Sasa Machinga wametushika pabaya

Sasa Machinga wametushika pabaya

Nilikwenda karume hatari tupu, vibanda vya biashara mpaka sehemu ya stand, hakuna pakusimama abiria kusubiria gari.
 
Ajira hizo Mkuuu
Machinga....
Bodaboda....
Betting.....
Teheteheeeeee
Betting inafanyika kote duniani, tena na mataifa yaliyoendelea. Ondoa betting katika orodha yako.

Mzee baba anazingua sana, hakuna ustaarabu kabisa mitaani Kwa sasa, kila kona kuna kijibanda, hadi barabarani. Lile lorry pale Milimani city ni matokeo ya watu kujipanga pembeni mwa barabara na kujifanyia biashara.
 
Nini kifanyike mkuu!! wenye exposure ya mataifa ya wenzetu hasa Waafrika wenzetu kwani wao wanafanyaje swala la wamachinga!! Ukweli hili swala limekuwa changamoto, Pale round about ya Mwanza jengo la Nyerere wamama wamepanga bidhaa barabaran muda wa jioni umakini unaotajika kwa wenye Magari..
 
Nini kifanyike mkuu!! wenye exposure ya mataifa ya wenzetu hasa Waafrika wenzetu kwani wao wanafanyaje swala la wamachinga!! Ukweli hili swala limekuwa changamoto, Pale round about ya Mwanza jengo la Nyerere wamama wamepanga bidhaa barabaran muda wa jioni umakini unaotajika kwa wenye Magari..
Mkuuu tukumbukeni mwamba siyo kila mtu awe machinga. Hivyo yaandaliwe maeneo rasmi ili biashara yao isiwe bugudha kwa wengine"
 
Rais wa wanyonge na masikini. Anasema hao ndio wapiga kura wake waliompa ushindi wa kishindo.
 
Nini kifanyike mkuu!! wenye exposure ya mataifa ya wenzetu hasa Waafrika wenzetu kwani wao wanafanyaje swala la wamachinga!! Ukweli hili swala limekuwa changamoto, Pale round about ya Mwanza jengo la Nyerere wamama wamepanga bidhaa barabaran muda wa jioni umakini unaotajika kwa wenye Magari..
Kuwe na maduka 24hrs. Kariakoo, tandika, mwananyamala na ferry.
Mtaa uwe na urefu wa kilometa moja na nusu au mile moja.
Mtaa uwe na taa za kutosha, barabara pana na defender mwanzo, na mwisho. Askari wa miguu katikati.
Kama pattaya Thailand au one moe Manila. Au walau kama forodhani gardens lakini pia kuwe na biashara za vitu vingine siyo chakula tu.
Kariakoo patapungua sana.
 
Wafanye biashara pasipo kuleta usumbufu kwa wengine vinginevyo sio HAKI. Endapo haki yako inaathiri haki ya mwingine hapo tambua kwamba kuna kasoro ya Utawala. Haki ya Machinga kufanya Biashara inapoingilia Haki ya Mwanafunzi kusoma, Inapoingilia haki ya Mtembea kwa Miguu mpaka anagongwa na gari, inapoingilia haki ya Mfanya biashara aliyekata leseni TRA na analipa VAT halafu Watanzania wastaarabu tuache huuu upuuuuzj uendeleee tutakuwa hatumpendi Mhe.Rais penye ukweli lazima usemwe na Msema kweli ni Mpenzi wa Mungu. Nasema Machinga wamevuruga ustaarabu na mifumo ya utoaji huduma katika Jamiii, wawe na Mipakaa imetosha.
Yaani Siku hizi Majiko ya kupikia, Nyama/mishikaki Choma, mahindi Choma, wapika Supu, wakaanza mihogo. Ndizi na Chips na Biis Sufuria na Majiko ya Moto ni Barabarani na vituo vya Mabasi vya kuzibiti Abiria. Kuna Siku nilinusurika kuchomwa na mafuta ya Moto ya kwenye Karai njiani. Yaani Biashara ya Chakula ni Holela Pita Mwenge, Posta Mpya, Pamba Road mjini, Ubungo utajionea Usumbufu huu. Hotel zimefungwa Majiko yamehamishiwa Side Walk(Pedestrians ways).
 
