Safari yangu ya Machimbo Msumbiji

Safari yangu ya Machimbo Msumbiji

GAZETI

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2011
Posts
5,292
Reaction score
6,769
Zilikuja taarifa kuwa Kuna madini yamegunduliwa Mozambique na watu wengi wanakimbilia huko, Rafiki zangu kadhaa na watu wengi ninao wafahamu waliacha shuguli zao na kuingia kwenye Mkumbo huo, wengi wao walirudi kimya kimya na kujikita kwenye shuguli zao bila hata kueleza kilichojiri huko.

Hiyo ilikuwa ni miaka kadhaa nyuma, Mwaka 2012 mwishoni kijana mmoja ambaye nilikuwa namtumia sana kwenye shuguli zangu za kusafisha Mabanda ya Kuku n.k aliniomba ruhusa ya kwenda Mozambique kujaribu bahati yake, hii ilikuwa ni baada ya tetesi za kugungulika madini ya RUBI katika eneo la MTIPWEZI. Safari hii utitiri wa Vijana ambao walikuwa wanamiminika kuelekea eneo hilo ulikuwa ni mkubwa zaidi. Tofauti na Mwanzo safari hii wengi walirudi na majibu mazuri, wengi walirudi wakiwa wamepata kati ya 5,000,000 mpaka milioni 50.

Yuko Mtu mmoja ambaye alielekea huko kama kuficha fedheha yake baada ya kufumaniwa na Mke wa Mkuu wa kituo cha polisi, yeye alirudi meno nje baada ya kuambulia dola15,000 huku akisahau yale yote ambayo yalimkuta, lakini kubwa ni kwa huyu aliyekuwa mfanyakazi wangu ambaye aliweza kupata kiasi cha Shilingi milioni 80. Aliporudi alikuja kunishukuru na kuniachia shilingi milioni 2. Kitendo cha kijana huyo ambaye alikuwa choka mbaya kurudi na mafanikio makubwa kiasi hicho kilimshawishi rafiki yangu wa karibu ambaye anamiliki Mashamba, mifugo, duka la spea za pikipiki na mashine ya kusaga naye kujaribu bahati yake.

Waliondoka watu wanne, ilimchukuwa wiki mbili tu naye kurudi akiwa na kiasi cha shilingi milioni 140 baada ya mgao wa watu watatu kufuatia kifo cha mwenzao mmoja ambaye alifia hukohuko akiwa shimoni.

Ikafika zamu yangu, Niliondoka mwezi wa kwanza 2014 kuelekea MTIPWEZI nilipitia Kilambo Mtwara pale tulivushwa na boti kwa Tsh 10,000 (ukivuka na pantoni ni tsh 500 (mia tano)) Tukafika eneo maarufu la uhamiaji la msumbiji linaloitwa NAMOTO, nikiwa na pasport yangu ya ujirani mwema lakini wewe kama unataka kwenda kwa kutokea huku Tanzania ni rahisi zaidi ukipitia Chikongo (uliza tu) nilipita vijiji kadhaa kama Kiyonga hadi kutokea wilaya ya Palma, hapo nilipumzika kwa siku moja kabla ya kuendelea na safari iliyonifikisha Musimbwa.

Nilipumzika Musimbwa kwa siku mbili kabla yakuendelea na safari, Nilikuwa peke yangu sikuongozana na yeyote yule, wenyeji wangu walinieleza ugumu wa ninakoenda lakini wakanipa moyo kuwa wengi hufanikiwa huko ingawa wao hakuna aliyejaribu bahati hiyo.

.Baada ya mapumziko hayo jiooni ya siku iliyofuata nikaingia Rasmi eneo la machimbo linalojulikana kama MTIPWEZI, Miongoni mwa vitu ambavyo vilinisisimua ni kukutana na rafiki yangu ambaye tuliachana mara ya mwisho baada ya kumaliza Darasa la saba, ni miaka mingi wengi walikuwa hawajui yuko wapi lakini nimemfuma huko, yeye alikuwa wa kwanza kunitambua na kustaajabu baada ya kuniona nikiwa na kitambi (Nimeanza kukiondoa) hakujua kuwa licha ya kitambi changu nina mazoezi ya kutosha kuweza kupiga kazi za kuchimba

