Samsung Galaxy note 3 dual vs sony xepria z3 with dual

Samsung Galaxy note 3 dual vs sony xepria z3 with dual

MAHENDEKA

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2010
Posts
340
Reaction score
181
Heshima kwenu wakuu na wajuzi wajuzi wa mambo

Ipi ni simu bora kati ya hizo mbili tukianza kuzichambua kipengele kimoja kimoja ?.Na je ipi ni simu bora yenye ufanisi kiujumla/overal performance ?

Kama kuna mtu anaweza kuweka tofauti katika lugha rahisi asaidie tafadhali,maaana nimetembelea huko GSMArena.com - GSM phone reviews, news, opinions, votes, manuals and more... nmekuta tofauti zake lakini mwisho wa siku nashindwa kujua maana kuna maneno yalokaa kiufundi sana


Hilo ni moja pili nina simu nimeletewa kama zawadi kutoka america kaskazini ni samsung galaxy note 3,lakini hii simu haikubali line kwa maana ya kwamba ukiweka line haisomi,nimefurukuta nayo mpaka nimeona nijisalimishe hapa kwa msaada zaidi.Simu hii ukiiwasha wakati inawaka inaandika neno "Sprint",mtu mmoja kaniambia kwamba hio simu imefungwa sasa sijajua imefungwaje ?

Tusaidiane wakuu mimi nna knowledge kidogo ya IT.
Naomba kuwakilisha
 
Heshima kwenu wakuu na wajuzi wajuzi wa mambo

Ipi ni simu bora kati ya hizo mbili tukianza kuzichambua kipengele kimoja kimoja ?.Na je ipi ni simu bora yenye ufanisi kiujumla/overal performance ?

Kama kuna mtu anaweza kuweka tofauti katika lugha rahisi asaidie tafadhali,maaana nimetembelea huko GSMArena.com - GSM phone reviews, news, opinions, votes, manuals and more... nmekuta tofauti zake lakini mwisho wa siku nashindwa kujua maana kuna maneno yalokaa kiufundi sana


Hilo ni moja pili nina simu nimeletewa kama zawadi kutoka america kaskazini ni samsung galaxy note 3,lakini hii simu haikubali line kwa maana ya kwamba ukiweka line haisomi,nimefurukuta nayo mpaka nimeona nijisalimishe hapa kwa msaada zaidi.Simu hii ukiiwasha wakati inawaka inaandika neno "Sprint",mtu mmoja kaniambia kwamba hio simu imefungwa sasa sijajua imefungwaje ?

Tusaidiane wakuu mimi nna knowledge kidogo ya IT.
Naomba kuwakilisha

Kuhusu Galaxy Note 3 ya sprint hiyo nafikiri ni CDMA sahau au poteza ndoto ya kuitumia Tanzania labda kama haupo Tanzania
CDMA providers ni TTCL na ZANTEL tu sasa sijajua kama wataweza kukupa Line za CDMA hao jamaa

Kuhusu Galaxy Note 3 Duos na Xperia Z3 Duos ntaongelea tu Camera na Battery life
Kwa kuangalia fasta Inaonesha Note 3 duos pamoja kwamba ina screen display kubwa battery lake(3200mah) ina uwezo mkubwa na battery life imeipita ya Z3 Duos(3100mah)

Wakati Z3 ina camera nzuri zaidi 20.7MP Note3 duos ina 13MP

Siwezi Ongelea snapdragon maana sizielewi tofauti zake labda wataalamu zaidi wataelleza ila vitu vingine ukiachana na Size vimefanana
 
kamera kama ipo zaidi ya nane mega pixel basj nali betry maana ndio inayokupa utulivu mzuri,mie natumia bb10 iko ovyo lkn kwa sasa application ni za social tu ndio natumia so inanifaa
 
Kuhusu Galaxy Note 3 ya sprint hiyo nafikiri ni CDMA sahau au poteza ndoto ya kuitumia Tanzania labda kama haupo Tanzania
CDMA providers ni TTCL na ZANTEL tu sasa sijajua kama wataweza kukupa Line za CDMA hao jamaa

Kuhusu Galaxy Note 3 Duos na Xperia Z3 Duos ntaongelea tu Camera na Battery life
Kwa kuangalia fasta Inaonesha Note 3 duos pamoja kwamba ina screen display kubwa battery lake(3200mah) ina uwezo mkubwa na battery life imeipita ya Z3 Duos(3100mah)

Wakati Z3 ina camera nzuri zaidi 20.7MP Note3 duos ina 13MP

Siwezi Ongelea snapdragon maana sizielewi tofauti zake labda wataalamu zaidi wataelleza ila vitu vingine ukiachana na Size vimefanana


nimeona samsung galaxy note 3 ina super amoled na sony xperia z3 ina lps lcd,hizi ni specifications za display

imekaaje hii ?
 
nimeona samsung galaxy note 3 ina super amoled na sony xperia z3 ina lps lcd,hizi ni specifications za display

imekaaje hii ?

Ndugu MAHENDEKA
Hizi ni display za kisasa zenye ubora wa hali ya juu, ukilinganisha na display za kawaida. Yaani ni kama exclusive kwa kuwa huwezi kukuta display hizi katika simu za bei ya kawaida. Nitaainisha tofauti zake.