Unasema wameshaanza kukupapasa sehemu gani???? Rekebisha sentensi please
 
Unasema wameshaanza kukupapasa sehemu gani???? Rekebisha sentensi please
Mkuuu hao watu wanachungulia kaburini...
Si umeskia wameanza kuparamiwa na malori huko barabarani. Kule Moro waliuliwa, Moshi pia, Majuzi tena Mlimani City tusipochukua hatua yatakuja maaffa makubwa halafu tuseme ni Mipango ya Mungu.
 
Mkuuu hao watu wanachungulia kaburini...
Si umeskia wameanza kuparamiwa na malori huko barabarani. Kule Moro waliuliwa, Moshi pia, Majuzi tena Mlimani City tusipochukua hatua yatakuja maaffa makubwa halafu tuseme ni Mipango ya Mungu.
Kwa awamu hii itakuwa sawa na kumpigia mbuzi gitaa,labda awamu ya 6
 
Serikali yetu tukufu imeruhusu Wanyonge kufanya biashara ya Umachinga holela na wasibughudhiwe wala kusumbuliwa na yeyete. Amini usiamni hiki ni kitanzi kwa Watanzania wapenda Ustaarabu.

Barabara za waenda kwa Miguu zimezibwa hivyo waenda kwa miguu wanapita njia ya Magari hatimaye kufyekea miguu yao na bodaboda.

Maeneo ya Shule za Serikali mahala pengine karibia kabisa na dirisha la darasa pamegeuka Soko la machinga (mfano mzuri ni pale Tabata Shule ya Msingi iliyo karibu na Dar West Club) Watoto usikivu umepotea madarasani. Huo ni mfano wa shule moja tu lkn hali ni mbaya sana karbia shule zote za maeneo ya Mijini.

Pale Mwanza ndio usiseme ile shule ya Sekondari imegeuzwa kuwa Stand ya Muda baada ya Nyegezi Stand kufungwa kwa muda, machinga wamevamia mpaka eneo la assemble. Inauma, inaudhi, inakera lkn ndio Kila Kiongozi anaogopa kutema kitumbua.

Upande wa Mitaro ya barabara ndio usiseme kabisaaa, yoooote inazibwa ili juuu yake Machinga ajenge kizimba chake kwa mwamvuli kwamba asiguswe wala kusumbuliwa na yeyote. Wauza embe, nanasi, miwa nk wametapakaa kila kona na wakimaliza biashara zao uchafu mwaaaa mitaroni. Sasa mitaro imejaaa na MAFURIKO yapo kila konaaaaa mvua ikinyesha. Mweeee Mhe. Rais katika hili hapana Kiongozi wangu tunataabika na kuharibu Miundombinu tuliyojenga kwa gharama kubwa.

Madhara ya ufanyaji biashara holela pia yamehatarisha wafanyabiashara wengine wakubwa kuathirika na kufunga biashara zao na kuinnyima serikali Mapato yaliyotokana na VAT nk, lkn pia Wataliii hawapendi kutembelea Nchi zisizokuwa na Mpangilio maalumu na hivyo kusababisha misongamano inayohatarisha nyendo zao wawapo kwenye eneo husika, aysee Kariakooo hapafai hata kwa dkk 1 machinga hao hao na vibaka hao haooooo katika hili Mhe. Makonda nakupongeza ingawa juhudi zako zilizimwa.

Kwa haya machache niishie kwa kusema wenye ushawishi kwa Mhe. Rais mwelezeni sasa imetosha hawa Machinga wametushika Shanga kiunoni na kalio ndio wanalipapasa kabisaaaa.(Madhara wanayosababisha hayalingani na elfu 20 ya Vitambulisho vyao).
Picha
 
Mambo mengine yanafanywa kwa ajili ya siasa haijalishi nini kietokea,hata tukio tulilolishuhudia hivi juzi la kutoa wafungwa
 
Back
Top Bottom