Siku ya pili nikaanza kazi baada ya kujiunga na watu wanne ambao nilikutana nao huko, wawili walikuwa ni wa Msumbiji, mmoja Mtanzania na yule mwingine alikuwa anatoka Zimbabwe, miongoni mwa maswali niliyoulizwa ni kama nilikuja na dawa yoyote ya kunisaidia katika mashimo, nikawajibu kuwa sina walinicheka sana wakisema kuwa nimekuja kitoto, yule mmoja wa Mozambique alinionyesha Korodani za Binadamu alizodai kuwa ni za mjombaake na amekuja nazo ili ziweze Kumsaidia. Sikuuliza kama kamuua au ilikuwaje kwani nilishaingiwa na woga na kundi hili na wala sikutaka kuuliza hao wengine wamefanya nini.

Ilipofika saa mbili usiku tukiwa tuko eneo la machimbo ilisikika milio ya Risasi, Shimo letu halikuwa kubwa sana Hivyo tuliwahi kuchomoka na kukimbia. Watu walikuwa wanakimbia ovyo kunusuru maisha yao wengine walikamatwa na tulionusurika ndio hivyo tena tulijichanganya maporini. Ndugu yangu usifanye mchezo na njaa ya siku mbili. Kitu nilichoambiwa (sijathibitisha) Ni kuwa wale wanaokamatwa huuwawa na kutupwa kwenye mashimo ya madini.

Tulikutana na mambo mengi sana, nafasi haitoshi kusimulia yote hayo, ni katika kisa ambacho nimeshuhudia mwenzetu ambaye tulikimbia naye akiiaga dunia.

Tofauti na Wenzangu mimi nilikuwa na ile TEMPORARY PASPORT hivyo sikupata shida kuingia katika eneo lolote lile. Niliachana na wenzangu katika kijiji kimoja ambako Nyoka huwa wanaliwa sana, wanaitwa CHIDUDU ukisikia chidudu kama huli nyoka acha maana inafanana sana na Samaki.

Kutoka hicho kijiji niliweza kusafiri hadi PALMA, Palma nilikutana na fursa kadhaa ambazo zilinifanya nijaribu kuwashawishi wanaJF humu ndani kuweza kuchangamkia fursa hizo lakini kama kawaida wengi walionekana kutoniamini, nilijua ilikuwa ni vigumu kuniamini lakini ulikuwa ni mpango mzuri ambao wachache ambao walichangamkia Fursa hizo wamefanikiwa sana (sio niliowashawishi mimi)

Mwisho napenda niwaeleze kuwa mafanikio yana mapito yake ambayo ni magumu kweli kweli kwa yeyote ambaye atakutana na mikasa kama hiyo basi hatakiwi kukata tamaa bali azidi kukaza Buti.

NAWATAKIA ASUBUHI NJEMA.
 
Dah unanitisha ndugu yangu maana kuna watu huko wamepotea na hawajulikani waliko mpaka sasa.

ndiyo ujiongeze yani ukienda nenda na mambo mawili kurudi au kutokurudi,,, na siku unaondoka aga kabisa mazima
 
Dah unanitisha ndugu yangu maana kuna watu huko wamepotea na hawajulikani waliko mpaka sasa.

Ndio mambo ya kutafuta Madini kaka

nakumbuka late 90's kuelekea miaka ya 2000, Boom kubwa sana la madini liliibuka Ngapa, Tunduru na kisha Ruangwa, watu waliama kutoka Ulanga na Mahenge kwenye Ruby na kukimbilia kusini kwenye Alexdrite, Green na Red Garnet, Tourmaline, Topaz nk

Palikuwa na Hotel maarufu sana pale Mtwara TINGATINGA sijuhi kama bado ipo, sasa pale ndio ilikuwa fujo kubwa ya wachimba madini walikuwa wanaingia pale kutoka Polini wanavikaptula vya Jeans vilivyochoka huku wakiwa na mabegi ya Mamilioni

Meneja wa Pale hotelini alikuwa anashangaa jamaa wanapata wapi pesa na alipopewa mchongo aliamua kuresign na kuchukua chake (30Mil). Nilikutanana nae Mbekenyera-Nanjaru (Ruangwa) yaliyomkuta siwezi yasema hapa, ila kila siku ya Mungu alikuwa analia kama mtoto mdogo.

ni biashara nzuri sana lakini na risk ni kubwa mno, kutelekeza familia na kupoteza malengo ya kimaisha na kupotelea moja kwa moja kwenye machimbo ni kitu cha kawaida kabisa.
 
