Asalaam Aleikum - Amani iwe juu yenu.
Kwa muda nimejaribu sana kujizuia kuandika lolote juu ya MKASA wa Kiongozi balozi mstaafu Humphrey Polepole. Mengi yamesemwa kwa Ubaya na Uzuri ili mradi kuridhisha nafsi na malengo ya wasemaji. Lakini UKWELI wa yote unabakia kuwa fumbo la Mbayuwayu.
Mimi nina maswala machache ya Kiutu uzima yanayonitia wasiwasi juu ya Taifa langu, hivyo naomba zaidi Hekima na Busara itumike kwani tunakoelekea sii shwari hata kidogo iwe siku ya Uchaguzi ama baada ya Uchaguzi huu.
Hoja ya kwanza ni pale napowasikia baadhi ya watu Wanasema Polepole kajiteka maana hayupo nchini yuko nje ya nchi hivyo hii ni sinema tu. Yawezekana kweli lakini swali linakuja hivi.
Kama Polepole alikuwa nje ya nchi kwa nini wale wasojulikana walivamia nyumba ya dada yake Wakamteka, wakampiga wakitaka awambie Polepole kajificha wapi? Kulikuwa na umuhimu wowote wa kuvamia nyumba ya dada yake ikiwa wanajua Polepole hayupo nchini? Laa sivyo basi dadake na Polepole wote waliongopa kuvamiwa haikutokea.
Hoja nyingine ni kwamba ikiwa Polepole ni mkosa kumsema vibaya rais wa nchi. Je, kwa kufanya hivyo tulivyomsikia ni 1. kosa la jinai? ama ni 2. Uthubutu wa muumbuzi katika Uzalendo kwa nchi yake (Whistleblower).
Tafakari yangu - katika hali inayoendelea sasa hivi - Je, ni nani haswa anayetakiwa kusema mabaya ya rais ama kiongozi kama itatokea mbeleni tumepata rais fisadi, dikteta, muuaji, na dhalimu? Nani baina yetu sote atakaye thubutu kumfunga Paka kengele? Kesho yetu sote imekaaje...
Ya mwisho kabisa ni kwa wale wanaosema Polepole alihudumu ndani ya Serikali ya Magufuli ambayo ilifanya utekaji na mauaji mengi kwa nini aje leo kuikosoa Serikali hii? Kwa nini asiseme haya wakati ule akiwa madarakani.
Ukweli ni kwamba Polepole alikuwa
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi sio Serikali, na baadae alihudumu kama Mbunge wa kuteuliwa na rais. Na hoja zake zilijikita zaidi kwenye Uongozi wa Chama chake na kukataa Uteuzi wa Mama Samia kuendelea kugombea Urais kwa sababu alizotaja yeye. Haya yote ni maswala ya ndani ya Chama cha Mapinduzi sio Serikali ya JMT, ni bahati mbaya tu kwamba Mwenyekiti wa CCM ndiye rais wa nchi.
Binafsi, nachukulia tuhumu hizo kwa uzito mkubwa sana na nilitegemea kati ya Rostam, rais Mstaafu Jakaya Kikwete, na wengineo walojumuishwa katika kundi hili akiliita WAHUNI kufungua mashtaka mahakamani dhidi ya Humphrey Polepole! Au laa sivyo maswala haya yangemalizwa ndani ya vikao vya Chama - HAIKUTOKEA. - Najiuliza kwa nini?
Siamini katika Uzushi na tungo za kuharibu twasira na hadhi za viongozi wetu lakini pia siamini katika Utekaji na mateso wanayopitia baadhi wananchi kwa sababu wametoa tuhuma nzito dhidi ya Viongozi wa nchi.
Kwa hoja na maandishi haya, nimetumia Uhuru wangu wa fikra kutoa dukuduku langu juu ya hofu ilotanda nchini kuelekea Uchaguzi Mkuu hiyo tarehe 29 October. Siwezi kuweka shaka juu ya matukio na siwezi kaa kimya kwa sababu ya woga!
Tukipoteza HAKI zetu Kikatiba, basi hatutakuwa na Tanzania wanayodai ni hii hii moja. Hiyo Tanzania moja ina upande mmoja tu wa HAKI kwa wote - HAKUNA ALOKUWA JUU YA SHERIA.
