Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 16,301
- 33,750
Please stop this madness! Tanzania ni moja ya Nchi 25 masikini sana Duniani. Kuna kundi la G7 , G20 na Fast developing coountries! Tanzania kundi lake ni HIPC, mikutano ya HIPC ni kule Paris! Kenya si miongoni mwa Nchi 25 masikini. Nani anatuonea wivu au uadui!Umeongea mengi unachosahau ni ukweli kwamba kadri nchi inavyozidi kupiga hatua inajitengenezea uadui kutoka kwa maadui wa nchi za nje na humu humu.,
Ikiwa Wakenya ndio walikuja kuleta vurugu, mbona waliojaa mahabusu kutokana na MO29 ni Watanzania?Mahabusu duniani kote zinajaa raia wa nchi husika, hakuna jipya katika hilo.
Martha Karua, Willy Mutunga na Agatha walivunja sheria gani kuhudhuria kesi Mahakamani?Wakenya washenzi tu, walianza na Martha Karua na yule jamaa Robert, waliochangia kutuvuruga ni kundi hilo hilo moja.
Kuna sheria gani ya Nchi inayozuia Raia wa nje kutofika Mahakamani kusikiliza kesi?
Inawezekanaje miili ya Watu ipotee bila kuwafikia Wapendwa wao! Hili ni swali lilobaki hewani , bila majibu tunatibu vipi nafsi za Wapendwa zinazohangaika?Suala la kutafuta wapendwa limetokea mara moja tu katika historia ya Tanzania hutalisikia likitokea tena. Hutasikia tena raia wakipigwa risasi kama ilivyotokea tarehe 29 October.
With all due respect anachokifanya Nanauka ni nonsense! Ni upuuzi uliobobea. Ni parroting bila kutumia akili.Serikali imejishusha baada ya Waziri Nanauka anayeshughulikia masuala ya vijana kuanza kupeleka sera zake kwa makundi makubwa ya vijana, Waziri msikivu anayewakilisha serikali sikivu.
Nani amesema tatizo la vijana ni sera! CCM ipo madarakani miaka 64 eti baada ya MO29 ndio wanazungumzia sera. Kuna Ilani gani ya CCM iliyokosa sera za Vijana!
Nanauka aache kupoteza rasilimali za Umma! Msiwafanye Vijana ni majuha kwamba hawajui kinachoendelea.
Tatizo mnalijua; Utakaji, kupotezwa watu , mauaji yasiyo na maelezo, kuminywa Demokrasia, matumizi ya rasilimali za Umma. Msiwafanye Watanzania Majuha! ilifanyika hivyo, baada ya MO29 hamjajifunza?