PostGE2025 Samia: Tofauti za kiitikati zisitugawe kama Taifa

PostGE2025 Samia: Tofauti za kiitikati zisitugawe kama Taifa

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza kuwa Serikali imeanza kuchukua hatua za kuunda Tume ya Maridhiano ya Kitaifa ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kujenga na kuimarisha umoja wa kitaifa kuelekea mwaka 2026, kufuatia changamoto za kisiasa na kijamii zilizojitokeza nchini mwaka 2025.

Akihutubia Taifa katika salamu za kufunga Mwaka 2025 na kuukaribisha Mwaka Mpya 2026, tarehe 31 Desemba 2025, kutoka Ikulu Ndogo ya Tunguu Zanzibar, Rais Samia amesema utulivu wa kisiasa pamoja na hali ya amani na usalama ni nguzo muhimu ya maendeleo ya taifa.

Amesema mwaka 2025, licha ya mafanikio makubwa yaliyopatikana, Taifa lilipitia pia changamoto na mitihani iliyowagusa Watanzania wengi, hususan katika kipindi cha mwezi Oktoba, ambacho kilihitaji subira, mshikamano na uzalendo wa hali ya juu.

Rais Samia amevishukuru vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na wananchi wote kwa kuendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano wa Taifa, hatua iliyoiwezesha Tanzania kudhihirisha mbele ya ulimwengu kuwa ni taifa imara, himilivu na lenye uwezo wa kushughulikia changamoto zake kwa misingi ya amani.

Ameeleza kuwa Serikali inapoanza mwaka 2026 imejipanga kujenga upya mshikamano wa kitaifa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, ambapo maandalizi ya kuunda Tume ya Maridhiano yameanza rasmi.

Kwa mujibu wa Rais Samia, Serikali itahusisha wadau wote katika mchakato wa kukubaliana kuhusu muundo wa tume hiyo, ikiwemo aina ya wajumbe, majukumu yao pamoja na muda wa utekelezaji wa kazi za tume, kwa lengo la kuimarisha umoja, amani na mshikamano wa Watanzania.
 
Wako wapi
IMG-20251228-WA0010.jpg
 
Huyu hazimo kabisa maridhiano atafanya na nani Lisu kamtupa lupango Polepole hajulikani alipo Gwajima ndiyo hivyo tena, watu bado wanatekwa kuna mpasuko unaendelea kati Tec na Waislam au machawa nk. Haya maridhiano ni ya namna gani.
 
Kaanza kulegea kaona mambo magumu hadi kuanza kusema wananchi wapendekeze wajumbe wa maliziano
 
Mbona amemweka Tundu Lissu ndani kwa sababu ya itikadi za kisiasa. Madhara ya raisi wa kuazima kutoka nchi jirani. Ameua Watanganyika na amejificha kwao zanzibar. Huyu ndo mzanzibar wa mwisho kutawala watanganyika. Haitatokea tena hadi mwisho wa dunia. Angekuwa mtanganyika mauaji yasingetokea kamwe. Huwezi kuuwa ndugu zako. Na bado anataka kupenyeza virusi vya udini...
 
Hivi ICC bado tu hawajamaliza kuchambua zile taarifa walizopewa na mashirika mbalimbali za haki za binadamu duniani ili waje waanze uchunguzi.

Time is running out and the justice delayed is the justice denied. We shall vanquish.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza kuwa Serikali imeanza kuchukua hatua za kuunda Tume ya Maridhiano ya Kitaifa ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kujenga na kuimarisha umoja wa kitaifa kuelekea mwaka 2026, kufuatia changamoto za kisiasa na kijamii zilizojitokeza nchini mwaka 2025.

Akihutubia Taifa katika salamu za kufunga Mwaka 2025 na kuukaribisha Mwaka Mpya 2026, tarehe 31 Desemba 2025, kutoka Ikulu Ndogo ya Tunguu Zanzibar, Rais Samia amesema utulivu wa kisiasa pamoja na hali ya amani na usalama ni nguzo muhimu ya maendeleo ya taifa.

Amesema mwaka 2025, licha ya mafanikio makubwa yaliyopatikana, Taifa lilipitia pia changamoto na mitihani iliyowagusa Watanzania wengi, hususan katika kipindi cha mwezi Oktoba, ambacho kilihitaji subira, mshikamano na uzalendo wa hali ya juu.

Rais Samia amevishukuru vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na wananchi wote kwa kuendelea kudumisha amani, umoja na mshikamano wa Taifa, hatua iliyoiwezesha Tanzania kudhihirisha mbele ya ulimwengu kuwa ni taifa imara, himilivu na lenye uwezo wa kushughulikia changamoto zake kwa misingi ya amani.

Ameeleza kuwa Serikali inapoanza mwaka 2026 imejipanga kujenga upya mshikamano wa kitaifa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, ambapo maandalizi ya kuunda Tume ya Maridhiano yameanza rasmi.

Kwa mujibu wa Rais Samia, Serikali itahusisha wadau wote katika mchakato wa kukubaliana kuhusu muundo wa tume hiyo, ikiwemo aina ya wajumbe, majukumu yao pamoja na muda wa utekelezaji wa kazi za tume, kwa lengo la kuimarisha umoja, amani na mshikamano wa Watanzania.
View attachment 3523304
Vipi zile za kikwapuaji kifisadi na za kiccm zilivyotugawa kama taifa?
 
Unahubiri maridhiano, halafu wakati huo huo kuna kiongozi wa chama kikuu cha upinzani, na chenye mashabiki wengi umemfunga gerezani kwa hila! Unahubiri maridhiano halafu kuna chawa wako lukuki kila siku wanajitokeza hadharani kuwashambulia TEC na Wakatoliki!

Hakika kuna mambo yanastaajabisha sana.
 
Mashehe wakatavichwa hawajakamatwa hajawakemea na Rais wa kweli Yuko selo yeye anataka kuridhiama na nanai?
 
Back
Top Bottom