VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Mshambuliaji wa kitanzania anayecheza kwenye klabu ya TP Mazembe,Mbwana Samatha aliiweka timu yake ya Mazembe katika nafasi nzuri ya kutinga hatua ya nusu fainali ya Kombe la Mabingwa barani Afrika kwa kuipachikia bao la ugenini. Samatha,aliyeingia dakika ya 65 katika mechi hiyo baina ya Al Alhli na Mazembe iliyochezwa nchini Misri,alifunga bao hilo kwa kichwa akimalizia krosi safi ya Kasusula. Mazembe,hatahivyo,ililala kwa mabao 2-1. Mechi ya marudio itapigwa juma lijalo nchini DRC-Kongo.