Hakuna jina limfaalo Sita kwa sasa maana tukimwita mhuni, wahuni wengi madhara yao huwa si kama ya Sita. Tukimwita mwizi, wevi wa kawaida huwa hawaibi pesa nyingi kama hizi alizoiba Sita na wenzake. Tukimwita mhaini, wahaini hupindua serikali, lakini Sita amepindua mamlaka ya wananchi.
Huyu Sita hakuna hata adhabu imfaayo. Akigombea tukamnyima kura, hata watu wema kuna wakati wanakosa kura. Akiwekwa jela, hata wevi wa kuku wapo jela. Tukiamua anyongwe, kuna walionyongwa kwa kuua hata mtu mmoja tu lakini Sita ameua Taifa lililotarajiwa. Sita anafaa kupewa adhabu gani? Mungu ndiye ajuaye.