Mtu wa Mungu
JF-Expert Member
- Nov 9, 2010
- 444
- 19
WanaJF hivi focus ni kuzuia malipo ya Dowans, au ni pamoja na Kuondoa mzizi wa janga la taifa kuangamizwa na mafisadi?
Bila kuweka wazi dira katika masuala haya nyeti kwa maslahi ya taifa, matokeo yatakuwa ni malumbano endelevu, na kila kukicha mafisadi wanabuni mbinu mpya za kuendelea kulididimiza na hatimaye kuliteka na kulitawala taifa hili!
Hivi kweli tunaelewa nani hasa kinara, aliye nyuma ya masakata haya yote, ambayo kwa miaka sasa yamelitikisa taifa hili? Mara EPA, mara Meremeta, mara Kagoda, mara Richmond, mara SONGAS, mara Dowans, nk; na yote haya barabara zake zote zinaelekea kwenye chama tawala; na vinara wake, hata wale usioweza kuwatarajia wako kimyaaa!
Ni bora kumfahamu adui, vinginevyo itabaki wakati wote kuwa ni mchezo wa paka na panya!!!!!!!!!!!!!!!!! Taifa lisisahau kuwa siku zote majuto ni mjukuu!
Bila kuweka wazi dira katika masuala haya nyeti kwa maslahi ya taifa, matokeo yatakuwa ni malumbano endelevu, na kila kukicha mafisadi wanabuni mbinu mpya za kuendelea kulididimiza na hatimaye kuliteka na kulitawala taifa hili!
Hivi kweli tunaelewa nani hasa kinara, aliye nyuma ya masakata haya yote, ambayo kwa miaka sasa yamelitikisa taifa hili? Mara EPA, mara Meremeta, mara Kagoda, mara Richmond, mara SONGAS, mara Dowans, nk; na yote haya barabara zake zote zinaelekea kwenye chama tawala; na vinara wake, hata wale usioweza kuwatarajia wako kimyaaa!
Ni bora kumfahamu adui, vinginevyo itabaki wakati wote kuwa ni mchezo wa paka na panya!!!!!!!!!!!!!!!!! Taifa lisisahau kuwa siku zote majuto ni mjukuu!