Kwa muda nimejaribu sana kujizuia kuandika lolote juu ya MKASA wa Kiongozi balozi mstaafu Humphrey Polepole. Mengi yamesemwa kwa Ubaya na Uzuri ili mradi kuridhisha nafsi na malengo ya wasemaji. Lakini UKWELI wa yote unabakia kuwa fumbo la Mbayuwayu.
Mimi nina maswala machache ya Kiutu uzima yanayonitia wasiwasi juu ya Taifa langu, hivyo naomba zaidi Hekima na Busara itumike kwani tunakoelekea sii shwari hata kidogo iwe siku ya Uchaguzi ama baada ya Uchaguzi huu.
Hoja ya kwanza ni pale napowasikia baadhi ya watu Wanasema Polepole kajiteka maana hayupo nchini yuko nje ya nchi hivyo hii ni sinema tu. Yawezekana kweli lakini swali linakuja hivi.
Kama Polepole alikuwa nje ya nchi kwa nini wale wasojulikana walivamia nyumba ya dada yake Wakamteka, wakampiga wakitaka awambie Polepole kajificha wapi? Kulikuwa na umuhimu wowote wa kuvamia nyumba ya dada yake ikiwa wanajua Polepole hayupo nchini? Laa sivyo basi dadake na Polepole wote waliongopa kuvamiwa haikutokea.
Hoja nyingine ni kwamba ikiwa Polepole ni mkosa kumsema vibaya rais wa nchi. Je, kwa kufanya hivyo tulivyomsikia ni 1. kosa la jinai? ama ni 2. Uthubutu wa muumbuzi katika Uzalendo kwa nchi yake (Whistleblower).
Tafakari yangu - katika hali inayoendelea sasa hivi - Je, ni nani haswa anayetakiwa kusema mabaya ya rais ama kiongozi kama itatokea mbeleni tumepata rais fisadi, dikteta, muuaji, na dhalimu? Nani baina yetu sote atakaye thubutu kumfunga Paka kengele? Kesho yetu sote imekaaje...
Ya mwisho kabisa ni kwa wale wanaosema Polepole alihudumu ndani ya Serikali ya Magufuli ambayo ilifanya utekaji na mauaji mengi kwa nini aje leo kuikosoa Serikali hii? Kwa nini asiseme haya wakati ule akiwa madarakani.
Ukweli ni kwamba Polepole alikuwa
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi sio Serikali, na baadae alihudumu kama Mbunge wa kuteuliwa na rais. Na hoja zake zilijikita zaidi kwenye Uongozi wa Chama chake na kukataa Uteuzi wa Mama Samia kuendelea kugombea Urais kwa sababu alizotaja yeye. Haya yote ni maswala ya ndani ya Chama cha Mapinduzi sio Serikali ya JMT, ni bahati mbaya tu kwamba Mwenyekiti wa CCM ndiye rais wa nchi.
Binafsi, nachukulia tuhumu hizo kwa uzito mkubwa sana na nilitegemea kati ya Rostam, rais Mstaafu Jakaya Kikwete, na wengineo walojumuishwa katika kundi hili akiliita WAHUNI kufungua mashtaka mahakamani dhidi ya Humphrey Polepole! Au laa sivyo maswala haya yangemalizwa ndani ya vikao vya Chama - HAIKUTOKEA. - Najiuliza kwa nini?
Siamini katika Uzushi na tungo za kuharibu twasira na hadhi za viongozi wetu lakini pia siamini katika Utekaji na mateso wanayopitia baadhi wananchi kwa sababu wametoa tuhuma nzito dhidi ya Viongozi wa nchi.
Kwa hoja na maandishi haya, nimetumia Uhuru wangu wa fikra kutoa dukuduku langu juu ya hofu ilotanda nchini kuelekea Uchaguzi Mkuu hiyo tarehe 29 October. Siwezi kuweka shaka juu ya matukio na siwezi kaa kimya kwa sababu ya woga!
Tukipoteza HAKI zetu Kikatiba, basi hatutakuwa na Tanzania wanayodai ni hii hii moja. Hiyo Tanzania moja ina upande mmoja tu wa HAKI kwa wote - HAKUNA ALOKUWA JUU YA SHERIA.