Suala la usafiri wa Mtwara mkuu lilishajadiliwa humu jf,labda kama unaenda kuangalia uwezekano wa kutoka kwa gesi,maana hata hapo unapotokea nna mashaka umetumwa..NENDA KAMANDA,ITATOKA TU.!
Mkuu tafuta hiyo thread humu ipo tena haina hata mwezi mzima tangu ibandikwe. Na ina mengi kuhusu mtwara mpaka majina ya mabasi na kiwango cha nauli tena hizi mpya.
Karibu Mtwara Mkuu! Huku mgeni salamu ni.... Itatoka? Tafadhali jibu "haitoki" vinginevyo balaa litakupata. Kwa kifupi jaribu kujiepusha na mijadala ya kuhusu gesi hasa ukiwa mgeni hata kama msimamo wako ni kama wa kwao. Mpaka watakapokuwa na imani kuwa wewe si mamluki.
Ingia website ya SUMATRA utaona bei elekezi, ila ni kati ya 20,000 hadi 30,000.
Basi zuri na linalowahi kufika ni Buti La Zungu, lakini unaweza pia wacheck na Royal Coach au Machinga.
Kwa kukata ticket nenda Temeke Mwisho au hata Ubungo Bus Terminal.
Suala la usafiri wa Mtwara mkuu lilishajadiliwa humu jf,labda kama unaenda kuangalia uwezekano wa kutoka kwa gesi,maana hata hapo unapotokea nna mashaka umetumwa..NENDA KAMANDA,ITATOKA TU.!