sasa tufundishane kupika.......

pauline

JF-Expert Member
Dec 26, 2010
650
140
hii ni mojawapo ya sectors za malavi davi inakyokuwa overlooked ila aparently inasababisha matatizo... sasa wenye uzoefu tupeane maujuzi humu,tusije tukaachika bure lol... tufundishane namna nyengine za kupika nyama, wali, mboga za majani na vile vyakula vya asili... kujua aina moja tu ya upishi inachosha tufundishane varieties jamani

NB: Na wale wengine wenye recipe rahisi rahisi na fupi mnaweza kuongezea hata wakaka wanaoishi kibachela napo wapate maujuzi, mie mpaka leo sijui kupika wali wa nazi ingawa kila siku najitahidi kujaribu lol, nawish by the time naolewa niwe nimejuwa lol.



nimeona hii picha facebook, nikawa mpole mie sijui kama nitaweza kuja siku moja kutandaza meza namna hii........
196267_1485452194639_1783941010_893784_7589132_n.jpg


najua siko peke yangu wadada tuzungumze kikike mambo yasiharibike:becky::becky::mwaaah:...naombeni kwa kuanzia mnaojua zile sambusa ile nyama ya ndani ya kusaga wanatia viungo gani/wanapikaje?.

Karibuni.
 
Hehehehe leo tu nimetoka kuombwa na mkaka mmoja nimfundishe kupika.Tungewekewa jukwaa mi kila siku ningeweka picha na recipe zangu...napenda kucheza na viuongompaka basi wee!Nwy ngoja nipige picha nianze nlivyopika leo...
 
jamani mnawekaje picha inakuwa kubwa?? mie nikiweka inatokea kadooogo???:confused2::confused2:
 
Hehehehe leo tu nimetoka kuombwa na mkaka mmoja nimfundishe kupika.Tungewekewa jukwaa mi kila siku ningeweka picha na recipe zangu...napenda kucheza na viuongompaka basi wee!Nwy ngoja nipige picha nianze nlivyopika leo...

thanks lizzy we are waiting....:mwaaah:
 
IMG382.jpg

Owkey so leo nimepika Chicken curry ndizi nyama na wali mweupe tu wa kawaida.

Chicken masala...
Kiasi cha vitu itabidi nikisie maana mi hua sipimi natumia tu uzoefu.
Kuku 1/2 kg
Beans kikombe kimoja
Mafuta vijiko 3 vya chakula
Tui la nazi kikombe kimoja
Nyanya nzima moja au ya kopo nusu kikombe
Curry vijiko 4 vya chakula
Chicken masala vijiko 3 vya chakula
Carrot moja na kitunguu na vipande viwili vya vitunguu swaumu.

Kwanza chemsha kuku na beans mbali mbali lakini..usisahau chumvi kiasi upendacho.Vikishaiva vichuje umwage maji ya beans ila mchuzi wa kuku uache.Kaanga vitunguu kabla hata havijawa brown weka karoti ulizozikata kwa umbo lolote upendalo.Karoti zikianza kulainika weka kuku wako navitungu swaumu hapo hapo.Binafsi hua sivikaangia na vitunguu ililadha yake isiishe kwenye kukaangwa.Nwy kaanga mpaka kuku nayo ianze kua brown kwa mbali...then tia beans na baada ya dakika mbili weka viuongo vyako vyote.Hapa kama ni mpenzi wa pilipili ndo muda muafaka kuweka. Acha viuonge vikolee mpaka uone vitu vinaanza kung'ang'ania kwenye sufuria weka nyanya zako na uruhusu ziive kidogo kabla ya kuweka ile supu kidogo iliyobaki.Funika kisha uache ichemke kwa dakika tano kabla ya kuweka tui lako la nazi.Koroga mpaka ianze kuchemka tena ili tui lisikatika...onja chumvi...funika kisha punguza moto.Baada ya dakika kama nane itakua tayari.



IMG387.jpg

Ndizi nyama.
Mahitaji

Ndizi nne au tano.
Viazi vikubwa 8-10
Nyama ya ng'ombe 1/2 kg
Kipande cha tangawizi + kipande cha limao
Nyanya moja + hoho + karoti 1
Kitunguu
Royco kijiko 11/2 cha chakula
Tui la nazi 11/2 kikombe cha chai
Vitunguu shaumu vipande vitatu
Mafuta kiasi

Kata nyama..kamulia kipande kimoja cha limao..kwangulia kipande cha tangawizi na vitunguu swaumu...weka maji kikombe kimoja na nusu+ chumvi kisha chemsha mpaka ilainike.

Wakati nyama inachemka menya ndizi na viazi vyako kisha vioshe.Chuku nusu ya ndizi na viazi vyako uweke kwenye sufuria unayotaka kupikia. Then katakata nyanya..hoho..vitunguu na karoti zako uweke kwenye mchanganyiko wako uliotanguliza kwenye sufuria.Baada ya hapo chukua ile nyama pamoja na mchuzi umimine juu ya mchanganyiko wako. Weka chumvi na ongeza maji kidogo kisha weka viazi na ndizi zilizobaki.Funika na uweke jikoni. Acha vichemke mpaka vilainike kisha weka royco yako na mafuta. Acha vichemke kwa dakika chache kabla ya kuweka tui lako la nazi.Usisahau kukoroga mpaka ndizi zako zianze kuchemka tena. Punguza moto.... funika na uache kwa dakika kumi kabla ya kuipua.

