Sakata la Zakaria Hans Pope na CAG

Aug 20, 2016
9
2
Matumaini yangu kuwa hamjambo na wazima wa afya, binafsi naendelea vizuri alhamdulillah maisha kimtindo yanakwenda japo twazidi kuzisoma namba.

Nimeona nitoe maoni yangu kwenu juu ya masuala yanayoendela ndani ya nchi yetu ya vi-wonder

Nikianza na sakata la Zakaria Hans Pope kwa magari yake kukamatwa, binafsi ningependa kuwapongeza TRA kwa kazi nzuri sana wanayofanya ya kukusanya mapato.

Kwa mujibu wa taarifa zinadai kwamba magari hayo ambayo yamebeba mafuta ya muwako, yamekaa mpakani Tunduma kuanzia Tarehe 19/01/2017 mpaka hii leo, ukipiga hesabu ni takribani miezi miwili.a

Magari yaliyokamatwa ni takribani 16 ambayo yote yapo chini ya mmiliki mmoja ambaye ni Zakaria Hans pope, kama hiyo haitoshi magari hayo yame-pack sambamba kabisa na magari mengine.

Kitendo kinachoelezwa kwamba huenda kikasababisha hatari ya mlipuko, rai yangu kwa serikiali ni kuitaka ifanye kazi kwa ufanisi, uweledi na bila kuingiza visasi au uhasama wa aina yoyote.

Unaambiwa kabla ya hapo, TRA walikwenda kukagua ofisi za malori ya Hans Pope mwishoni mwa mwaka jana na kwa habari zilizochini ya kapeti ni kwamba kipindi MKULU akiwa WAZIRI walipishana kauli na kamanda Z.H.POPE.


KWA UPANDE WA PROF. ASSAD

Kusema ukweli nikijaribu kuangalia mwenendo wa nchi yetu tunapotaka kwenda na mienendo yake ama kwa hakika sipati jibu, nahisi ni kama mchezo wa karata.

Haiwezekana kiranja mkuu wa fedha za serikali (CAG) Prof.Assad akapunguziwa budget ya ofisi yake kwa takribani asilimia 40, mpaka kufikia hatua ya yeye kusema kwamba ukata umeikumba ofisi zake.

Hivi hizi pesa tunazoziita za miradi ya maendeleo ambazo zinatoka kwetu wavuja jasho kwa kubanwa kila kona ya kodi, Ni nani atakayeweza kuzikagua kama zinafanya kazi yake ipasavyo kama sio huyu CAG?

Kitendo cha ofisi ya CAG kufinywa budget yake kinaonyesha wazi kabisa serikali yetu inachokifanya sio kutufikisha kwenye Tanzania tunayoitaka au ambayo tuliahidiwa wakati wa kampeni.

Rai yangu kwa Taifa zima ni kuingia kwenye maombi ya nguvu kwa waumini wa dini zote, kuliombea hili Taifa na kuvunja roho mbaya, za chuki, visasi na kiburi cha hali ya juu kwa viongozi wanaotuongoza.


 
Eee mwenyezi mungu wape haki walio serikalini na walio nje ya serikali..kila MTU apate haki yake...
 
Mod ataufuta huu uzi muda si mrefu
Nikweli Hansi anakomolewa bila sababu ya msingi the same na manji
Utawala wa visasi chuki ubaguzi dhuluma na uzandiki ni hatari kwa taifa
Tuliokuwa tunayasikia Rwanda na Burundi sasa tunayaonja
 
Pale mlimani City kwenye harambee ya kuchangia UKAWA chini ya mgombea uraisi- ndugu Lowassa,Hans Pope lichangia 20mln,ikiwa tu mkata umeme anakataza Lema asijuliwe hali gerezani na wabunge wenzie,sishangai visasi hivi!!
 
Daaaa....ila huyu jamaa lile ghorofa analojenga pale Nyumbani kwao Iringa (opposite na hotel ya Mr au mkabala na beki ya CRDB na ofisi za posts mkoa Iringa) , aiseee ni sheeda sidhan kama kwa sasa kuna mjengo kama huo kwa wanyalu aiseee. Boongeee la ghorofa...TRA mchunguzeni tu kwa kina maana siamini kama ni simba na masuala ya usafirishaji yanaweza mpatia Pesa yote hiyo.
 
AaAHAAA WA NYUMBANI HUYU NDO WANAMFANYIA HIVI HATA SIMBA IMEGUSWA ...MEEEEESSSS
 
Habari hazieleweki kabisa mara hans poppe mara prefosa assad yaani fupi fupi umeunganisha umekuwa kama mange mkuu
 
Mod ataufuta huu uzi muda si mrefu
Nikweli Hansi anakomolewa bila sababu ya msingi the same na manji
Utawala wa visasi chuki ubaguzi dhuluma na uzandiki ni hatari kwa taifa
Tuliokuwa tunayasikia Rwanda na Burundi sasa tunayaonja
Leo kwa sababu kaguswa na Hans ndiyo mmeanza kumtetea Manji?
 
Daaaa....ila huyu jamaa lile ghorofa analojenga pale Nyumbani kwao Iringa (opposite na hotel ya Mr au mkabala na beki ya CRDB na ofisi za posts mkoa Iringa) , aiseee ni sheeda sidhan kama kwa sasa kuna mjengo kama huo kwa wanyalu aiseee. Boongeee la ghorofa...TRA mchunguzeni tu kwa kina maana siamini kama ni simba na masuala ya usafirishaji yanaweza mpatia Pesa yote hiyo.
Mkuu Zacharia Hans Poppe ana Truck zaidi ya 100 Nina kija truck changu kibovu bovu zamani alikuwa ananipatia order ila alipobadilisha utaratibu wa mirage na mafuta kujitegemea nimemkimbia ila hiyo ghorofa na kipato anachopata naona alitakiwa awe Nazi hata 4 Hera nyingi anapoteza Simba
 
Mkuu Zacharia Hans Poppe ana Truck zaidi ya 100 Nina kija truck changu kibovu bovu zamani alikuwa ananipatia order ila alipobadilisha utaratibu wa mirage na mafuta kujitegemea nimemkimbia ila hiyo ghorofa na kipato anachopata naona alitakiwa awe Nazi hata 4 Hera nyingi anapoteza Simba
Duuu..kumbe ni bourgeoisie Mkubwa sana huyu jamaa zakaria hanspope , by the way ngoja akomae na CAG prof Asad.
 
Daaaa....ila huyu jamaa lile ghorofa analojenga pale Nyumbani kwao Iringa (opposite na hotel ya Mr au mkabala na beki ya CRDB na ofisi za posts mkoa Iringa) , aiseee ni sheeda sidhan kama kwa sasa kuna mjengo kama huo kwa wanyalu aiseee. Boongeee la ghorofa...TRA mchunguzeni tu kwa kina maana siamini kama ni simba na masuala ya usafirishaji yanaweza mpatia Pesa yote hiyo.
Ana uwezo hta wa kumjenga mama yako sio ghorofa tu
 
Back
Top Bottom