KERO Sarafu za Sh. 100 na 200 zimepotea mtaani

KERO Sarafu za Sh. 100 na 200 zimepotea mtaani

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Hili suala la sarafu kuadimika limekaaje? Niliona kwenye forum Moja ya Mwananchi wakiuliza kwa Afisa Sarafu B.O.T kuhusu kuadimika kwa sarafu hasa Tsh 100, Tsh 200 lakini alijibu kua hakuna shida hio na sarafu zipo.

Sasa swali ni kua nini kinaendelea kwa sababu mtaani hazionekani kweli na Kuna maeneo wanauza hizi sarafu kwa bei mbaya. Ukitoa elfu moja unapewa Tsh 600 ya sarafu za mia mia.

Kwanini kusiwe na uwazi juu ya hili ili hata watu wanaopanga bei wajue namna ya kuendana na hili. Maana watu tunaacha sana hizi chenchi lakini wao wanasema hakuna tatizo
 
Mia nyingi ni mbovu bora hata hamsini ingawa zote hazipo kwenye mzunguko kitaa

mia mbili tuwaulize wachina wa ma bonanza wanazipeleka wapi

mia tano au jero nazo zinapotea hata buku buku change yake ni tizi
Sijui tatizo ni nini?
 
Kiuweli sisi tunaofanya biashara zinzohusisha hzo sarafu tajwa imekua changamoto unajikuta umeacha hela nyingi Kwa siku...Na baadhi ya watu wamekua wakitumia hl Kwa maslahi binafsi... Ajabu ni kwamba mamlaka husika hazitoi taarifa yyte wamekaa kimya tu.
 
Mia nyingi ni mbovu bora hata hamsini ingawa zote hazipo kwenye mzunguko kitaa

mia mbili tuwaulize wachina wa ma bonanza wanazipeleka wapi

mia tano au jero nazo zinapotea hata buku buku change yake ni tizi
Sijui tatizo ni nini?
Yaan sku ya mzunguko wa biashara n kazi unatembe kutafuta buku buku kweli
 
Tanzania tuko nyuma sana wenzetu wakenya wako juu kwa matumizu ya card au kulipa kwa simu nilishangaa hadi mama mboga wanapokea pesa kwa lipa namba nilishangaa mno
Nadhani hadi kwenye daladala na bodaboda pia.
 
Back
Top Bottom