Sasa tunakaribia patamu

Sasa tunakaribia patamu

1. Bodaboda wafunga barabara Mbeya.

2.Jaji agoma kujitoa - kesi ya CUF.

3.Max anyimwa dhamana.

4.Lema anyimwa dhamana.

5.Ben Saanane haonekani.

6.Maiti zakutwa ndani ya mifuko.

7.Rais afumua sisiemu.

8.Bei ya sembe yapaa.

Mungu ibariki Tanzania manake tunakoelekea tunaambiwa ni kuzuri zaidi.
Ni miezi michache tuu bodaboda kajiingiza babaran bila tahadhari pale mataa ya TAZARA, huku gari zikiwa zimeruhusiwa... Alipondwa na wala hakutambulika. Sekunde chache baboda wakafunga Babara. Ss kwa issue km hii tosha kujua akili za bodaboda.
 
Mengine yote sawa ila sembe hapana, acha wakulima tufaidike kuuza mazao kwa bei inayoendana na jasho letu.
 
Max atatoka kweli huko aliko naona kama mnapepea moto
 
Simtetei magufuli wala hanijui na sitegemei anijue yeye kama binadamu anamadhaifu yake ila kama rais hapana tusimuonee anafanya mazuri mengi anachemka machache ngoja nchi ikae vizuri kuna watu watu waliifanya tz Mali yao binafsi kwasasa wote sawa anayekula anakula kihalali kwa jasho lake yapo ya kumlaumu kakini mengine hapana kabisa tunamuonea
Ushakula michembe umeshiba kinachobaki ni kuropoka eti halali? Halali ipi?
Nyingeza ya mshahara halali hatuioni.
 
11. bei ya sembe yapaaa
Inanikumbusha mwaka jana ilipopanda bei ya mchele. Serikali ikawa lawamani. Ilipoagiza mchele toka nje kufidia upungufu, ikawa lawamani tena michele ya wazawa inaozea maghalani!! Kuwaelewa watanzania ni ngumu. Ni vyema kutosikiliza kelele, kwani kadri unavyoelekea sehemu sahihi huwa zinazidi ili ugeuke na kuwa jiwe ( hadithi ya Baba wa Taifa. JK Nyerere).
 
Back
Top Bottom