Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa kivita mjini The Hague ICC imetakiwa kuchunguza madai ya mauaji ya watu wengi wakati wa msako mkali wa maandamano wakati wa uchaguzi nchini Tanzania mwezi uliopita.
Mawakili wa watu wanaodaiwa kuwa waathiriwa wanaoungwa mkono na Chama cha Wanasheria Duniani na Chama cha Wanasheria wa Madrid wamewasilisha hati kwa ICC inayoelezea madai ya mauaji hayo pamoja na utekaji nyara, utesaji na vitendo vingine vya vitisho dhidi ya upinzani wa kisiasa.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan alishinda uchaguzi wa Oktoba 29 kwa karibu asilimia 98 ya kura baada ya wapinzani wake wakuu kuzuiwa kuwania katika uchaguzi huo..
Maandamano hayo - ambayo ni ya hivi punde zaidi ya vijana wa Kiafrika waliokasirishwa na ukosefu wa ajira, kupanda kwa gharama na uhuru mdogo wa kisiasa - yanafuatia kile kinachoitwa maandamano ya Gen Z nchini Morocco na Madagascar, ambapo serikali iliondolewa na jeshi baada ya wiki kadhaa za machafuko.
Hati ya mahakama, iliowasilishwa pamoja na shirika la Intelwatch la Afrika Kusini tarehe 13 Novemba, inaitaka ICC kuzingatia uhalifu dhidi ya ubinadamu na kutoa hati za kukamatwa
Source: Jasusi TV
Mawakili wa watu wanaodaiwa kuwa waathiriwa wanaoungwa mkono na Chama cha Wanasheria Duniani na Chama cha Wanasheria wa Madrid wamewasilisha hati kwa ICC inayoelezea madai ya mauaji hayo pamoja na utekaji nyara, utesaji na vitendo vingine vya vitisho dhidi ya upinzani wa kisiasa.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan alishinda uchaguzi wa Oktoba 29 kwa karibu asilimia 98 ya kura baada ya wapinzani wake wakuu kuzuiwa kuwania katika uchaguzi huo..
Maandamano hayo - ambayo ni ya hivi punde zaidi ya vijana wa Kiafrika waliokasirishwa na ukosefu wa ajira, kupanda kwa gharama na uhuru mdogo wa kisiasa - yanafuatia kile kinachoitwa maandamano ya Gen Z nchini Morocco na Madagascar, ambapo serikali iliondolewa na jeshi baada ya wiki kadhaa za machafuko.
Hati ya mahakama, iliowasilishwa pamoja na shirika la Intelwatch la Afrika Kusini tarehe 13 Novemba, inaitaka ICC kuzingatia uhalifu dhidi ya ubinadamu na kutoa hati za kukamatwa