Mkuu story yako inafaa uipeleke njia panda,tutafurahi kumsikia mwana jf akifanya kipindi njia panda,
Nina maswali mengi ya kukuuliza lkn anyway ngoja niulize haya machache
1.Ww ulitoka mkoa upi kwenda machimbo.
2.Family yako baada ya kurudi ulikuta wapo ktk Hali gani na wao pia walijiskiaje kukuona.
3.Ulikaa machimbo kwa mda gani kabla ya kurejea Tanganyika
4.Mfanyakazi wako,uliwahi kumuuliza yy alifanikiwaje kule mozambique?
5.Rfk yako aliyepoteza maisha ulijiskiaje,na ulikuwa na mawasiliano yyte na familia yake!?
Hebu ngoja niishie hapa,
Nitoe Dukuduku langu plz.
GAZETI
 
Last edited by a moderator:
Mwaka 2012 nilisafiri kwa ndege kwenda Maputo, safari hii ilikuja baada ya taarifa za kuwa kumekuwa na mauaji ya watanzania wanaochimba madini maeneo ya Mutipwezi (mtipweshi),

Balozi wa Tz kule maputo alinipa ushirikiano mkubwa sana, baada ya siku tatu za kuwepo Maputo safari yangu kuja jimbo la Pemba ilianza na nilitumia usafiri wa Toyota Landcruser mkonga, lipofika Pemba nilionana na Balozi mdogo wa Tz nae akanipa msaada hadi kisiwa cha Vamizi, hapo ndio kituo changu mhimu cha kuelekea mtipweshi kilipokuwa,

Nilifanikiwa kusafiri kwa Boti hadi eneo maarufu wanaloliita RENAMO Camp mahali pa kambi za waasi wa Renamo, ilikuwa kazi ngumu sana kuvuka kikwazo hiki cha makomandoo wa renamo kwakuwa walidhani nimekwenda kuwadukua, lakini mungu mkubwa nilifanikiwa kuwatoka na nikaibukia Msimbwa.

Hapo nilikutana na vijana wa kitz waliokuwa wanaelekea machimboni, nilibahatika kumpata rafiki mmoja Joseph mchaga wa Arusha aliyenisaidia kunipa habari zote za kinachofanyikaga huko machimboni kwakuwa yeye alikuwa ni mzoefu na alikuwa akitoka Tz kwenda huko machimboni.

Tulifika jioni, ajabu tulikaribishwa kwa risasi za moto kutoka kwa askari wa Musumbiji waliovamia makambi na kuanza kupora madini,

Wenzangu walitaka kukimbia, nikawambia tulieni asikimbie mtu, nilishuhudia watu wanne wakipigwa risasi wazi wazi, watatu ni watz na mmoja ni mzambia.

Walitusogelea wakaanza kukagua hati zetu, ilikuwa patashika kweli kweli kwakuwa wengi wa vijana hati zao zilikuwa zimeisha muda wake, kitu cha kusikitisha nikuwa wale polisi walianza kuchanachana pasi za watu wote,

Niliamua kuwauliza kuwa sisi tumeingia nchini mwao kwakufuata taratibu zote na tupo kihalali kwamjibu wa sheria za kimataifa, je haya wanayofanya yanabaraka za serikali yao? (niliuliza kwa kiingereza)

Wakasitisha lile zoezi la kuchana pasi wakanisogelea na kunyang'anya pasi yangu, wakaichana na yule bosi wao akanitemea mate usoni, bahati nilikuwa na PPV

Kisha wakaongia kwenye gari yao na wakasema kwakireno kuwa kesho tena lazima waje,

Siku iliyofuata niliendelea kupata habari za matukio ya Mtipweshi kwa Watz, kama kawaida ya tatu wakaja tena wale askari, siku hiyo walikuta tunaangalia mpira, siku hiyo ndio walimimina risasi na kuchoma mahema ya wachimbaji, nilifanikiwa kukimbilia begi langu na kumshika mkono jamaa yangu Joseph kisha tukaingia mitini,

Tulipofika kwenye kibonde flani nilimwambia jamaa yangu tusimame, ntaka kuwajibu hawa wapuuzi, bahati nzuri na jamaa yangu nae alikuwa na mguu wa kuku, tukajaribu kujibu mapigo,

Daaah jamaa waliposikia mlio wa risasi walishusha mvua ya risasi kwetu, bahati mbaya sisi silaha zilikuwa ndogo, hivyo askari wale walizidi kutusogelea tukaamua kukimbia zaidi na kutokomea hadi msimbwa.

