Sasa Machinga wametushika pabaya

Sasa Machinga wametushika pabaya

Kwahiyo wewe huwa unavaa shanga? Na kwanini unaruhusu kushikwa na kupapaswa kalio? Anyway, hali ya machinga mtaani imekuwa mbaya sana...
 
Kwahiyo wewe huwa unavaa shanga? Na kwanini unaruhusu kushikwa na kupapaswa kalio? Anyway, hali ya machinga mtaani imekuwa mbaya sana...
Mkuu hiyo ni lugha ya picha tafakari mtu anapozishika shanga kwenye eneo husika anakua kafika wapi
 
Mambo mengine yanafanywa kwa ajili ya siasa haijalishi nini kietokea,hata tukio tulilolishuhudia hivi juzi la kutoa wafungwa
Mkuuu siasa aina gani hiyo zinaleta bugudha kwa wengine? Ni ndio siasa za Majitaka?
 
Serikali yetu tukufu imeruhusu Wanyonge kufanya biashara ya Umachinga holela na wasibughudhiwe wala kusumbuliwa na yeyete. Amini usiamni hiki ni kitanzi kwa Watanzania wapenda Ustaarabu.

Barabara za waenda kwa Miguu zimezibwa hivyo waenda kwa miguu wanapita njia ya Magari hatimaye kufyekea miguu yao na bodaboda.

Maeneo ya Shule za Serikali mahala pengine karibia kabisa na dirisha la darasa pamegeuka Soko la machinga (mfano mzuri ni pale Tabata Shule ya Msingi iliyo karibu na Dar West Club) Watoto usikivu umepotea madarasani. Huo ni mfano wa shule moja tu lkn hali ni mbaya sana karbia shule zote za maeneo ya Mijini.

Pale Mwanza ndio usiseme ile shule ya Sekondari imegeuzwa kuwa Stand ya Muda baada ya Nyegezi Stand kufungwa kwa muda, machinga wamevamia mpaka eneo la assemble. Inauma, inaudhi, inakera lkn ndio Kila Kiongozi anaogopa kutema kitumbua.

Upande wa Mitaro ya barabara ndio usiseme kabisaaa, yoooote inazibwa ili juuu yake Machinga ajenge kizimba chake kwa mwamvuli kwamba asiguswe wala kusumbuliwa na yeyote. Wauza embe, nanasi, miwa nk wametapakaa kila kona na wakimaliza biashara zao uchafu mwaaaa mitaroni. Sasa mitaro imejaaa na MAFURIKO yapo kila konaaaaa mvua ikinyesha. Mweeee Mhe. Rais katika hili hapana Kiongozi wangu tunataabika na kuharibu Miundombinu tuliyojenga kwa gharama kubwa.

Madhara ya ufanyaji biashara holela pia yamehatarisha wafanyabiashara wengine wakubwa kuathirika na kufunga biashara zao na kuinnyima serikali Mapato yaliyotokana na VAT nk, lkn pia Wataliii hawapendi kutembelea Nchi zisizokuwa na Mpangilio maalumu na hivyo kusababisha misongamano inayohatarisha nyendo zao wawapo kwenye eneo husika, aysee Kariakooo hapafai hata kwa dkk 1 machinga hao hao na vibaka hao haooooo katika hili Mhe. Makonda nakupongeza ingawa juhudi zako zilizimwa.

Kwa haya machache niishie kwa kusema wenye ushawishi kwa Mhe. Rais mwelezeni sasa imetosha hawa Machinga wametushika Shanga kiunoni na kalio ndio wanalipapasa kabisaaaa.(Madhara wanayosababisha hayalingani na elfu 20 ya Vitambulisho vyao).
Mkataa pema pabaya panamuita. Kwani ukikaa kimya itakugharimu nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa watu hawana shida kama wange baki kuwa Machinga, means kutembea na bidhaa wakiziuza na sio kujenga jenga hovyo vibanda kila mahala visivyo eleweka na kuziba njia za waenda kwa miguu!!!


Lakini pia kama imeshindikana kutembeza wanataka kujenga, wangepewa mchoro wa kibanda kinachotembea chenye tyres na mwavuli wa rangi moja na kinakuwa na kikapu cha taka wajitengenezee na wajipange katika maeneo yaliyo pendekezwa huku wakizingatia usafi


Nje ya kitambulisho wavae reflecta zenye utambulisho wao na wawe wasafi wooote na maeno wanayo fanyia kazi wahakikishe ni masafi ma saa24, kama zilivyo kanuni za watumishi kwenye mavazi hawa nao wapewe dress codes maana wanakaa katikati ya miji so hakuna kuwa nandala mjini, wala nguo chafu chafu wawe wasafi

Pata picha unashuka kariakoo unakuta machinga wanavibanda vyao flani hivi simple and ameizing wanaweka bidhaa zao na miavuli yao na kapu zao zataka wamejipanga vizuriiiii na wote wasafi raia na magari bado wanapita vizuuri bila tatizo, inapendeza sana!!!

Wengine niboda boda, hawa wameanzisha kujenga nao vistend vyao vya hovyo hovyo, hawa wanapaswa kuwekewa sheria wawe na reflecta zilizo printiwa jina lake na namba zake za simu


Serikali za mitaa ziwapangie vituo vidogo vidogo mitaani, na vitambulike na zisimamie ujenzi wa vituo hivyo vidogo (parking) alafu waweke ushuru mdogo wa serikali ya mtaa (100) kila piki piki inapotoka, ushuru huu uwezeshe kuboreshwa kwa usafi wa mitaaa.


Wengine wapiga debe hawa nao wanapaswa kutoka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom