The Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 10,986
- 13,482
Rais Daktari, profesa, al hajat, ustaadha, field marshal, generali, mtukufu, muadhamana nk nk nk Samia Suluhu Hassan asiposhinda urais kura ya wiki hii nitashangaa.
Kwanza, anagombea na chawa na si binadamu.
Pili, ni mtenda maajabu na miujiza kama kuweza kufuga na kuishi na machawa asikonde.
Tatu, timu yake ya uchafuzi, sorry, uchaguzi, ina kazi moja tu, kumtangaza tena akiwa ameshindishwa sorry ameshinda kwa kishindo.
Nne, anapondwa, sorry anapendwa sana kuliko hata Mungu mwenyewe.