*SAHARA MEDIA GROUP NI MFUPA ULIOISHINDA SERIKALI*
Kwanza kabisa naomba mfahamu fika kuwa mpaka sasa kampuni ya Sahara media group inayobeba vyombo vya habari vya Radio free Africa, kiss fm na Startv, inasimamiwa na kuendeshwa na mdogo wa mmiliki wa kampuni hiyo Samwel Nyalla. Mabadiliko haya ya kiuongozi yanafuata baada ya mmiliki wa kampuni hiyo ndugu Diallo kushindwa kuhimili mikimiki inayosukumwa na waliokuwa wafanyakazi wa kampuni hiyo kila mara walipotia kambi katika kampuni hiyo kushinikiza kulipwa stahiki za malimbikizo ya mishahara hiyo.
Hapa naomba muelewe kitu kimoja, mabadiliko haya ya Uongozi ndani ya sahara media ni ujanja ujanja unaofanywa na kampuni hiyo kutaka kukwepa na kuchelewesha zaidi malipo ya wadai hao ambao mpaka sasa wameweka kambi mbele ya ofisi za mdogo wa Diallo aitwaye Samwel Nyalla. Mpaka sasa maandika waraka huu leo ni siku ya 17 wadai hao wanalala nje tangu walipoingia kambini tarehe 22 mwezi July.
Sasa kwa wasio mfahamu Samwel Nyalla ni kwamba huyu ni mtu ambaye ana kiburi, nyodo na majibu ya kunya kila mara wadai wa kampuni hiyo wanapozungumza naye. Huyu bwana Alisha kaa kikao na wadai nakuomba apewe mwaka ili ajipange namna ya kulipa na alipoambiwa ni mda mrefu sana aliwajibu wadai hao kuwa “sina pesa na kampuni haina pesa hivyo nikazinye na nikiamua kutowalipa mtanifanya nini”. Sasa kwa mtu mwenye akili haya sio majibu ya kuwapa watu wanaokudai kwa zaidi ya miaka mitatu mpaka sasa. Kinachotia wasiwasi ni Bwana Nyalla kujiapiza kuwa *over my dead body sitawalipa*, sasa tunajiuliza anajiamini nini? Tunaodai tuna uadui gani na Rais Magufuli kiasi kwamba serikali ielekeze tusilipwe? Kwanza miongoni mwa wafanyakazi tupo tuliokuwa timu Magufuli hata kabla hajachukua fomu ya kugombea kuliko Diallo ambaye mpaka sasa anaamini Rais wa moyo wake ni Membe.
Hivi karibuni juma moja limepita kumekuwa na matukio kadhaa baina ya Samwel Nyalla na wadai wake walioweka kambi. Moja ni Nyalla kuamuru wafanyakazi hao kutolewa nje na kampuni ya ulinzi na akaamuru kuwa atayegoma wao wachinje tu na mmoja wa wadai alipogoma getini Nyalla aliamuru walinzi akisema “mkate”. Baada ya hapo Samwel Nyalla aliona kimbembe kinaweza kutokea na wadai wamegoma akatuma apewe bastola anayomiliki akijihami na kutoa shutuma kuwa wadai wanataka kumdhuru jambo la uongo maana walikuwa wamelala kwenye magodoro nje ya ofisi yake.
Baada ya hapo Samwel Nyalla aliwakalipia walinzi akidai wameshindwa kazi na akaamuru waende kushitaki polisi ambapo walienda kutoa taarifa Viongozi wa Kampuni ya ulinzi ya *MASA* na jibu walilopewa ni kwamba mwenye wajibu wa kwenda kushitaki ni Nyalla walipobrudisha majibu hayo Nyalla hakukanyaga polisi hadi leo hii ambapo anaogopa kwenda kutokana na makubaliano aliyoingia na wadai mbele ya OCD Makubi kuahidi angewalipa wadai wote toka mwaka jana mwezi wa kumi na mbili jambo ambalo hajatekeleza na aliambiwa atakapo piga simu tena polisi watakuja kuwachukua wadai na mdaiwa jambo analoogopa mpaka muda huu kutoa taarifa
Siku ya 28/07/2019 RPC wa mkoa alikuwa na kipindi cha Tuongee Asubuhi ambapo baada ya Walinzi wa Sahara media waligoma kufungua geti ili aingie wakimwomba apite geti jingine lakini RPC aligo akawaamuru wafungue geti akihoji “kwanini nizunguke na hapa mnaficha nini”?. Walipofungua geti alikwenda kufanya kipindi na kuondoka kumbe kilicho kuwa kina fichwa ni RPC asione magodoro na net za wadai na hii ni kwa wageni wote wanao kuja Sahara Media kwa sasa.
