Bra-joe
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 1,562
- 986
Tanzania tangu uhuru tumekuwa tukiongozwa na Ccm na matokeo yake tumeyaona kuna mabaya na mazuri, kln kwa sasa ccm imetuweka ktk maisha ambayo kila siku tunasema bora ya jana, kwa kifupi ccm haina tena uwezo wa kuleta misha bora na maendeleo kwa watanzania, hivyo basi ni bora tukiweke chama kingine madarakani, na kwa sasa chama kilichojipanga kutuongoza na chenye nguvu ni Chadema, tuwachague Chadema halafu tuwape muda maalumu kuturekebishia nchi yetu, wakishindwa kurekebisha ndani ya huo muda tuwapige chini halafu tuchague chama kingine kitakachokuwa tayari wakati huo. Tukifanya hivyo vyama vya siasa vitajua watanzania tupo vipi. Mabadiliko ni muhimu.