Samia: Serikali ya Dk. Magufuli itanunua meli tano

Samia: Serikali ya Dk. Magufuli itanunua meli tano

chaikavu

JF-Expert Member
Joined
Apr 18, 2015
Posts
760
Reaction score
473

Samia-19Sept2015.png

Mgombea mwenza wa urais, kupitia CCM Samia Suluhu Hassan.


Mgombea mwenza wa urais, kupitia CCM Samia Suluhu Hassan, amesema chama chake kikishinda katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, serikali ya Dk. John Magufuli, itanunua meli tano kubwa, ikiwamo ya shughuli za uvuvi katika ukanda wa kiuchumi wa Bahari ya Hindi.

Aidha, imeahidi kuingiza nchini meli nyingine nne za kisasa zitakazofanya kazi ya kutoa huduma ya usafiri kati ya kisiwa cha Mafia, Dar es Salaam, Mtwara, Lindi na Tanga.

Aliyasema hayo jana katika mkutano wake wa hadhara wa kampeni uliofanyika mjini hapa, akitokea mkoani Mtwara.

Alisema serikali ya awamu ya tano itakayoundwa na Dk. John Magufuli, imepanga kuimarisha usafiri wa Bahari ya Hindi ikiwamo Mafia, ambako itaelekeza nguvu kwa kununua boti tano kubwa za usafiri na uvuvi.

"Mafia mnastahili kuwezeshwa zaidi hasa baada ya kuonyesha juhudi zenu kwa kujenga kiwanda cha samaki lakini ilani yetu pia inasema tutanunua vyombo kwa ajili ya uvuvi ili kwenda katika ukanda wa kiuchumi wa bahari kuu na kuvua samaki wenye thamani kubwa. Mpango huu kwanza utakuza ajira na kufungua fursa nyingine," alisema.
Alisema katika awamu hiyo, Serikali ya CCM imejiwekea pia malengo ya kuanzisha uhifadhi wa bahari, katika kisiwa cha Mafia ili kutunza mazingira ya bahari na kufuga samaki wengi zaidi.

"Nawaomba wataalam watakapokuja Mafia, mtoe maoni yenu ili ijulikane maeneo ya kufanyiwa uhifadhi na yatakayoachwa huru kwa ajili ya shughuli za uvuvi," alisisitiza. Kuhusu kuwawezesha kiuchumi wakazi wa Mafia, Samia alisema Ilani ya CCM inaeleza kwamba itatenga Sh. 1,000,000 katika kila kijiji cha Mafia ili kuwawezesha wananchi wake kununua vyombo vikubwa vya uvuvi. Awali, mgombea ubunge wa jimbo la Mafia, Mbaraka Dau, alisema pamoja na mafanikio yaliyotekelezwa visiwani hapo na mbunge anayemaliza muda wake Abdulkarim Shaha, bado jimbo hilo lina changamoto kadhaa.

CHANZO: NIPASHE


 
Yeye kaaidi tano ndo watakazo nunua na huyo magufuli sasa kama ni tano magufuli kesha ahidi meli mbili Mpya na bado mahitaji ya meli Mpya yapo ukiwa muongo usiwe mwepesi kusahau,
 
maskrepa kwenu ni meli?....bora mkae kimya tu!
 
CCM ni magwiji Wa kutoa ahadi za uongo mpaka sasa wameshaahidi ahadi tele mpaka zingine wamesahau
 
Yaani wanafikiri watanzania wote wana vichwa vya nyumbu! Jamani mwenye ile orodha ya ahadi za JK za 2010 anaweza kutuwekea hapa? Kama sikosei JK alitoa ahadi kama hizo hizo.
 
Nasikitika Magufuli ameingia katika mtego ule ule uliomnasa Kikwete
 
Na zile laptop bado zitagawiwa wadau wa chaki?
 
