PreGE2025 Salma Kikwete: Tumejipanga kuiomba serikali pesa za kukarabati soko la samaki kwenye kijiji cha Mchinga

PreGE2025 Salma Kikwete: Tumejipanga kuiomba serikali pesa za kukarabati soko la samaki kwenye kijiji cha Mchinga

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,564
Reaction score
2,483
"Jana tarehe 16/03/2025 nilipata wasaa wa kutembelea soko la Samaki la katika Kijiji Cha Mchinga II kilichopo katika Jimbo la Mchinga na kujionea shughuli za biashara ya Samaki zinavyofanyika.

Hivi karibuni, soko hili limepatwa na kadhia ya Mafuriko yaliyopelekea Miundombinu yake kubomoka kutokana na Mvua kubwa zilizonyesha usiku wa kuamkia tarehe 11/03/2025.

Tumejipanga kufanya jitihada za makusudi, kuiomba Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, kutusaidia pesa kwa ajili ya kufanya marekebisho ya soko hili. Soko hili limekuwa na Mchango mkubwa katika kuongeza Mapato ya Halmashauri na kurahisisha shughuli za kibiashara kwa Wananchi wa Jimbo la Mchinga na Wakazi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi." - Salma Kikwete, Mbunge Jimbo la Mchinga

Soma pia: Pre GE2025 Miradi kuelekea Uchaguzi Mkuu: Mhandisi Kundo akagua mradi wa maji unaonufaisha zaidi ya wakazi 200,000 Chalinze
 
Sijaona mwanamke mwenye tamaa na asiyeridhika kama huyu.

Hivi ile proposal yake ya wake wa viongozi kulipwa mshahara bunge la manyani walipitisha?
 
Back
Top Bottom