Kilichobaki sasa ni kupakua na kufurahia tu....usisahau kushushia na maji.Ukiwa na parachichi ndizi zako zitanoga zaidi!!
 
hii ni mojawapo ya sectors za malavi davi inakyokuwa overlooked ila aparently inasababisha matatizo.....sasa wenye uzoefu tupeane maujuzi humu,tusije tukaachika bure lol.....tufundishane namna nyengine za kupika nyama,wali,mboga za majani na vile vyakula vya asili.....kujua aina moja tu ya upishi inachosha tufundishane varieties jamani..................
NB.....na wale wengine wenye recipe rahisi rahisi na fupi mnaweza kuongezea hata wakaka wanaoishi kibachela napo wapate maujuzi........mie mpaka leo sijui kupika wali wa nazi ingawa kila siku najitahidi kujaribu lol....nawish by the time naolewa niwe nimejuwa lol................
nimeona hii picha facebook,nikawa mpole mie sjui kama nitaweza kuja siku moja kutandaza meza namna hii........View attachment 31517

najua siko peke yangu wadada tuzungumze kikike mambo yasiharibike:becky::becky::mwaaah:...naombeni kwa kuanzia mnaojua zile sambusa ile nyama ya ndani ya kusaga wanatia viungo gani/wanapikaje?..........karibuni.

Pauline:
Whoever made this, hongera zake maana its very impressive! Ila mimi personally my biggest problem is quantity, yaani I can make a kick a** meal for 4 people or less, lakini usually fail miserably when chakula kikiwa cha wengi. Taste inakuwaga "mbofu mbofu". Sijui ndio uchoyo au.......:smiling:
Anyways wacha nisubiri wenye maujuzi yao wakija, so I can learn.
 
Lizzy:
The chicken does look delicious. THanks for the recipe, Ill try it soon enough nikiwa na wageni.
 
Pauline:
Whoever made this, hongera zake maana its very impressive! Ila mimi personally my biggest problem is quantity, yaani I can make a kick a** meal for 4 people or less, lakini usually fail miserably when chakula kikiwa cha wengi. Taste inakuwaga "mbofu mbofu". Sijui ndio uchoyo au.......:smiling:
Anyways wacha nisubiri wenye maujuzi yao wakija, so I can learn.

uko kama mimi Nemo.....especially ugali nitajitahidi kama ni wa mtu mmoja au wawili zaidi ya hapo ni madudu tu...:becky::glasses-nerdy:
 
View attachment 31521
Owkey so leo nimepika Chicken curry ndizi nyama na wali mweupe tu wa kawaida.

Chicken masala...
Kiasi cha vitu itabidi nikisie maana mi hua sipimi natumia tu uzoefu.
Kuku 1/2 kg
Beans kikombe kimoja
Mafuta vijiko 3 vya chakula
Tui la nazi kikombe kimoja
Nyanya nzima moja au ya kopo nusu kikombe
Curry vijiko 4 vya chakula
Chicken masala vijiko 3 vya chakula
Carrot moja na kitunguu na vipande viwili vya vitunguu swaumu.

Kwanza chemsha kuku na beans mbali mbali lakini..usisahau chumvi kiasi upendacho.Vikishaiva vichuje umwage maji ya beans ila mchuzi wa kuku uache.Kaanga vitunguu kabla hata havijawa brown weka karoti ulizozikata kwa umbo lolote upendalo.Karoti zikianza kulainika weka kuku wako navitungu swaumu hapo hapo.Binafsi hua sivikaangia na vitunguu ililadha yake isiishe kwenye kukaangwa.Nwy kaanga mpaka kuku nayo ianze kua brown kwa mbali...then tia beans na baada ya dakika mbili weka viuongo vyako vyote.Hapa kama ni mpenzi wa pilipili ndo muda muafaka kuweka. Acha viuonge vikolee mpaka uone vitu vinaanza kung'ang'ania kwenye sufuria weka nyanya zako na uruhusu ziive kidogo kabla ya kuweka ile supu kidogo iliyobaki.Funika kisha uache ichemke kwa dakika tano kabla ya kuweka tui lako la nazi.Koroga mpaka ianze kuchemka tena ili tui lisikatika...onja chumvi...funika kisha punguza moto.Baada ya dakika kama nane itakua tayari.



View attachment 31522
Ndizi nyama.
Mahitaji

Ndizi nne au tano.
Viazi vikubwa 8-10
Nyama ya ng'ombe 1/2 kg
Kipande cha tangawizi + kipande cha limao
Nyanya moja + hoho + karoti 1
Kitunguu
Royco kijiko 11/2 cha chakula
Tui la nazi 11/2 kikombe cha chai
Vitunguu shaumu vipande vitatu
Mafuta kiasi

Kata nyama..kamulia kipande kimoja cha limao..kwangulia kipande cha tangawizi na vitunguu swaumu...weka maji kikombe kimoja na nusu+ chumvi kisha chemsha mpaka ilainike.

