William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,584
- 10,466
1. M/S REAL ENERGY (UK).
2. M/S AGGREKO INTERNATIONAL (U.A.E.).
3. M/S RICHMOND DEVELOPMENT COMPANY LLC (USA).
4. M/S REMCP SPA (ITALY).
5. M/S APGUM CO. LIMITED (GERMANY).
6. M/S GLOBELEO LTD (UK).
7. GAPCO (T) LTD (TANZANIA).
8. M/S QUANTUS (GERMANY).
TANESCO, iliunda kamati ya tathmini (Evaluation Committee), yenye watu kumi na mbili (12). Wajumbe nane kutoka TANESCO, Mjumbe mmoja toka Wizara ya Nishati, Mjumbe mmoja toka Wizara ya Fedha, Wajumbe wawili toka Kampuni ya Ushauri ya Lahmeyer International (GERMANY) ambayo kwa kisheria na kawaida ni kampuni ya ushauri kwa TANESCO.
Lakini baada ya mchujo wa kwanza, katika kutathmini makampuni hayo manane (8), makampuni yote hayo nane yalionekana kama kukosa sifa kulingana na vigezo ambavyo vilikuwa vimewekwa na TANESCO, na ndipo Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO iliiiagiza Bodi ya Zabuni ya TANESCO kufanya International Shopping. Kutokana na hali ya dharura na uharaka wa kutatua tatizo la umeme, serikali iliona kwamba utaratibu wa kupata mzabuni kwa njia ya International Shopping bado ungechelewesha mchakato, hivyo Waziri mkuu aliunda kamati maalum ya viongozi watatu (3).
..........to be continued.........!
Jamani tatizo la Richmond ni nini?
1. Wameleta genereta
2. Bei yao ni nafuu
Hivyo sioni hizo kampuni nyingine zingefanya nini zaidi. Ukubwa wa kampuni si sababu ya huduma nzuri kinacho zingatiwa ni mahitaji ya wananchi kwa bei nafuu.
Tatizo ambalo Tanesco imefanya siyo kuchagua kampuni ndogo kwani genereta si kitu ambacho ni lazma kampuni iwe kubwa, lakini tatizo ni kwamba Tanesco na serikali ingeweza kununua hiyo genereta yenyewe kutoka kiwandani bila kupitia wabia ambao ni namna nyingine ya kula rushwa. Watu serikalini wanatumia ubia ili waweze kula rushwa kwani ni vigumu sana hawa wala rushwa wakaenda kuhonga kampuni kubwa kama GE. Hata kama tenda ingetolewa kwa kampuni kubwa bado rushwa ingeliwa kwani tatizo ni namna tender zinavyotolewa na si kampuni inayopewa. Kumekuwa na maneno mengi sana kwamba Richmond haina uwezo lakini je ni uwezo gani? Richmond haijaombwa wataalamu bali genereta na kununua genereta hakuhitaji uwezo wowote zaidi ya pesa, hivyo kwa mtu yeyote mwenye pesa na anajua ni genereta gani inahitajika basi angeweza kutoa huduma hiyo. Ndiyo Richmond inarushwa lakini imekuwa wazi kwa sababu mwenye kampuni ni Mtanzania na watu wanaongea lakini kila tender ya Tanzania ina rushwa Rada, Madini, Ndege ya raisi n.k. Mfano mzuri ni ndege la raisi hiyo ndege mpya ukienda hapo Geogia kwenye kampuni ya Gulf Stream ndege mpya kama ya raisi ni $10m hata kama uki customize haiwezi kuzidi $20m sasa inawezekana vipi imeuzwa $40m bei ya boeing 703? ni kwa sababu ya tender na tender ni njia ya rushwa kila mtu anajua hivyo hata raisi. Kwa nini wasingeweka deal wenyewe na wakalipia gharama za kuipeleka nyumbani kwani hiyo service ipo lakini ni rushwa. Hivyo Watanzania wenzangu tusiishie kuisema richmond kama wenyewe tu ndiyo wabaya kila tender Tanzania ina rushwa, na Richmond watu wamekuja juu kwa sababu ni Mtanzania. Richmond ni hafadhali kuliko deal nyingine kwa ingawa ameonga ni mtanzania na gharama yake ni nafuu lakini hizo deal nyingine zilikuwa over-priced. Hivyo kama tunataka kutatua tatizo tuanzie kwenye mizizi ndugu zangu.
Lakini baada ya mchujo wa kwanza, katika kutathmini makampuni hayo manane (8), makampuni yote hayo nane yalionekana kama kukosa sifa kulingana na vigezo ambavyo vilikuwa vimewekwa na TANESCO, na ndipo Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO iliiiagiza Bodi ya Zabuni ya TANESCO kufanya International Shopping. Kutokana na hali ya dharura na uharaka wa kutatua tatizo la umeme, serikali iliona kwamba utaratibu wa kupata mzabuni kwa njia ya International Shopping bado ungechelewesha mchakato, hivyo Waziri mkuu aliunda kamati maalum ya viongozi watatu (3).