McLaren
JF-Expert Member
- Feb 19, 2025
- 889
- 2,863
Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Dkt Samia Suluhu Hassan, amewaambia wananchi wa Tabora kuwa atajenga barabara ya mzunguko yenye urefu wa kilomita 82 ili kupunguza msongamano mkoani humo.
Ameeleza hayo, leo Ijumaa Septemba 12,2025 wakati akihitimisha kampeni zake za mkoa wa Tabora kabla ya kuelekea mkoani Kigoma kuendelea kusaka kura kupitia mikutano ya hadhara iliyoandaliwa na CCM.
“Ninayo furaha kuwaeleza kuwa tunakuja na ujenzi wa barabara mpya ya mzunguko ya Tabora Mji. Tumeshafanya tathimini ya barabara hii itakayokuwa na urefu wa kilomita 82”
“Hii itahakikisha magari yote yasiyokuwa na ulazima wa kupita ndani ya mji wa Tabora, yanapita barabara ya nje kwenda yanakoelekea.Tunataka Tabora yenye historia kubwa, iwe na hadhi kubwa pia,”amesema Dkt Samia.
Ameeleza hayo, leo Ijumaa Septemba 12,2025 wakati akihitimisha kampeni zake za mkoa wa Tabora kabla ya kuelekea mkoani Kigoma kuendelea kusaka kura kupitia mikutano ya hadhara iliyoandaliwa na CCM.
“Ninayo furaha kuwaeleza kuwa tunakuja na ujenzi wa barabara mpya ya mzunguko ya Tabora Mji. Tumeshafanya tathimini ya barabara hii itakayokuwa na urefu wa kilomita 82”
“Hii itahakikisha magari yote yasiyokuwa na ulazima wa kupita ndani ya mji wa Tabora, yanapita barabara ya nje kwenda yanakoelekea.Tunataka Tabora yenye historia kubwa, iwe na hadhi kubwa pia,”amesema Dkt Samia.