ILANI ya sisi em mbona hayapo hayo maadi ya meli!!
Watasema yale yale ya j.kikwete mpk anaondoka meli hatujaziona mwz...
 
amesema pia watafanya sensa ya samaki na dagaa wote kwenye lakes na bahari ya hindi ili kuzuia uvuvi haramu
 
Jaman CCM msiongeleee meli, huyo magufuli katununulia kivuko cha mwaka 1978, hatutaki meli
 
Mimi binafsi nakerwa na kitendo/vitendo vya hawa ccm kuwa watu ahadi hivi ni kwanini nyie mnakuwa watu wa kuhaidi haidi hili hali mmeshapewa ridhaa kwa muda mrefu.tuelezeni yale mliotufanyia na mikakati ya yale pungufu mtayatekeleza vipi?
 
[h=2]Samia: Serikali ya Dk. Magufuli itanunua meli tano.[/h]


NA GODFREY MUSHI



19th September 2015


email.png

B-pepe



printer.png

Chapa










Samia-19Sept2015.png

Mgombea mwenza wa urais, kupitia CCM Samia Suluhu Hassan.


Mgombea mwenza wa urais, kupitia CCM Samia Suluhu Hassan, amesema chama chake kikishinda katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, serikali ya Dk. John Magufuli, itanunua meli tano kubwa, ikiwamo ya shughuli za uvuvi katika ukanda wa kiuchumi wa Bahari ya Hindi.

Aidha, imeahidi kuingiza nchini meli nyingine nne za kisasa zitakazofanya kazi ya kutoa huduma ya usafiri kati ya kisiwa cha Mafia, Dar es Salaam, Mtwara, Lindi na Tanga.

Aliyasema hayo jana katika mkutano wake wa hadhara wa kampeni uliofanyika mjini hapa, akitokea mkoani Mtwara.

Alisema serikali ya awamu ya tano itakayoundwa na Dk. John Magufuli, imepanga kuimarisha usafiri wa Bahari ya Hindi ikiwamo Mafia, ambako itaelekeza nguvu kwa kununua boti tano kubwa za usafiri na uvuvi.

“Mafia mnastahili kuwezeshwa zaidi hasa baada ya kuonyesha juhudi zenu kwa kujenga kiwanda cha samaki lakini ilani yetu pia inasema tutanunua vyombo kwa ajili ya uvuvi ili kwenda katika ukanda wa kiuchumi wa bahari kuu na kuvua samaki wenye thamani kubwa. Mpango huu kwanza utakuza ajira na kufungua fursa nyingine,” alisema.
Alisema katika awamu hiyo, Serikali ya CCM imejiwekea pia malengo ya kuanzisha uhifadhi wa bahari, katika kisiwa cha Mafia ili kutunza mazingira ya bahari na kufuga samaki wengi zaidi.

“Nawaomba wataalam watakapokuja Mafia, mtoe maoni yenu ili ijulikane maeneo ya kufanyiwa uhifadhi na yatakayoachwa huru kwa ajili ya shughuli za uvuvi,” alisisitiza. Kuhusu kuwawezesha kiuchumi wakazi wa Mafia, Samia alisema Ilani ya CCM inaeleza kwamba itatenga Sh. 1,000,000 katika kila kijiji cha Mafia ili kuwawezesha wananchi wake kununua vyombo vikubwa vya uvuvi. Awali, mgombea ubunge wa jimbo la Mafia, Mbaraka Dau, alisema pamoja na mafanikio yaliyotekelezwa visiwani hapo na mbunge anayemaliza muda wake Abdulkarim Shaha, bado jimbo hilo lina changamoto kadhaa.




CHANZO: NIPASHE





Wakaongeze Meli nyingine za ALOSCO ili kampuni ya silent ocean isafirishe mizigo mingi ya ccm pale lumumba
 
Sasa tshs 1,000,000 zitanunua vyombo gani vya kisasa kwa ajili ya uvuvi?
 
Aliahidi jk kashindwa magufuli na mv dar es salaam mbovu bil 8 hatuna tena imani na hawa watu.
 
walikuwa wakisema nchi haina hela, sasa hii hela ya hizo ahadi zilizoahidiwa zitapatikana wapi?
 
Back
Top Bottom