Samwel Nyalla alipoona amebaki na kimbebe akaamua kubadili kampuni ya ulinzi wiki iliyopita na kuweka kampuni ya shemeji yake, yaani mume wa dada yake inayoitwa *HOME KK LINK LTD* na kuamuru yeyote atakayetoka kati ya wadai hao basi asirudi tena ndani, sasa unajiuliza hawa watu unawafungia nje hutaki kuongea nao wanadai vipi pesa zao? Mara kwa mara amekuwa akijinadi kuwa hakuna wa kumfanya lolote maana yuko karibu na Rais na ndio maana kampuni yake haiguswi inapeta tu. Tarehe 3 August Bashiru Ally katibu mkuu CCM Taifa meenda tena Mwanza lakini mpaka sasa inaonesha dhahiri hata yeye hana nguvu ya ushawishi kusaidia wadai hao kulipwa na mmiliki wa kampuni hiyo ambaye pia ni mwenyekiti CCM mkoa wa Mwanza Anthony Diallo.
Lakini juzi alipomaliza kipindi kaatika kituo cha Startv Bashiru Ally alisimamishwa tena na wadai hao alipokuwa akitoka naakaonesha dhahiri kusikitishwa na watu hao wanao lala nje na ameahidi kumtafuta mmiliki ndugu Anthony Diallo ili kulitatua tatizo hilo, swali langu, Bashiru Ally alisimamishwa kwa mara ya pili na watu walewale kwa tatizo lilelile, Je atalitatua kweli au ndio anapotea kama mara ya kwanza?. Kinacho sikitisha zaidi ni maboss wa kampuni hiyo kujilipa na kuacha wafanyakazi wakidai, wamejijali wao kwanza nakuwasahau wanaowatumikia.
Kwa taarifa zilizopo Samwel Nyalla na Mwanaye Emmanuel Nyalla wanafatilia kubadilisha pass za kusafiria nje ya nchi. Nyalla anaongoza kwenda India anakopatiwa matibabu kila mara lakini haoni umuhimu wa hospital za Tanzania na hivyo kuamua kutumia mamilioni ya fedha kwenda nje na waliokuwa watumishi wake kuendelea kutaabika na mbu nje ya ofisi yake huku yeye akitibiwa kwa pesa za kampuni na mpaka mahitaji yake yeye na familia yake kampuni ina muhudumia kuanzia ununuzi wa gesi ya kupikia mpaka kumlipa msichana wake wa kazi lakini wafanyakazi wanao fanya kazi ili mambo yake yaende amekuwa akiwajibu ovyo.
Nyalla ana hofu sana na sasa ameamuru wafanyakazi wote wapaki magari nje.
Kwa sasa kuna kubambikwa kesi muda wowote baada ya waliokuwa wafanyakazi hao ambao wameweka kambi kuamka alfajiri na kukuta Nyungu, mayai na njiwa ambayo wanadai kuwa waliweka kwenye mlango wa kupitia Samwel Nyalla. Wadaihao wanahofu kuwa kuna mpango mkubwa sana umepangwa kuhakikisha wanatoka kambini hapo hata kwa karandinga ili kuondoa aibu hiyo, lakini kampuni imesahau kuwa imeweka camera za ulinzi kila kona na eneo walilokaa wadai na kulala camera zinaona kila kitu na hawatoki kwenda kwingine zaidi ya hapo.
Mwisho, nimekuwa nikisoma waraka nyingi sana juu ya tatizo hili lakini sahara media group inaonekana ni mfupa uliomshinda Mh.Jenista Mhagama waziri anayehusika na masuala ya ajira, mfupa huu pia umemshinda baba wa tasnia ya habari waziri mwenye dhamana ameshindwa hata kutoa tamko kwa wanahabari hawa wanaoteseka. Mh. Mwakyembe ajipime haiwezekani miaka yote hii ya madai amekaa kimya tu kanakwamba halioni hili.
Pongezi ziende kwa jeshi la polisi mkoa wa Mwanza RPC, OCD MAKUBI ambao wamelifatilia suala hili kwa karibu, wanataarifa za watu hawa na wanajua kuwa hawana madhara na ni watu wa amani na mara kwa mara polisi wamekuwa wakiiomba kampuni kulimaliza tatizo maana hata wao linawakera. Polisi Mwanza Mungua wabariki kwa utendaji haki maana katu hamkutumia nguvu na naambiwa mmekuwa mkikaa na kuzungumza kwa amani na pande zote. Barikiwa sana.
