Mama Samia ameshinda tuzo ya Tyrant of the Year. Watanzania wengi walimpigia kura. Walihamasishana mitandaoni na wakafanya kampeni kuhakikisha anashinda. Lakini ukweli ni huu: sidhani kama alipaswa kushinda tuzo hii, hata kama orodha ya madhambi yake haina mwisho. Ni kweli aliwateka nyara na kuwafunga wapinzani. Aliwaua waandamanaji. Aliyaruhusu polisi kupiga, kuua, kubaka na kuwatesa Watanzania wasio na hatia bila uwajibikaji wowote—kutaja machache tu. Kwa kweli, nilidhani Netanyahu angechukua ushindi huu moja kwa moja! Maana ni nini kinaweza kushinda mauaji ya kimbari? Naweza kumfikiria Donald Trump akiwa amekasirika kwa kutoshinda, licha ya juhudi zake zote (mbaya zaidi).
Soma Pia: Taasisi ya Kimataifa - Index On Censorship (IoC) yatoa majina 10 ya wanaowania Tuzo ya Dikteta wa mwaka (Tyrant of Year 2025)
Kama si matukio ya tarehe 29 Oktoba 2025, Samia asingekuwa hata kwenye orodha, hata kidogo. Hadi wakati huo, alikuwa bado yuko ligi ndogo, dikteta wa kujitakia tu. Lakini alifanya kile ambacho madikteta hufanya: alipuuza sauti ya wananchi waliotaka mageuzi ya uchaguzi kabla ya uchaguzi mkuu. Kuna methali ya Kiswahili isemayo, “Sikio la kufa halisikii dawa.” Samia alijizunguka na chawa (wapambe) na akaanza kuwakusanya na kuwakamata wapinzani.
Hakujali uchaguzi huru na wa haki, akaendelea na uchaguzi huku chama kikuu cha upinzani kikisusia. Akaendelea wakati kiongozi wa upinzani, Tundu Lissu, alipokuwa gerezani, na mgombea mwingine wa upinzani akiondolewa kwenye kinyang’anyiro kwa uamuzi wa mahakama wenye utata. Akaendelea huku waandamanaji kote nchini wakimiminika barabarani. Akaendelea huku kura zikichakachuliwa, na hatimaye akatangazwa mshindi wa urais kwa asilimia kubwa ya kushangaza—asilimia 98.
Uchaguzi mkuu wa 2025 ulikuwa uchaguzi wenye umwagaji damu mkubwa zaidi katika historia ya nchi. Polisi na vyombo vya ulinzi vya Tanzania waliwashambulia waandamanaji, raia waliokuwa wakipita, na watu wasio na hatia, wakiwapiga risasi hadharani. Vurugu za siku ya uchaguzi zilikuwa za kutisha, lakini ukatili uliofuata katika siku zilizofuata ulikuwa wa kuhuzunisha zaidi.
Nilisikia kwamba Mbeya na Mwanza, polisi waliingia ndani ya nyumba, wakawapanga vijana—watoto tu, kwa kweli—na kuwapiga risasi mmoja baada ya mwingine. Waliwaua watu ndani ya nyumba zao. Miili ilijazwa kwenye mochari na inadaiwa kuzikwa kwenye makaburi ya pamoja. Watu wengi hawakupata nafasi ya kuwaomboleza na kuwazika wapendwa wao. Walikamata washukiwa, wakawabaka na kuwatesa bila kufuata taratibu zozote za kisheria. Wakati huo wote, wananchi walifungiwa ndani ya nyumba zao bila mtandao wa intaneti wala upatikanaji wa habari za kuaminika (vyombo vya habari vya ndani havikuwa huru, na serikali ilizima intaneti).
Soma Pia: Taasisi ya Kimataifa - Index On Censorship (IoC) yatoa majina 10 ya wanaowania Tuzo ya Dikteta wa mwaka (Tyrant of Year 2025)
Kama si matukio ya tarehe 29 Oktoba 2025, Samia asingekuwa hata kwenye orodha, hata kidogo. Hadi wakati huo, alikuwa bado yuko ligi ndogo, dikteta wa kujitakia tu. Lakini alifanya kile ambacho madikteta hufanya: alipuuza sauti ya wananchi waliotaka mageuzi ya uchaguzi kabla ya uchaguzi mkuu. Kuna methali ya Kiswahili isemayo, “Sikio la kufa halisikii dawa.” Samia alijizunguka na chawa (wapambe) na akaanza kuwakusanya na kuwakamata wapinzani.
Hakujali uchaguzi huru na wa haki, akaendelea na uchaguzi huku chama kikuu cha upinzani kikisusia. Akaendelea wakati kiongozi wa upinzani, Tundu Lissu, alipokuwa gerezani, na mgombea mwingine wa upinzani akiondolewa kwenye kinyang’anyiro kwa uamuzi wa mahakama wenye utata. Akaendelea huku waandamanaji kote nchini wakimiminika barabarani. Akaendelea huku kura zikichakachuliwa, na hatimaye akatangazwa mshindi wa urais kwa asilimia kubwa ya kushangaza—asilimia 98.
Uchaguzi mkuu wa 2025 ulikuwa uchaguzi wenye umwagaji damu mkubwa zaidi katika historia ya nchi. Polisi na vyombo vya ulinzi vya Tanzania waliwashambulia waandamanaji, raia waliokuwa wakipita, na watu wasio na hatia, wakiwapiga risasi hadharani. Vurugu za siku ya uchaguzi zilikuwa za kutisha, lakini ukatili uliofuata katika siku zilizofuata ulikuwa wa kuhuzunisha zaidi.
Nilisikia kwamba Mbeya na Mwanza, polisi waliingia ndani ya nyumba, wakawapanga vijana—watoto tu, kwa kweli—na kuwapiga risasi mmoja baada ya mwingine. Waliwaua watu ndani ya nyumba zao. Miili ilijazwa kwenye mochari na inadaiwa kuzikwa kwenye makaburi ya pamoja. Watu wengi hawakupata nafasi ya kuwaomboleza na kuwazika wapendwa wao. Walikamata washukiwa, wakawabaka na kuwatesa bila kufuata taratibu zozote za kisheria. Wakati huo wote, wananchi walifungiwa ndani ya nyumba zao bila mtandao wa intaneti wala upatikanaji wa habari za kuaminika (vyombo vya habari vya ndani havikuwa huru, na serikali ilizima intaneti).