Mwenyewe umesema huku kwetu hakuna kufuata sheria ni kuoneana tu, likely na Lissu anatafutiwa sababu ya kufungwa.Hakuna mpango wowote hapo, lissu amekosa jukwaa sasa ameamua kutafuta kwa njia nyingine. Tatizo lake anafikiri serikali ya sasa ni ile iliyo pita, kama atakutwa na kosa basi atahukumiwa na hakuna wa kufanya lolote. Tatizo la watanzania wengi wamesahau kuwa sisi tuko Africa na africa mambo ni tofauti na kwa wazungu. Huku kwetu hakuna kufata sheria, sio serikali wala upinzani, wote wanafata wanayo taka wao. Chukua mfano wa hii movie ya Lissu, anacho pigania ni nini hasa?
Na akiendelea hivi basi ujue anako elekea ni magereza. Hovi weee unafikiri Lissu akifungwa nini kitatokea? Nchi itachafuka au wazungu watakata misaada? Ukweli ni kuwa maisha yataendelea huku uraiani kama kawaida na atasahulika haraka sana.Mwenyewe umesema huku kwetu hakuna kufuata sheria ni kuoneana tu, likely na Lissu anatafutiwa sababu ya kufungwa.
Mimi sikubali atusemee Watanzania.Mimi nakubali atusemee Watanzania
Sasa hiyo mikutano na maandamano inazuiaje maendeleo? Walioweka sheria na taratibu hawakujua kuwa kuna maendeleo? Na mbona yeye rais anafanya mikutano na kuingiza wanachama katika CCM?Hakuna sharia hapa yeye anataka maendeleo.
Hakuna kitu kama hicho kunapokuwapo na katiba na uchaguzi wa kidemokrasia. Hicho huwapo pale nchi inapopinduiwa ikiwa katika kipindi cha mpito. Hicho iliwahi kuwepo hapa baada ya muungano wakati katiba ikiandaliwa. Baada ya hapo raisi akiapa kufuata katiba na akienda kinyume cha hapo hafai kuwa rais hata baba wa taifa alishawahi kusema sifa ya kwanza ya rais ni kufuata katiba aliyoapa kuongoza nchi. Alisema kinyume cha hapo ni uhuni. Rejea wakati ule wa Mwingi kwenye sakata la IOC na vugu vugu la kurudishwa kwa Tanganyika. Katiba ndio sheria mama mkuu na hakuna presidential decree Tanzania kwa sasa labda uniambie mabavu au hicho wanachomshtakia Lissu kinachohusiana na mambo ya uchwara! Ndio maana wapinzani wanatumia katiba na sheria zinazotambua shughuli zao lakini rais anasema tu mimi sijaribiwi mara oh mimi ndiye rais kana kwamba kuna mtu kasema yeye sio rais. Sasa kwa maelekezo ya rais vyama visivyokuwa na wabunge na madiwani lakini vina usajili wa kudumu visifanye mkutano? Na chama nini? Si watu? Sasa utaendeshaje chama bila kukutana na wanachama na kutafuta wanachama wapya? Si hata madhehebu ya dini yanafanya hivyo hivyo ndio maana unaona mihadhara na mikutano ya kidini ya hadhara na kupitia vyombo vya habari. Yote hiyo ni kuhubiri imani yao na kupata waumini au wafuasi wapya ili kukua na kujiimarisha vinginevyo basi baada ya watu kuokoka kungekuwa hakuna haja ya kuendelea na mahubiri au basi watu wangesali mara moja au mbili kwa mwaka. Ukweli ni kuwa katika mahali ambapo JPM anaiharibu CV yake yeye mwenyewe ni hapa kwenye kupiga marufuku mkutano na maandamano ya vyama vya siasa wakati yeye na CCM yake wakifanya na vile kuwapangia pa kufanya hii inabomoa umoja wa kitaifa. Vyama vimesajiliwa kitaifa na vinapaswa kufanya kazi hivyo yeye anasema wafanye tu kule walikochaguliwa. Analeta utengano badala ya utangamano! Mr. President, please rethink!Kuna kitu kinaitwa Presidential Decree.
Ndio yale matamko au ndio nn?! Maanake sisi watu wa sadam usein wa libya kidhungu kinatupa shida.Kuna kitu kinaitwa Presidential Decree.
Una uhakika gani wewe pia haupo?Sema mawazo yako inatosha, sio kuchanganya watanzania wote.