LCD
Hii inafahamika kama "Liquid Crystal Display" LCD ni abbreviation tu. Kama jina linavyojitaja, display hii imetengenezwa na liquid crystals ambazo zikutana na mwanga zinatengeneza rangi halisi na zenye mvuto. Lakini LCD haipo vizuri katika kutengeneza realistic black. (Yaani rangi nyeusi inakuwa brighter kidogo. LCD inatumia teknolojia mpya iitwayo IPS (In-Pane Switching) ambayo inaboresha muonekano wa rangi na unakuwa unaexperience viewing agles zenye muonekano thabiti. Sifa kubwa ya LCD ni kwamba zinadumu zaidi.

AMOLED (Active Matrix Organic Light Emitting Diode) ni teknolojia iliyojipatia umaarufu mkubwa sana kwa miaka ya karibuni, display hii utikuta sana katika Samsung Smartphones ama Nokia. Simu kama Nokia N8, Lumia 820 ni baadhi ya Nokia zinazotumia display za AMOLED, pia Samsung ndiyo wamekuwa watumiaji wakubwa wa AMOLED displays. Screen za amoled zimetengeezwa kwa gamba lenye molecules nyingi ambazo zinatoa mwanga endapo zikikutana na mkondo wa umeme. Teknolojia hii rahisi ya amoled imeweza kutumika kufanya matengenezo ya screen nyembamba ambazo hazihitaji backlight. Kwa mantiki hii, AMOLED screens zinakuwa zinazalisha rangi nyeusi amabayo ni nzito sana, yaani inakuwa imekolea kiasi kwamba pixels za mwanga hazihitaji kutumika wakati kwa sehemu zote zenye rangi nyeusi zinapoonekana kwenye picha wakati unapotumia simu yako. Na hii ni sababu kubwa ya simu zenye amoled screen kupunguza may matumizi makubwa ya battery. Pia kuna Amoled iliyoboreshwa zaidi iitwayo Super Amoled ambayo utaikuta kwenye devices za hadhi ya juu.

FAIDA:
AMOLED.
• Display hii ina contrast ya kiwango cha juu.
• Ina rangi nzuri iliyokolea (Saturated colors)
• Ina rangi ambazo zinavutia kwa macho yako.
• Bado ni technolojia mpya ambayo inaendelea kukua na improvements nyingi zitafanyika kuongeza ubora.
• Inarespond kwa haraka sana, katika activities za mtumiaji.

IPS:
• Ni technolojia kongwe, kwa hiyo ina asilimia kubwa ya kuendelezwa.
• Ina zalisha rangi halisi kabisa (kasoro black ambayo inakuwa inaonekana kama grey)
• Inazalisha mwanga mkubwa zaidi.
• Ni muhimu kutumika mahali popote (kwa kuwa hata sehemu kama juani, bado utaona vyema.

HASARA:
AMOLED. Hasara kubwa ya kutumia device yenye Amoled ni kwamba ina limited lifetime (ambayo ni miaka mitano) screen hizi huweza kuchoka mapema iwapo mtumiaji atakuwa anatumia screen kwa maximum brightness, ambayo husababisha light pixels kuchoka mapema. Lakini hili lisikue wasiwasi kutokana kuwa Amoled technology bado ni mpya na inazidi kukua, hivyo maboresho yataongezeka maradufu.

LCD
Hasara kubwa ya LCD ni kuwa inatumia kiasi kikubwa cha umeme kutokana na kutumia technology backlight kuongeza mwanga zaidi katika screen. Pia LCD ni technolojia kongwe hivyo hakuna haja ya kutegemea maboresho mengi (Maboresho makubwa hayatatokea, labda madogomadogo tu).
 
Last edited by a moderator:
Wadau nimefanikiwa kupata sony xperia z3 dual, hii simu ni bora kuliko nilivyodhani na inastahili pesa,haingii maji,kamera ina ubora wa hali ya juu 20mega-pixel,inaendesha magemu makubwa makubwa vizuri tu haijastuck kwenye mazingira yeyote yale

battery inadumu kiasi,mimi mtumiaji wa internet karibia masaa 24 nipo on skype,whatsapp,twitter,facebook,tango jamiiforums instagram nk nk lakini nadumu na chaji kwa siku moja na nusu,nikizima data nakaa siku mbili na nusu

Disadvantage niloiona hadi sasa ni kwamba hii simu ni kama inachemka flani hivi unapokuwa umetumia camera kwa muda mrefu au ukiwa unasikiliza muziki kwa muda mrefu

Disadvantage ingine ni kwamba kioo chake hicho lcd kinakula asilimia kubwa ya chaji zaidi ya 40% lakini pamoja na hayo battery linakwenda mpaka siku moja na nusu, sasa kama wakifanyia modifications zaidi hii simu itakuwa bora zaidi

Pili ni display ipo vizuri (tft lcd) lakini sio kama ile ya samsung galaxy note 3(super amoled)....hii super amoled ina display nzuri kuliko hio ya (tft lcd) lakini sio rahisi kwa user kawaida kugundua tofauti zake

Najivunia kuwa kwenye ulimwengu wa sonny
 
Samsung ni nguo ya maduka ya kihindi Kila mtu anayo. Performance ya Samsung haiwezi kufikia Sony.
 
Back
Top Bottom