GE2025 Salum Kinyori 'Kibakuli' ajitosa kugombea Ubunge katika Jimbo la Handeni Mjini

GE2025 Salum Kinyori 'Kibakuli' ajitosa kugombea Ubunge katika Jimbo la Handeni Mjini

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
3,177
Reaction score
7,472
WhatsApp Image 2025-06-30 at 19.11.14_dad08fd3.jpg
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mdau wa maendeleo Salum Kinyori 'Kibakuli', leo Juni 30, 2025 amechukua fomu ya kugombea ubunge Jimbo la Handeni mjini Mkoani Tanga.

Salum ambaye ni mdau wa Maendeleo na msomi aliyebobea kwenye fani ya uchumi na mfanyabiashara mbobevu amechukua fomu hiyo katika Ofisi ya CCM Wilaya ya Handeni mjini lengo likiwa ni kuleta mabadiliko chanya na mwanga mpya wa maendeleo ya Jimbo hilo.

Hatua hiyo ya Salum kuingia rasmi katika mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM imeibua msisimko mpya Kwa wakazi wa Handeni Mjini hasa ukizingatia historia yake ya kiongozi na ufanisi alionyesha katika nyanja mbali mbali za maendeleo katika Jimbo hilo.
WhatsApp Image 2025-06-30 at 19.11.15_4583a49d.jpg

WhatsApp Image 2025-06-30 at 19.11.14_3bfb8f1f.jpg
 
Back
Top Bottom