GE2025 Samia: Nitajenga barabara ya mzunguko Tabora

GE2025 Samia: Nitajenga barabara ya mzunguko Tabora

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

McLaren

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2025
Posts
889
Reaction score
2,863
Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Dkt Samia Suluhu Hassan, amewaambia wananchi wa Tabora kuwa atajenga barabara ya mzunguko yenye urefu wa kilomita 82 ili kupunguza msongamano mkoani humo.

Ameeleza hayo, leo Ijumaa Septemba 12,2025 wakati akihitimisha kampeni zake za mkoa wa Tabora kabla ya kuelekea mkoani Kigoma kuendelea kusaka kura kupitia mikutano ya hadhara iliyoandaliwa na CCM.

“Ninayo furaha kuwaeleza kuwa tunakuja na ujenzi wa barabara mpya ya mzunguko ya Tabora Mji. Tumeshafanya tathimini ya barabara hii itakayokuwa na urefu wa kilomita 82”

“Hii itahakikisha magari yote yasiyokuwa na ulazima wa kupita ndani ya mji wa Tabora, yanapita barabara ya nje kwenda yanakoelekea.Tunataka Tabora yenye historia kubwa, iwe na hadhi kubwa pia,”amesema Dkt Samia.

 
Mkoa kwenye sensa ulikuwa watatu kwa idadi ya watu Tanzania Tabora Nimkoa Wakazi wake asilimia kubwa watumishi wa umma mkoa asilimia kuwa vijana wapo wengi hawana ajira

Kipaumbele kingekuwa kuwawezesha fursa kama viwanda viwepo vyakutosha kuliko haya mengine

Ukizungumzia ukuaji Tabora bado mkoa mdogo sana kimaendeleo ukifaninisha na Arusha Dodoma Mwanza Mbeya Morogoro hivyo Tabora kwanza maendeleo ya mtu mmoja mmoja ndiyo lakuzingatia zaid
 
Mkoa kwenye sensa ulikuwa watatu kwa idadi ya watu Tanzania Tabora Nimkoa Wakazi wake asilimia kubwa watumishi wa umma mkoa asilimia kuwa vijana wapo wengi hawana ajira
Kipaumbele kingekuwa kuwawezesha fursa kama viwanda viwepo vyakutosha kuliko haya mengine
Ukizungumzia ukuaji Tabora bado mkoa mdogo sana kimaendeleo ukifaninisha na Arusha Dodoma Mwanza Mbeya Morogoro hivyo Tabora kwanza maendeleo ya mtu mmoja mmoja ndiyo lakuzingatia zaid
uko sahihi kabisa mkuu...

na kama tabora hatustahiri kuwa na viwanda...

maana kiwanda cha tumbaku ni haki yetu na si morogoro...

basi barabara ya mbeya sikonge na ile ya kahama kaliua ni muhimu kuliko ring road...
 
uko sahihi kabisa mkuu...

na kama tabora hatustahiri kuwa na viwanda...

maana kiwanda cha tumbaku ni haki yetu na si morogoro...

basi barabara ya mbeya sikonge na ile ya kahama kaliua ni muhimu kuliko ring road...
Kabisa ile Sensa wangeitazama wangepata maswali mengi sana nawangeweza kuja na sera sahihi kusaidia wakazi wakoa wa TABORA
 
ujinga mwingine huo, kwa nini hiyo fedha asiisambaze mkoani tbr kujenga barbara wilayani na kuziunganisha kwanza? barabara nyingi za mzunguko kwenye mji zina faida gani kama wilaya zilizozunguka tope tupu ? ..
 
Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Dkt Samia Suluhu Hassan, amewaambia wananchi wa Tabora kuwa atajenga barabara ya mzunguko yenye urefu wa kilomita 82 ili kupunguza msongamano mkoani humo.

Ameeleza hayo, leo Ijumaa Septemba 12,2025 wakati akihitimisha kampeni zake za mkoa wa Tabora kabla ya kuelekea mkoani Kigoma kuendelea kusaka kura kupitia mikutano ya hadhara iliyoandaliwa na CCM.

“Ninayo furaha kuwaeleza kuwa tunakuja na ujenzi wa barabara mpya ya mzunguko ya Tabora Mji. Tumeshafanya tathimini ya barabara hii itakayokuwa na urefu wa kilomita 82”

“Hii itahakikisha magari yote yasiyokuwa na ulazima wa kupita ndani ya mji wa Tabora, yanapita barabara ya nje kwenda yanakoelekea.Tunataka Tabora yenye historia kubwa, iwe na hadhi kubwa pia,”amesema Dkt Samia.

Hiyo ndiyo njia za kuwadanganya watanzania maskini. Kwanini hiyo barabara asingejenga miaka 10 iliyopita???? Fala huyu. Tangu lini mipango ya serikali kama ipo inakufa kiongozi au chama kikishindwa? Hiyo barabara ambayo hata watu wa Tabora hawahitaji, itajengwa tu kwa pesa za kodi zetu, siyo kwa ujinga wa huyo Samia wenu. Amezoea kudanganya kila mahali huyu CHURA Kiziwi. Awadanganye mbwa wake akina Msigwa Gerson, Palamagamba na wenzake.
 
Fala huyu.
Mkuu, kulikuwa na ulazima gani wa kutukana? Kwani huwezi kueleza hoja zako bila kutukana? Kwani huwezi kupinga hoja zake bila kutukana? Wewe ukiitwa fala au msen&e urafurahi kweli? Ebu tutumieni uwezo wetu wa kufikiri kwa ufanisi.
 
Back
Top Bottom