GE2025 Samia: Tunataka Tanzania ijitegemee Kiuchumi bila kutegemea mikopo mikubwa kutoka nje

GE2025 Samia: Tunataka Tanzania ijitegemee Kiuchumi bila kutegemea mikopo mikubwa kutoka nje

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Mgombea Urais wa CCM, Samia Suluhu Hassan, akizungumza katika kampeni za Uchaguzi Mkuu katika eneo la Dakawa, Mvomelo, Mkoa wa Morogoro leo, tarehe 30 Agosti 2025, amesema lengo la Serikali ni kuona Tanzania ikijitegemea kiuchumi kufikia mwaka 2050, bila kutegemea mikopo mikubwa kutoka nje, akisisitiza umuhimu wa sera na mikakati endelevu ya maendeleo inayolenga kuimarisha uchumi wa taifa na kuboresha maisha ya wananchi.

"Niwaombe sasa, tusimame pamoja na kukiunga mkono Chama Cha Mapinduzi ili tuendelee na kasi ya kuijenga Tanzania tunayoitaka. Tumesema ikifika 2050, Dira yetu inatuambia tuwe tumefika kwenye Tanzania tunayoitaka- Tanzania ya uchumi wa kipato cha kati lakini cha ngazi ya juu, Tanzania ambayo hakuna atakayelia na huduma za afya wala huduma za elimu wala atakayekosa maji bora na kukosa umeme wa kufanyia kazi zake na kumwangazia pahali alipo. Hiyo ndiyo Tanzania tunayoitaka, Tanzania ambayo uchumi wake utasimama na kujitegemea, Tanzania ambayo hatutaishi wala kufanya shughuli zetu za maendeleo kwa mikopo mikubwa, hiyo ndiyo Tanzania tunayoitaka, ifikapo mwaka 2050, safari yake inaanza miaka mitano inayokuja"
 

Attachments

  • SAMIA MVOMELO.mp4
    17.7 MB
Kwahiyo tujitegemee ila kwa mikopo midogo.. kwanini asiitoe yote
 
Mgombea Urais wa CCM, Samia Suluhu Hassan, akizungumza katika kampeni za Uchaguzi Mkuu katika eneo la Dakawa, Mvomelo, Mkoa wa Morogoro leo, tarehe 30 Agosti 2025, amesema lengo la Serikali ni kuona Tanzania ikijitegemea kiuchumi kufikia mwaka 2050, bila kutegemea mikopo mikubwa kutoka nje, akisisitiza umuhimu wa sera na mikakati endelevu ya maendeleo inayolenga kuimarisha uchumi wa taifa na kuboresha maisha ya wananchi.

Huyu jamaa naye anaongea utafikiri ana basics za uchumi na maendeleo
 
Mgombea Urais wa CCM, Samia Suluhu Hassan, akizungumza katika kampeni za Uchaguzi Mkuu katika eneo la Dakawa, Mvomelo, Mkoa wa Morogoro leo, tarehe 30 Agosti 2025, amesema lengo la Serikali ni kuona Tanzania ikijitegemea kiuchumi kufikia mwaka 2050, bila kutegemea mikopo mikubwa kutoka nje, akisisitiza umuhimu wa sera na mikakati endelevu ya maendeleo inayolenga kuimarisha uchumi wa taifa na kuboresha maisha ya wananchi.


Mbona anajichanganya sasa!

Maana uongozi wake ndio umekuwa kinara wa kukopa na kupitia waziri wa fedha wamekuwa wakikiri wazi kwamba wanakopa na wataendelea kukopa maana hata Marekani ina madeni...
 
Nilistuka hapo aliposema tumpe kura Salha, kumbe Sarah; nikajisemea huyu mama sasa anakufuru.

Sababu ya kustuka ‘Bi Tozo’ ana mtoto wa mdogo wake nae anaitwa Salha anaishi Morogoro (walau she is educated), before that alikuwa U.K.

Yupo fisadi mmoja kajivutia jiko, ili ale neema za zama hizi kwa uraisi na yeye.

Ukitaka kumjua huyo Salha, Junaithar alikuwa ana mpost sana kama best friend miaka ya nyuma kabla Samia ajawa raisi.
 
Back
Top Bottom