Salary Slip zero shillings

mchepuko

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2014
Posts
1,192
Reaction score
1,418
Huu mkopo umenitesa jamani! tangu 2012 nilikopa kama 15m hamna cha maana nilichofanya zaidi ya kuishia kununua gari kuu kuu na kiwanja feki kilicho na kesi hadi leo.

Nimekoma nimekoma kukopa bila malengo maalum,lakini hata kama nna malengo maalum basi umakini unahitajika kuyafikia malengo hayo nimejifunza aisee hayo makato sasa uwii.

Kwa wale msiokopesheka mpite hivi.

hata hivyo DENI LIMEISHA MWEZI HUU...GLORY TO GOD..NILIKUA NIFE MWENZENU
 
hashahahah dah umenifanya nicheke ahahahahahahah yelewoooo
 
Tafuta bwana akugharamie basi hapa mjini
 
Hahahahahahaaaaaaaaaaaaa nacheka kama inafurahisha vile kunbe inanikumbusha machungu ya mkopo wangu nilomaliza last year nilisota sana asee nimekoma sirudii tena?
 
hata me nimekoma marejesho noma had nakonda
 
Haaaaahaaaa habari ya mkopo uisikie tu! Mm nilipokuwa nakatwa niliona kama naibiwa. Nimejifunza nikitaka kukopa tena najipanga kwanza nini nitafanya na tena kiwe kinaingiza zaidi ya makato ninayokatwa kwa mwezi kila mwezi, la sivo waweza kuishia kuwa unapiga kelele kila siku za mshahara hautoshi, kumbe salary slip ni majanga!
 
mnanitisha mie nimetoka kusaini mkataba wa mkopo leo mchana! sijawai kukopa
 
mnanitisha mie nimetoka kusaini mkataba wa mkopo leo mchana! sijawai kukopa

kama una malengo na huo mkopo sawa.....hakikisha unafanyia kitu ambacho hata kama utakuwa unakatwa .....ukikiona kile kitu machungu yanapungua.....
 
Mwaka jana nilikopa hela nikawa nakatwa miezi mitano salary yote nilijikomit ili nimalize haraka sababu sikua na kazi na mshahara. Hela ya matumizi nauza kuku zangu life linasonga coz sina mke wala dem. Mwaka huu nimedhamiria kujenga na kwa mazoea ya kutotumia hela nilojenga salary ya january mpaka march sijaigusa. Nilipokopa nilinunua kiwanja na sasa nawaza kujenga kibanda cha room na sebule. Nasikia maisha ya kuoa magumu sana sasa sitaki nifike huko niwe sijajipanga na kitu hata kimoja.
 
Mkuu,

Mwajiri wakonae ni feki kabisa yaani haruhusiwi kukata ubalki na zero hata kama nikampuniyako......anatakiwa akuache na robo tatu yamshahara wako
 
Pole Sana sasa ukome kukopa ili uweke heshima corner bar
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…