kabanga;
Usiwe ka hao wasio na roho ya huruma. Imagine; ametokea hospitali, mtoto kalazwa ghafla. Mr. ndo alimtupa siku tele. Tangu ametoka home hajanywa hata uji. Saa zimeenda, na watoto wengine tangu warudi shule mlango umefungwa.
Kwa sababu zisizotabirika, kadi imemezwa. Saa za kazi zimekwisha saa nyingi. Atarudije home? Ataupata wapi msaada hata wa msamaria mwema kumpa nauli? Mji shule, kila mbuzi hula usawa wa kamba. Nani anamjali mwenzake?
Naamini, kwa kuwa alijua Mungu hajamwacha, hata kama kadi haikutoka, lakini kulitokea muujiza na si ajabu weye uliyempiga picha alipokuelezea masahibu yake, ulimsaidia. Huo ndo muujiza. Popote ulipo, Mungu amesema; Niite nami nitakuitikia, nitakuonesha mambo makubwa, magumu usiyo yajua.
Nasema; Lazima Mungu alimsikia. Si kila ombi ni kutoa pepo, mengine ni kuita miujiza itokee hima. Nawasilisha
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.