Wakati nyama inachemka menya ndizi na viazi vyako kisha vioshe.Chuku nusu ya ndizi na viazi vyako uweke kwenye sufuria unayotaka kupikia.Then katakata nyanya..hoho..vitunguu na karoti zako uweke kwenye mchanganyiko wako uliotanguliza kwenye sufuria.Baada ya hapo chukua ile nyama pamoja na mchuzi umimine juu ya mchanganyiko wako.Weka chumvi na ongeza maji kidogo kisha weka viazi na ndizi zilizobaki.Funika na uweke jikoni.Acha vichemke mpaka vilainike kisha weka royco yako na mafuta.Acha vichemke kwa dakika chache kabla ya kuweka tui lako la nazi.Usisahau kukoroga mpaka ndizi zako zianze kuchemka tena.Punguza moto...funika na uache kwa dakika kumi kabla ya kuipua.

Kilichobaki sasa ni kupakua na kufurahia tu....usisahau kushushia na maji.Ukiwa na parachichi ndizi zako zitanoga zaidi!!

Thanks lizzy....nitajaribu hio kuku kesho....
 
...kwa jinsi ninavypenda chapati,...sijui itakuwaje tu mamsapu akinambia hajui kuzipika.
 
Daaah
Hii fani mara zote ni mgumu kuielewa ila napenda kula
 
...kwa jinsi ninavypenda chapati,...sijui itakuwaje tu mamsapu akinambia hajui kuzipika.

I opened my teeth now
:becky::becky::becky:

Mkuu chapati haina kazi sana, labda chapati za kuwekea makorombwezo mpaka zionekane kama mayai ya Spanish
 
  • Thanks
Reactions: Mbu

nimeona hii picha facebook,nikawa mpole mie sjui kama nitaweza kuja siku moja kutandaza meza namna hii........View attachment 31517

najua siko peke yangu wadada tuzungumze kikike mambo yasiharibike:becky::becky::mwaaah:...naombeni kwa kuanzia mnaojua zile sambusa ile nyama ya ndani ya kusaga wanatia viungo gani/wanapikaje?..........karibuni.

...zaidi ya zile chapati pale, hakuna chochote hapo ninachoweza msifia mpishi huyu ufundi wa kupika 'mahanjumati'
 
hii ni mojawapo ya sectors za malavi davi inakyokuwa overlooked ila aparently inasababisha matatizo.....sasa wenye uzoefu tupeane maujuzi humu,tusije tukaachika bure lol.....tufundishane namna nyengine za kupika nyama,wali,mboga za majani na vile vyakula vya asili.....kujua aina moja tu ya upishi inachosha tufundishane varieties jamani..................
NB.....na wale wengine wenye recipe rahisi rahisi na fupi mnaweza kuongezea hata wakaka wanaoishi kibachela napo wapate maujuzi........mie mpaka leo sijui kupika wali wa nazi ingawa kila siku najitahidi kujaribu lol....nawish by the time naolewa niwe nimejuwa lol................

nimeona hii picha facebook,nikawa mpole mie sjui kama nitaweza kuja siku moja kutandaza meza namna hii........View attachment 31517

najua siko peke yangu wadada tuzungumze kikike mambo yasiharibike:becky::becky::mwaaah:...naombeni kwa kuanzia mnaojua zile sambusa ile nyama ya ndani ya kusaga wanatia viungo gani/wanapikaje?..........karibuni.

Pauline, hebu ongezea ugali hapo, bamia/mchicha na samaki wa kukaanga :) ili wengine tuweze kujisikia sikia kama tumepata mlo wa uhakika
 
I opened my teeth now
:becky::becky::becky:

Mkuu chapati haina kazi sana, labda chapati za kuwekea makorombwezo mpaka zionekane kama mayai ya Spanish
Chapati haina kazi??Chapati gani unaongelea wewe!??
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
I opened my teeth now
:becky::becky::becky:

Mkuu chapati haina kazi sana, labda chapati za kuwekea makorombwezo mpaka zionekane kama mayai ya Spanish

Mkate wa kusukuma bana, ule unauzungusha layer kwa layer,...! Sio chapati ilimradi imesukumwa tu :becky:

Kweli KILA MBUTU NA SHETANI WAKE . . .

hapo pamejaa vilivyokaangwa tu. Kwa meza hiyo, nampa mpishi maksi 6/10...tena sababu ya chapati tu.
The rest sijui ni uvivu wa kupika, amekaanga tu kila kitu! Na hiyo nyama ya mchuzi wala haina mvuto kiviiile!

Chapati haina kazi??Chapati gani unaongelea wewe!??

ha ha ha, anaongelea mkate wa maji huyo, sio ule kule unguja tunaouita mkate wa kusukuma.
Wakati wa kula unauchambua layer after layer...
Sio chapati ikishachomwa dakika tano baadae inakauka utadhani 'kipepeo cha mkono!'
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom