Naomba anaefahamu ni lini sasa ving'amuzi vya azam,zuku na DSTV vitarejesha channel za bure ukizingatia kwamba channel hizo zimeondolewa kabisa ambapo hata ukilipia kifurushi channel hazifunguliwi,kuoneshwa basi bure kama ambavyo sheria inawataka hazioneshwi.Kweli serikali imeridhia sasa wananchi wanyonge tukose habari jambo ambalo ni razima kwa kila mtanzania?.Mf:king'amuzi cha zuku kifurushi kikiisha wao wanakata hadi TBC ambayo ilikua FTA kwa ving'amuzi vingine sasa mim nashindwa kuelewa hizo leseni ambazo zinawataka kurusha local channels bure kwamba zilitolewa kwa upendeleo?