Kwanza kabisa naomba mfahamu fika kuwa mpaka sasa kampuni ya Sahara media group inayobeba vyombo vya habari vya Radio free Africa, kiss fm na Startv, inasimamiwa na kuendeshwa na mdogo wa mmiliki wa kampuni hiyo Samwel Nyalla. Mabadiliko haya ya kiuongozi yanafuata baada ya mmiliki wa kampuni hiyo ndugu Diallo kushindwa kuhimili mikimiki inayosukumwa na waliokuwa wafanyakazi wa kampuni hiyo kila mara walipotia kambi katika kampuni hiyo kushinikiza kulipwa stahiki za malimbikizo ya mishahara hiyo.
Hapa naomba muelewe kitu kimoja, mabadiliko haya ya Uongozi ndani ya sahara media ni ujanja ujanja unaofanywa na kampuni hiyo kutaka kukwepa na kuchelewesha zaidi malipo ya wadai hao ambao mpaka sasa wameweka kambi mbele ya ofisi za mdogo wa Diallo aitwaye Samwel Nyalla. Mpaka sasa maandika waraka huu leo ni siku ya 17 wadai hao wanalala nje tangu walipoingia kambini tarehe 22 mwezi July.
Sasa kwa wasio mfahamu Samwel Nyalla ni kwamba huyu ni mtu ambaye ana kiburi, nyodo na majibu ya kunya kila mara wadai wa kampuni hiyo wanapozungumza naye. Huyu bwana Alisha kaa kikao na wadai nakuomba apewe mwaka ili ajipange namna ya kulipa na alipoambiwa ni mda mrefu sana aliwajibu wadai hao kuwa “sina pesa na kampuni haina pesa hivyo nikazinye na nikiamua kutowalipa mtanifanya nini”. Sasa kwa mtu mwenye akili haya sio majibu ya kuwapa watu wanaokudai kwa zaidi ya miaka mitatu mpaka sasa. Kinachotia wasiwasi ni Bwana Nyalla kujiapiza kuwa *over my dead body sitawalipa*, sasa tunajiuliza anajiamini nini? Tunaodai tuna uadui gani na Rais Magufuli kiasi kwamba serikali ielekeze tusilipwe? Kwanza miongoni mwa wafanyakazi tupo tuliokuwa timu Magufuli hata kabla hajachukua fomu ya kugombea kuliko Diallo ambaye mpaka sasa anaamini Rais wa moyo wake ni Membe.
Hivi karibuni juma moja limepita kumekuwa na matukio kadhaa baina ya Samwel Nyalla na wadai wake walioweka kambi. Moja ni Nyalla kuamuru wafanyakazi hao kutolewa nje na kampuni ya ulinzi na akaamuru kuwa atayegoma wao wachinje tu na mmoja wa wadai alipogoma getini Nyalla aliamuru walinzi akisema “mkate”. Baada ya hapo Samwel Nyalla aliona kimbembe kinaweza kutokea na wadai wamegoma akatuma apewe bastola anayomiliki akijihami na kutoa shutuma kuwa wadai wanataka kumdhuru jambo la uongo maana walikuwa wamelala kwenye magodoro nje ya ofisi yake.
Baada ya hapo Samwel Nyalla aliwakalipia walinzi akidai wameshindwa kazi na akaamuru waende kushitaki polisi ambapo walienda kutoa taarifa Viongozi wa Kampuni ya ulinzi ya *MASA* na jibu walilopewa ni kwamba mwenye wajibu wa kwenda kushitaki ni Nyalla walipobrudisha majibu hayo Nyalla hakukanyaga polisi hadi leo hii ambapo anaogopa kwenda kutokana na makubaliano aliyoingia na wadai mbele ya OCD Makubi kuahidi angewalipa wadai wote toka mwaka jana mwezi wa kumi na mbili jambo ambalo hajatekeleza na aliambiwa atakapo piga simu tena polisi watakuja kuwachukua wadai na mdaiwa jambo analoogopa mpaka muda huu kutoa taarifa
Siku ya 28/07/2019 RPC wa mkoa alikuwa na kipindi cha Tuongee Asubuhi ambapo baada ya Walinzi wa Sahara media waligoma kufungua geti ili aingie wakimwomba apite geti jingine lakini RPC aligo akawaamuru wafungue geti akihoji “kwanini nizunguke na hapa mnaficha nini”?. Walipofungua geti alikwenda kufanya kipindi na kuondoka kumbe kilicho kuwa kina fichwa ni RPC asione magodoro na net za wadai na hii ni kwa wageni wote wanao kuja Sahara Media kwa sasa.
