.

Wamedai kufanya hivyo itasaidia sana kupunguza mikwaruzano na ugomvi katika familia, kwani mama au baba tasa atawaheshimu na kuwathamini watoto hao, kwa sababu watakuwa ndio watoto pekee katika familia. Pia wazazi wengine waliozaa na wale waliooana watapata imani kwamba watoto wao wanalelewa na kutunzwa vema, kutokana na kutokuwepo kwa uhasama na uadui dhidi ya watoto hao ambao ungeweza kusababishwa na watoto watakaozaliwa baada ya ndoa.

Mnalionaje hili wadau?

Jamani someni vizuri basi muelewe nilichoandika - ina maana nyie katika mazoezi, majaribia na mitihani swali la "comprehension" shule ya msingi mlikuwa hamfanyi au hilo swali lilikuwa optional?
 
Tasa then amezaa before? Au sijaelewa mie nirudi kusoma tena uzi?
 
Tasa then amezaa before? Au sijaelewa mie nirudi kusoma tena uzi?

Labda urudie kusoma. Nimemaanisha hivi, mfano, wewe umezaa na mwanaume watoto 2 ila hamna mpango wa kuoana naye, badala yake ukaenda kuoana na mwanaume mwingine tasa halafu mkalea hao watoto.
 
Tasa then amezaa before? Au sijaelewa mie nirudi kusoma tena uzi?
Yaani mhusika mwenyewe awe mzima ila atakaye muoa/atakayeolewa nae awe tasa!!ila walee mtoto huyo alozaa mhusika huo si ubinafsi kha
 
Tasa tena kazaa duuh majanga

Labda urudie kusoma. Nimemaanisha hivi, mfano, wewe umezaa na mwanamke/wanawake watoto 4, ila huna mpango wa kuwaoa, badala yake ukaenda kuoa mwanamke mwingine ambaye ni tasa halafu mkalea hao watoto.
 
Yaani mhusika mwenyewe awe mzima ila atakaye muoa/atakayeolewa nae awe tasa!!ila walee mtoto huyo alozaa mhusika huo si ubinafsi kha

Yeah, mmoja tasa mwingine ameshazaa na mwingine. Ubinafsi uko wapi? Si wametoa sababu?
 
Labda urudie kusoma. Nimemaanisha hivi, mfano, wewe umezaa na mwanaume watoto 2 ila hamna mpango wa kuoana naye, badala yake ukaenda kuoana na mwanaume mwingine tasa halafu mkalea hao watoto.

Apo sasa nimeelewa nakushkuru
 
Yaani mhusika mwenyewe awe mzima ila atakaye muoa/atakayeolewa nae awe tasa!!ila walee mtoto huyo alozaa mhusika huo si ubinafsi kha

Ok ahsante bi shosti kwa ufafanuzi hujambo lakin?
 
Yeah, mmoja tasa mwingine ameshazaa na mwingine. Ubinafsi uko wapi? Si wametoa sababu?
inamaana huyo alokuwa na mtoto atatafuta mtu tasa kwa maslahi yake binafsi sio!!Wewe unaona sio ubinafsi huo?Au unamaanisha hivo ili hao matasa wasiwe wapweke na wasinyanyaswe!!
 
inamaana huyo alokuwa na mtoto atatafuta mtu tasa kwa maslahi yake binafsi sio!!Wewe unaona sio ubinafsi huo?Au unamaanisha hivo ili hao matasa wasiwe wapweke na wasinyanyaswe!!

Mbona kuna faida zaidi: tasa hawi mpweke, watoto watalelewa bila masimango, mwoaji/aliyeolewa anakuwa amepata mtu anayempenda. Sidhani ati kwa sababu mtu ni tasa hawezi kupenda au kupendwa.
 
Mbona kuna faida zaidi: tasa hawi mpweke, watoto watalelewa bila masimango, mwoaji/aliyeolewa anakuwa amepata mtu anayempenda. Sidhani ati kwa sababu mtu ni tasa hawezi kupenda au kupendwa.
Sawa nimekuelewa rafiki!Ni wazo zuri!!The problem will be accomplishing the whole ideology!!
 
Back
Top Bottom