Kwa jinsi ilivyo badala ya kucheza itachezewa sana kwakuwa yenyewe haina sheria za kuhalalisha hayo inayoyafanya wakati mwenzao ana sheria na kanuni zinazoruhusu mikutano na maandamano kikatiba na sheria ya vyama vya siasaSerikali inacheza mziki wa Lissu
Nina wasiwasi jengo lako litakuwa limesingirwa na jeshi muda huu. Kutumia hilo neno ni uhaini mkuu.Nataka niwe mwana JF uchwara
Uliambiwa Sadam Hussein ni wa KuwaitNdio yale matamko au ndio nn?! Maanake sisi watu wa sadam usein wa libya kidhungu kinatupa shida.
Kwa kumtaja tu inadhirisha ni kiki tosha.Huyo Lissu ana kiki gani?
Asante kwa kunikumbusha mkuu.. na yule jirani yetu wa libya si wa iraq pia?!Uliambiwa Sadam Hussein ni wa Kuwait
Mbona unaleta vijimaswali visivyo na mbele wala nyuma?Una uhakika gani wewe pia haupo?
Libya ya Iraq au kuwait mkuu.Wapuuzi wenzako walishashituka kuwa walifanya kosa kumuondoa Gadaf bado wewe tu. yaelekea kwako Libya ya sasa ni Bora kuliko ile ya gadaf! kweli kwenye dunia hii kuna mataahira mengi sana.
Kivipi sasa mkuu.Mbona unaleta vijimaswali visivyo na mbele wala nyuma?
ni ngumu kujadili na taahira.Libya ya Iraq au kuwait mkuu.
Alifungwa Shekhe Ponda Issa Ponda waliojifanya want mihemko naye wakafyata mikia hapo hamna kitu anaweza kufungwa na wasifanye loloteTumeshuhudia siku za hivi karibuni polisi imekuwa ikihangaika na matamshi ya Mbunge wa Singida Mashariki Mh. Tundu Lissu kuwa rais Magufuli ni "dikteta uchwara".
Hebu tujiulize nini hasa lengo la hili sakata kwa pande zote zinazovutana.
Haiwezekani mtu unakamatwa/shitakiwa kwa kosa fulani halafu unarudi kutenda kosa lilelile tena nje tu ya jengo la mahakama.
Binafsi naona ni kama kuna mtego fulani kwa chama tawala utakaohitimishwa September 1, chini ya Operation UKUTA.
Nafikiri nia hasa ya Chadema ni ama Lissu afungwe au awekwe ndani ipatikane sababu ya kufanikisha operation hiyo.
Lengo lingine nafikiri ni kukiweka chama kwenye headline kwa muda mrefu na kufifisha ziara za mtukufu rais zinazoendelea. Kumbuka kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Mh. Mbowe alisema wanauwezo wa kufanya siasa ndani na nje ya bunge.
Lengo lingine "nafikiri" ni mkakati wa kumuandaa mtu atakayeaminiwa na kuonewa huruma na jamii (Mandela style) ili labda baadaye aje kugombea cheo kikubwa ndani au nje ya chama.
Lengo lingine nafikiri ni kuionyesha dunia na watanzania kwa ujumla kuwa serikali ya Magufuli ni ya kidikteta inayovunja katiba yake ili kuthibitisha maneno ambayo yamekuwa yakisemwa na chama hicho.
Serikali ijue Chadema ni chama kikubwa kina uzoefu mkubwa kina wanasiasa wazoefu na wakongwe, hivyo kina mikakati yake na mbinu mbalimbali za kujiimarisha. Hivyo, serikali isilichukulie sakata la Lissu kama jambo dogo, should handle this issue with care.
Kumbuka moto huanza na cheche moja baadaye husambaa na kuunguza msitu mzima.
Haya ni mawazo yangu binafsi.
Yaani nimeahidi mbele ya Mungu sitaki tens kusikiliza hotuba zake wala kuangalia TV kwa kipindi chote atalacho kaa madarakani kwani nafsi yangu imekereka kupita Maelezo.Hivi anadhani Nchi hii Ni take kama familia yake?Dikteta anajiamini kupita kawaida, anadhani watanzania tunamuona malaika kumbe tunamuona kichekesho
We mwenyewe umeshindwa kuvumilia kukaa kimya! Lisu ni kama maji, usipoyaoga basi utakunywa!