Samwel Nyalla alipoona amebaki na kimbebe akaamua kubadili kampuni ya ulinzi wiki iliyopita na kuweka kampuni ya shemeji yake, yaani mume wa dada yake inayoitwa *HOME KK LINK LTD* na kuamuru yeyote atakayetoka kati ya wadai hao basi asirudi tena ndani, sasa unajiuliza hawa watu unawafungia nje hutaki kuongea nao wanadai vipi pesa zao? Mara kwa mara amekuwa akijinadi kuwa hakuna wa kumfanya lolote maana yuko karibu na Rais na ndio maana kampuni yake haiguswi inapeta tu. Tarehe 3 August Bashiru Ally katibu mkuu CCM Taifa meenda tena Mwanza lakini mpaka sasa inaonesha dhahiri hata yeye hana nguvu ya ushawishi kusaidia wadai hao kulipwa na mmiliki wa kampuni hiyo ambaye pia ni mwenyekiti CCM mkoa wa Mwanza Anthony Diallo.
Lakini juzi alipomaliza kipindi kaatika kituo cha Startv Bashiru Ally alisimamishwa tena na wadai hao alipokuwa akitoka naakaonesha dhahiri kusikitishwa na watu hao wanao lala nje na ameahidi kumtafuta mmiliki ndugu Anthony Diallo ili kulitatua tatizo hilo, swali langu, Bashiru Ally alisimamishwa kwa mara ya pili na watu walewale kwa tatizo lilelile, Je atalitatua kweli au ndio anapotea kama mara ya kwanza?. Kinacho sikitisha zaidi ni maboss wa kampuni hiyo kujilipa na kuacha wafanyakazi wakidai, wamejijali wao kwanza nakuwasahau wanaowatumikia.
Kwa taarifa zilizopo Samwel Nyalla na Mwanaye Emmanuel Nyalla wanafatilia kubadilisha pass za kusafiria nje ya nchi. Nyalla anaongoza kwenda India anakopatiwa matibabu kila mara lakini haoni umuhimu wa hospital za Tanzania na hivyo kuamua kutumia mamilioni ya fedha kwenda nje na waliokuwa watumishi wake kuendelea kutaabika na mbu nje ya ofisi yake huku yeye akitibiwa kwa pesa za kampuni na mpaka mahitaji yake yeye na familia yake kampuni ina muhudumia kuanzia ununuzi wa gesi ya kupikia mpaka kumlipa msichana wake wa kazi lakini wafanyakazi wanao fanya kazi ili mambo yake yaende amekuwa akiwajibu ovyo.
Nyalla ana hofu sana na sasa ameamuru wafanyakazi wote wapaki magari nje.
Kwa sasa kuna kubambikwa kesi muda wowote baada ya waliokuwa wafanyakazi hao ambao wameweka kambi kuamka alfajiri na kukuta Nyungu, mayai na njiwa ambayo wanadai kuwa waliweka kwenye mlango wa kupitia Samwel Nyalla. Wadaihao wanahofu kuwa kuna mpango mkubwa sana umepangwa kuhakikisha wanatoka kambini hapo hata kwa karandinga ili kuondoa aibu hiyo, lakini kampuni imesahau kuwa imeweka camera za ulinzi kila kona na eneo walilokaa wadai na kulala camera zinaona kila kitu na hawatoki kwenda kwingine zaidi ya hapo.
Mwisho, nimekuwa nikisoma waraka nyingi sana juu ya tatizo hili lakini sahara media group inaonekana ni mfupa uliomshinda Mh.Jenista Mhagama waziri anayehusika na masuala ya ajira, mfupa huu pia umemshinda baba wa tasnia ya habari waziri mwenye dhamana ameshindwa hata kutoa tamko kwa wanahabari hawa wanaoteseka. Mh. Mwakyembe ajipime haiwezekani miaka yote hii ya madai amekaa kimya tu kanakwamba halioni hili.
Pongezi ziende kwa jeshi la polisi mkoa wa Mwanza RPC, OCD MAKUBI ambao wamelifatilia suala hili kwa karibu, wanataarifa za watu hawa na wanajua kuwa hawana madhara na ni watu wa amani na mara kwa mara polisi wamekuwa wakiiomba kampuni kulimaliza tatizo maana hata wao linawakera. Polisi Mwanza Mungua wabariki kwa utendaji haki maana katu hamkutumia nguvu na naambiwa mmekuwa mkikaa na kuzungumza kwa amani na pande zote. Barikiwa sana.