Kesho yake nikamuaga jamaa yangu Joseph nikaanza safari ya kurudi home kupitia boda ya Kilambo hadi mtwara kisha dar,

Ajabu nikuwa serikali ya ccm haijachukua hatua madhubuti kutatua mgogoro huu wa watz huko Msumbiji.
 
Mwaka 2012 nilisafiri kwa ndege kwenda Maputo, safari hii ilikuja baada ya taarifa za kuwa kumekuwa na mauaji ya watanzania wanaochimba madini maeneo ya Mutipwezi (mtipweshi),

Balozi wa Tz kule maputo alinipa ushirikiano mkubwa sana, baada ya siku tatu za kuwepo Maputo safari yangu kuja jimbo la Pemba ilianza na nilitumia usafiri wa Toyota Landcruser mkonga, lipofika Pemba nilionana na Balozi mdogo wa Tz nae akanipa msaada hadi kisiwa cha Vamizi, hapo ndio kituo changu mhimu cha kuelekea mtipweshi kilipokuwa,

Nilifanikiwa kusafiri kwa Boti hadi eneo maarufu wanaloliita RENAMO Camp mahali pa kambi za waasi wa Renamo, ilikuwa kazi ngumu sana kuvuka kikwazo hiki cha makomandoo wa renamo kwakuwa walidhani nimekwenda kuwadukua, lakini mungu mkubwa nilifanikiwa kuwatoka na nikaibukia Msimbwa.

Hapo nilikutana na vijana wa kitz waliokuwa wanaelekea machimboni, nilibahatika kumpata rafiki mmoja Joseph mchaga wa Arusha aliyenisaidia kunipa habari zote za kinachofanyikaga huko machimboni kwakuwa yeye alikuwa ni mzoefu na alikuwa akitoka Tz kwenda huko machimboni.

Tulifika jioni, ajabu tulikaribishwa kwa risasi za moto kutoka kwa askari wa Musumbiji waliovamia makambi na kuanza kupora madini,

Wenzangu walitaka kukimbia, nikawambia tulieni asikimbie mtu, nilishuhudia watu wanne wakipigwa risasi wazi wazi, watatu ni watz na mmoja ni mzambia.

Walitusogelea wakaanza kukagua hati zetu, ilikuwa patashika kweli kweli kwakuwa wengi wa vijana hati zao zilikuwa zimeisha muda wake, kitu cha kusikitisha nikuwa wale polisi walianza kuchanachana pasi za watu wote,

Niliamua kuwauliza kuwa sisi tumeingia nchini mwao kwakufuata taratibu zote na tupo kihalali kwamjibu wa sheria za kimataifa, je haya wanayofanya yanabaraka za serikali yao? (niliuliza kwa kiingereza)

Wakasitisha lile zoezi la kuchana pasi wakanisogelea na kunyang'anya pasi yangu, wakaichana na yule bosi wao akanitemea mate usoni, bahati nilikuwa na PPV

Kisha wakaongia kwenye gari yao na wakasema kwakireno kuwa kesho tena lazima waje,

Siku iliyofuata niliendelea kupata habari za matukio ya Mtipweshi kwa Watz, kama kawaida ya tatu wakaja tena wale askari, siku hiyo walikuta tunaangalia mpira, siku hiyo ndio walimimina risasi na kuchoma mahema ya wachimbaji, nilifanikiwa kukimbilia begi langu na kumshika mkono jamaa yangu Joseph kisha tukaingia mitini,

Tulipofika kwenye kibonde flani nilimwambia jamaa yangu tusimame, ntaka kuwajibu hawa wapuuzi, bahati nzuri na jamaa yangu nae alikuwa na mguu wa kuku, tukajaribu kujibu mapigo,

Daaah jamaa waliposikia mlio wa risasi walishusha mvua ya risasi kwetu, bahati mbaya sisi silaha zilikuwa ndogo, hivyo askari wale walizidi kutusogelea tukaamua kukimbia zaidi na kutokomea hadi msimbwa.

