Sasa nimemuelewa kamanda Sirro

Incredible

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
1,031
1,602
Sirro ni mtu ambaye huko nyuma alikuwa na record nzuri ndani ya jeshi la polisi. Na hiyo record nzuri ndiyo iliyomfikisha kwenye nafasi aliyonayo sasa.

Kipindi mkuu wa mkoa anawataja watu kwa majina tena kwenye vyombo vya habari na kuwaambia wajisalimishe polisi, niliingia na wasiwasi juu ya uwezo wa kamanda Sirro. Nikajiuliza iweje mtuhumiwa anapewa muda ili aweke mambo yake sawa? Nikasema kamanda wangu amekuwaje? mbona anaburuzwa na huyu kijana?

Kumbe mimi nilikuwa nakosea. Mimi nilikuwa namuona mkuu wa mkoa. Kumbe kamanda wangu macho yake ni makali sana yanaona mtu aliyenyuma ya mkuu wa mkoa. Hivyo akaamua kucheza ngoma kufuatana na mdundo.

Sasa nimekuelewa kamanda wangu
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom