Salamu za Edward Lowassa kwa Taifa Stars

Salamu za Edward Lowassa kwa Taifa Stars

EmmaGMangwela

Senior Member
Joined
May 11, 2015
Posts
139
Reaction score
54
Baada ya mikutano yangu mitatu ya Kigoma Kaskazini, Kigoma Kusini na Kigoma Mjini, napenda kutumia nafasi hii kuwatakia kila la heri vijana wetu wa Timu ya Taifa Stars kwenye mechi yao ya kwanza ya kuwania kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) 2017 watakapokuwa wakiuamana vikali na Timu ya Taifa ya Nigeria (Super Eagles).

Napenda kuwatia moyo vijana wetu hawa kuwa watambue kwa dhati kabisa kuwa wanabeba matumaini yetu sote kama taifa katika kuhakikisha kuwa Tanzania inapunguza ile dhana ya kwamba 'kila mmoja anaweza kujifunza kunyoa kupitia kichwa chetu' linapokuja suala la michezo, hususan mpira wa miguu kwa maudhui ya hapa. Ushindi watakaoupata dhidi ya Wanaigeria hao, ni sifa kwa Watanzania wote.

Salaam zangu hizi za kuitakia kila la heri Taifa Stars pia ziende kwa watu wote wanaohusika katika kuwanoa vijana hao kuhakikisha Taifa ndilo linashinda, nikianzia na makocha, madaktari, halikadhalika uongozi wa Shirikisho la Michezo nchini (TFF).

Aidha ningependa kumalizia salaam hizo kwa kuzungumzia suala moja la kisera kuhusu michezo. Watanzania wakinichagua kuwa rais wao hapo Oktoba 25, mwaka huu na Mwenyezi Mungu akaridhia, tunajiandaa kuwa serikali itakayokuwa rafiki wa micehzo na sanaa.

Mojawapo ya masuala ambayo nitayapatia uzito katika eneo hili ni kujenga taasisi na vyuo vya kukuza michezo ili kuhakikisha kuwa ndani ya miaka mitano Tanzania inashiriki kwa ushindi katika mashindano ya kimataifa.
 
Imekaa vizuri. Tunaiombea mema timu yetu pendwa.
 
Mungu ibariki Taifa Stars,Mungu mbariki raisi wetu ajaye..kipenzi cha watanzania..mh.Edward Ngoyai Lowasa.
 
Vijana chezeni mpira kwa moyo wa kivita.Achaneni na sifa za majukwaa Bali kelele zile ziwe chachu ya kukumbusha kiu ya watanzania.ushindi mwema vijana
 
Mbona huko hajamwaga mihela kama kwingine, kaishiwa!!?
 
Safi sana,hizi ni kauli thabiti!hembu wekeni ile video mkulu akipapasa totoz siku ile ya wasanii feki mlimani city
 
Ni mtizamo wake tu kama mtz

Humu jf nimegundua Id ambazo ni kongwe nyingi hazimtetei ila kuna baadhi zinamtetea kwa maslahi yao zilizojaa mpya tu

Vijana nendeni field sio kwenye mitandao hapa ni kakikundi kadogo sana ka watu

Hii ndo siasa za tz na watz ni unafiki na wanafiki tu mwanzo mwisho
 
Ni mechi ya kwanza au ya pili ktk kufuzu? ile tuliyocheza na Mafirauni tukafungwa ilikua ktk ushiriki upi muwe makini
 
Ni mtizamo wake tu kama mtz

Humu jf nimegundua Id ambazo ni kongwe nyingi hazimtetei ila kuna baadhi zinamtetea kwa maslahi yao zilizojaa mpya tu

Vijana nendeni field sio kwenye mitandao hapa ni kakikundi kadogo sana ka watu

Hii ndo siasa za tz na watz ni unafiki na wanafiki tu mwanzo mwisho

Field ipi unayoengea ww na id zipi kongwe mbona huku mitaani kila mtu Edward au ww ndio huendi field
 
CCM tokaaaaaaa,lowasa atoooooshaaaaaaaaaa.as ante muheshimiwa raisiiiiiiiiiii
 
Aliwahi kukupatia hela? Mpaka useme kaishiwa? Acha kuaminisha vibaya watu. Mzee wa watu atashinda kwa propoganda zenu
 
Kila la Heri Taifa stars ushindi ni muhimu .Kila la Heri Lowassa ushindi ni neno sahihi kwako na wanamabadiliko
 
Back
Top Bottom