Kesho yake nikamuaga jamaa yangu Joseph nikaanza safari ya kurudi home kupitia boda ya Kilambo hadi mtwara kisha dar,

Ajabu nikuwa serikali ya ccm haijachukua hatua madhubuti kutatua mgogoro huu wa watz huko Msumbiji.

tuna wachimbaji wakitanzania wengi wametolewa kwa nguvu sehemu mbalimbali ndani ya tanzania kwa sababu mbalimbali za kisheria hadi kupelekea vifo vya baadhi ya wachimbaji.
Japo kuna ukweli wa matumizi ya nguvu kupita kiasi stahili kwa majeshi ya msumbiji, watanzania wanaofanya kazi kihalali wapo wengi katika majimbo mbalimbali ndani ya msumbiji na wanafanikiwa kwa kufuata tafatibu zilizowekwa.
 
duh!story zenu nzuri sana
ngoja nisubirie hii movie kwanza
attachment.php
 
Wa tz maf.ala sana hapa hapa bongo kuna madini mengi sana na aina tofauti na mengine huwa yanatoka aina hata 7 kwenye chimbo moja tu tatizo tamaa na utapeli ndio vinavyowaponza mzigo wa rubi ya tunduru hauna tofauti sana na wa msumbiji sasa jiulize upo camp miezi6 na hujafanikiwa bado kisha unasikia kuna chimbo sehemu fulan linatema unaenda haraka wakati hata hapo ulipo ulisikia panatema vile vile.
 
kweli wakuu kuna ndugu yangu alienda huko mwaka jana na mil 2 baada ya mizi 3 akarudi na sh mil 90 yaan hata ac alikuwa hana ikabidi nimuwkee kwenye ac yangu baadae nikatamtolea kidogo kidogo
 
Usinikumbushe ndugu yangu, mimi na mdogo wangu tuliwahi kwenda huko msumbiji sehemu inayo itwa mpepo kwenye machimbo ya madini ya dhahabu mwaka 1993 enzi hizo kuna waasi wa renamo walicho tufanyanyia wale mbwa, ptuuu!! Sina hamu.
 
Usinikumbushe ndugu yangu, mimi na mdogo wangu tuliwahi kwenda huko msumbiji sehemu inayo itwa mpepo kwenye machimbo ya madini ya dhahabu mwaka 1993 enzi hizo kuna waasi wa renamo walicho tufanyanyia wale mbwa, ptuuu!! Sina hamu.

Aiseee!! inaogopesha sana na inahitaji ujasiri.Mkuu Wildfish tujuze waliwatenda nn hao mambwa??dooo!
 
kuna rafiki yangu alikuwa msumbiji na nilikuwa na appointment naye mwezi wa 5 mwaka huu mbeya simu yake haipatikani mpaka leo!
 
habari zenu zinasisimua na kuhuzunisha hapohapo, hebu tupeni kamili kamili mnatuonjesha kidogo tu inatuachia maswali mengi
 
Du kumbe hakufai kwenda huko

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mkuu story yako inafaa uipeleke njia panda,tutafurahi kumsikia mwana jf akifanya kipindi njia panda,
Nina maswali mengi ya kukuuliza lkn anyway ngoja niulize haya machache
1.Ww ulitoka mkoa upi kwenda machimbo.
2.Family yako baada ya kurudi ulikuta wapo ktk Hali gani na wao pia walijiskiaje kukuona.
3.Ulikaa machimbo kwa mda gani kabla ya kurejea Tanganyika
4.Mfanyakazi wako,uliwahi kumuuliza yy alifanikiwaje kule mozambique?
5.Rfk yako aliyepoteza maisha ulijiskiaje,na ulikuwa na mawasiliano yyte na familia yake!?
Hebu ngoja niishie hapa,
Nitoe Dukuduku langu plz.
GAZETI

1. Mimi ni Mwenyeji wa Mtwara lakini nilienda machimbo nikitokea Dar.
2. Walikuwa kawaida kwani sikuaga kuwa naenda machimbo walijua ni safari za kawaida.
3.Machimbo nilikaa muda usiozidi Juma moja na hata niliporudi bado nilikuwa Msumbiji
lakini katika eneo lingine na kwa mambo mengine.
4.Sikumuuliza kwani alichoeleza ni kuchimba tu.
5. Hakuwa rafiki yangu ila mwenzangu katika uchimbaji, ilinihuzunisha.
 
Back
Top Bottom