View attachment 3552819
Makamu Mwenyekiti mstaafu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar, Said Issa Mohamed akiongea na Waandishi wa Habari, leo Machi 5 akizungumzia mazingira ya kisiasa nchini ameeleza kuwa kitendo cha CHADEMA kutoshiriki uchaguzi mkuu kimepelekea chama kujikwamisha, kwani ili chama kiweze kujipima lazima kishiriki chaguzi, ameongeza kuwa hali hiyo imepelekea viongo wengi waliokuwa na ndoto na matarajio waondoke kwenye chama.
Pia soma
Said Mohamed: Kesi ya mgawanyo wa mali za chama niliyofungua ina baraka za viongozi wa CHADEMA Zanzibar
Ni hivi tu umemaliza kuandika yote au bado unaendelea....?
By the way, fahamu haya:
1.
Said Issa Mohammed sio kiongozi (makamu mwenyekiti) mstaafu wa CHADEMA kwa kuwa hakuwahi kustaafu bali alishindwa kwenye uchaguzi huru, wa haki na wa wazi kabisa. Kwa hiyo status ya huyo Saidi Issa Mohammed ni "
aliyeshindwa kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi.."
2. Viongozi wastaafu (yaani wale walioacha kuwa viongozi rasmi wa CHADEMA) kwa utashi na hiari yao, sio wajinga, wapumbavu, wenye chuki na roho mbaya ya kutaka kuharibu au kukivuruga CHADEMA kama alivyo
Said Issa Mohammed na wenzake. Hawa wamejaa tamaa ya uchu wa madaraka wa kutaka "wawe wao tu". Na kwa kuyakosa, kwa tamaa zao hizohizo, maadui na wapinzani wa CHADEMA wakaiona hiyo fursa ya udhaifu wao na hivyo wakajiuza na kuuza utu na heshima yao wenyewe kwa shekeli (hongo) kwa maadui wa CHADEMA ili watumike kama rungu la kujaribu kuiponda CHADEMA na kuisambaratisha. Lakini Mungu wa mbinguni sio
Said Issa Mohamedi wala
Anna Komu kwamba wanaweza kumhonga ili abariki ushenzi wa uovu wao. WAMESHINDWA NA WATASHINDWA TENA NA TENA...!!
3. Hakukuwa na uchaguzi 2025 bali kulikuwa na uchafu na mauaji ya halaiki ili Samia na wauaji wenzake wajitangaze washindi...!
4. Na mwisho, hakuna kipimo cha chama cha siasa kujipima kwa kutumia aina ya uchafu unaoitwa uchaguzi wa 2025. Hata hao waliokimbilia vyama vingine, chini ya mfumo wa kisheria na kikanuni wa uchaguzi walioushiriki walipata nini? Sio kwamba hata hawajui walipata kura ngapi japo walikuwa wagombea...?
5. MWISHO KABISA: Mlipaswa kuelewa slogan ya
CHADEMA ya
NO REFORMS NO ELECTION ilikuwa na maana gani. Huwezi kushiriki kula mavi au kinyesi halafu baadae ulalamike unaumwa tumbo la kuhara - kipindupindu. Wewe utakuwa mjinpga bila shaka. Ndivyo walivyokuwa wale G55 ambao hawakuyaona matatizo ya mfumo wa chaguzi zetu ili washiriki kwanza kushinikiza marekebisho ya kisheria, kikanuni na kikatiba ili kutengeneza uwanja sawa wa uchaguzi kwa kila washiriki/wagombea. Lakini wao kwa ujinga wao wakajipeleka wenyewe machinjioni na wamechinjwa kwelikweli...!!